Wakuu,
1:Kuna watetezi wa Zitto hapa ambao ni genuine wanaona Zitto alionewa ingawa hawasemi kwamba alipewa barua kujulishwa makosa yakw
2:Kuna watetezi Genuine wa Chama hapa wanaotaka katiba ifuatwe na ukuu wa Taasisi uzingatiwe
3:Kuna watetezi wa Zitto hapa ambao sio genuine bali ni maadui wake na maadui wa Chadema.Ni maadui wa upinzani.Kazi ya kuchochea upande wanaoamua
4:Kuna wasiofungamana na upande wowote ila wanapenda haki na upinzani imara usio na doa na migogoro
5:Kuna wasiojua chochochote
6:Kuna ambao hawataki kabisa kuhoji ukweli wa hoja hii aliyoleta mleta mada na wapo kwenye hayo makundi yote hapo juu na hii inaweza kupelekea hata wanachama kukwaruzana
7:Kuna wahusika wakuu katika suala hili nao wako hapa hawatasema kwa ID zao halisi au wanafuatilia kwa karibu bila kujali credibility ya thread.
Kila mmoja awe genuine na azingatie haki na ubora wa mijadala sasa. I'm out!
Hiyo namba 3 ndio mbaya sana, na bahati mbaya watu wengi hawaitambui.Ndio maana unakuta wwngi uishia kusema "mbona anatetewa na CCM?"
Na kundi hili limewaingiza king ata watu wengi wenye akili humu, likijifanya linampenda sana Zitto kumbe lengo ni kuhakikisha Chadema hakipati mshikamano na umoja kati ya viongozi na wanachama kwa kuwatia hasira wale wanachadema wapenzi wa Mbowe au Slaa.