Zitto aitibua CHADEMA

Zitto aitibua CHADEMA

Wakuu,

1:Kuna watetezi wa Zitto hapa ambao ni genuine wanaona Zitto alionewa ingawa hawasemi kwamba alipewa barua kujulishwa makosa yakw

2:Kuna watetezi Genuine wa Chama hapa wanaotaka katiba ifuatwe na ukuu wa Taasisi uzingatiwe

3:Kuna watetezi wa Zitto hapa ambao sio genuine bali ni maadui wake na maadui wa Chadema.Ni maadui wa upinzani.Kazi ya kuchochea upande wanaoamua

4:Kuna wasiofungamana na upande wowote ila wanapenda haki na upinzani imara usio na doa na migogoro

5:Kuna wasiojua chochochote

6:Kuna ambao hawataki kabisa kuhoji ukweli wa hoja hii aliyoleta mleta mada na wapo kwenye hayo makundi yote hapo juu na hii inaweza kupelekea hata wanachama kukwaruzana

7:Kuna wahusika wakuu katika suala hili nao wako hapa hawatasema kwa ID zao halisi au wanafuatilia kwa karibu bila kujali credibility ya thread.

Kila mmoja awe genuine na azingatie haki na ubora wa mijadala sasa. I'm out!

Hiyo namba 3 ndio mbaya sana, na bahati mbaya watu wengi hawaitambui.Ndio maana unakuta wwngi uishia kusema "mbona anatetewa na CCM?"

Na kundi hili limewaingiza king ata watu wengi wenye akili humu, likijifanya linampenda sana Zitto kumbe lengo ni kuhakikisha Chadema hakipati mshikamano na umoja kati ya viongozi na wanachama kwa kuwatia hasira wale wanachadema wapenzi wa Mbowe au Slaa.
 
nyie ndio mamuruki, wachonganishi wakubwa mnajifanya, mnauchungu na chama kumbe ndio mnakiharibu chama, imefika hatua chadema wayamalize na zitto maana umoja pekee ndiyo hazina kuu ya kupambana na mkoloni ccm, zitto ananafasi yake ndani ya chadema na chadema pia kama chama wana nafaasi na mchango mkubwa juu ya zitto, kama kweli waliungana kule bungeni na kupambana na mkoloni mamboleo ambaye ni ccm kwa nn wasiungane tena na kufanya kazi kwa pamoja kama ilivyokuwa mwanza,,,niwaombe zitto na mbowe na chadema kwa ujmla myamalize ili mulete ukombozi mpya ndani ya nchi hii
 
Wakimsamehe Zitto,wawe na tahadhari naye sana.Haaminiki.Akiona pesa hakawii kubadilika.Chunga sana hiyo namba CDM
 
Nilitamani sana na ninatamani sana Zito angerudi CDM. Ila ninwasiwasi mkubwa kwamba ile tabia yake chafu ya kujikweza kuliko mtu yeyote hajaicha. Zito kwa kauli moja achwe aende zake ACT tutakutana bungeni kulisaidia taifa kwenye mada za kitaifa tutamuunga mkono akae huku huko.

Zito bado ana kichwa kisichokuwa tayari kwa muafaka. Akirudi ataanzisha kasheshe jipya. Bado ninaamini kwenye siasa hakuna urafiki wala uadui wa kudumu akifikisha miaka 50 atakuwa kakomaa kiakili na hekima.

Tulikupenda sana ila ulituchukia mno.
Ni sisi wana CDM
 
Mbowe ameogopa masharti ya zitto akijua wazi kuwa yeye ndio mwenye makosa. Kwanini asikubali kutoa ushahidi kama ni kweli zitto ana kosa

I would imagine one of Zitto's terms and conditions would be democracy within chadema it self. That includes the facts that every leadership position should be democratically contested. That is the pill that is too bitter for Muheshimiwa Mbowe to swallow.

Zitto is riding at the crest of the wave at the moment, very popular for the hard work he has done to the country he loves. Now the "opportunists" are ingratiating themselves to Zitto trying to drag him back into chadema so they can claim credits for his accomplishments. Unfortunately Zitto can see through their foolish plans.
 
Dawa yake alishwe sumu tuu huyu Zitto. Kwani yule kijana Ben mbeba sumu wa chadema siku hizi yuko wapi? au kazi imemshinda?
 
MSALANI Pasco & MaCCM Co
Mbona mnangangana Kumrudisha Zito CHADEMA??
Kwani hawezi kufanya siasa nje ya CDM??
Mna maslahi gani kuturudishia msaliti kundini??
Zito hana tija CDM, nihatari sana kukaa na ndumila kuwili!!
Tujenge chama sio kubomoa!!
 
Last edited by a moderator:
Watu humu ndani mnaongea sana.yani hata hukumu mahakanani haitolewi hivi.mtu lazima ajitetee ajue kosa lake kisha Kama kuomba radhi ndio aombe .Na Kama ameonewa je?ndio maana nayeye anataka kuwe na masharti kwenye kurudi.

hahitajiki chadema ....hizi kelele za wapambe wa zitto tu .... atambae zake!
 
Wa TZ, hasa wana Chadema wajinga kweli. Mtu anahoji kosa lake la kuvumiliwa uwanachama imekuwa kero? Mbowe na Slaa ni virusi vya Ebola katika CDM. Zitto alivuliwa uwanachama kwa sababu alionyesha nia ya kugombea uwenyekiti, pili ukanda, tatu dini yake. Baada ya uchaguzi Mbowe alinukuwa akisema ni vigumu CDM kuongozwa na mwislam au CCM kuongozwa na mkristo. Akili na macho ya ziada inaitajika ili uitambue hili.
 
Na vipi wale bendera fuata upepo waliofukuzwa chamani kwa ajili yake kwa kutoa matamshi yasiyo na mshiko,kisa mapenzi binafsi kwa zito. Vipi akina Samson na kitila na vilaza wengine? Sipati picha, ni chenga tu kwenye hii movie. dah!!!
 
Sometimes huwa nina question busara za Zitto. Au ndiyo hiyo mnayosema kwamba anapenda kuabudiwa?!

Hivi ulishaona wapi mtaka msamaha akitoa MASHARTI.

Nikajiuliza suppose hilo sharti alilolitoa Zitto CDM wanalikataa, what next to Zitto? Kweli akili NYINGI HUONDOA MAARIFA.
 
Wa TZ, hasa wana Chadema wajinga kweli. Mtu anahoji kosa lake la kuvumiliwa uwanachama imekuwa kero? Mbowe na Slaa ni virusi vya Ebola katika CDM. Zitto alivuliwa uwanachama kwa sababu alionyesha nia ya kugombea uwenyekiti, pili ukanda, tatu dini yake. Baada ya uchaguzi Mbowe alinukuwa akisema ni vigumu CDM kuongozwa na mwislam au CCM kuongozwa na mkristo. Akili na macho ya ziada inaitajika ili uitambue hili.

Sasa kama ukweli ndiyo huo kwanini basi atake kurudi CDM in the first place?!

Hoja nyingine hata mtoto wa STD I hawezi kuzijenga. Tunarudi kule kule CDM ni chama cha Wakiristu, CUF ni chama cha Waislamu. Sasa wameungana na kufanya UKAWA, Je muungano wa UKAWA ni wa watu gani?

Propoganda nyingine za Ma-CCM ni sawa mchimba kisima ampapo hutumbukia mwenyewe.
 
zitto yuko sahihi ...ataomba msamaha kwa kosa lipi?aambiwe kosa ndipo aombe msamaha.....
 
Hivi ni Zitto ndio ametaka kurudi au viongozi wa CHADEMA ndio wamemtaka arudi???
Hapo sijaelewa nadhan.

Na kama wao ndio wanamtaka arudi, sion ubaya kuwawekea mashart cz mwanzo walimfukuza nw wamemuona amebadilika nini mpk wamtake arudi???
 
Mtu anahoji kosa lake la kuvumiliwa uanachama
Hapa unamaana gani?? [/QUOTE] Baada ya uchaguzi Mbowe alinukuwa akisema ni vigumu CDM kuongozwa na mwislam au CCM kuongozwa na mkristo.[/QUOTE]
Inaonyesha unaongea usilolijua. Aidha umekariri ama umehadithiwa. J.K Nyerere na B. Mkapa walikuwa dini gani?
 
Kamanda sio mpango huo, yani urudishe kadi kwa reason rahisi hivyo? Mimi kadi hii sitoirudisha kamwe, tena ngoja kesho nikalipie na ada ya uanachama kabisa.

Kuendelea kumbembeleza mtu aliyeshiriki ku destruct Chama a Big time ni kukaribisha more Destructions kwenye Chama.
Wacha tusonge,amejua kuwa hii move ya UKAWA sio ya KITOTO,ameipenda,anaitaman anatafuta namna ya kuijoin kiaina.
Mwenzake Kafulila aliomba Msamaha kwa machozi na Magoti,sio yeye anatoa Mashart ya Kipuuzi kabisa.
Ni bora CHADEMA ife kuliko kumuomba MSAMAHA huyu JUHA
To hell
 
Zitto hadi kajengewa barabara kwake, ni Mbunge gani wa upinzani kajengewa barabara kama ZZK. Nataka nijue tu.
 
Jeshi la kuijenga CHADEMA na UKAWA kwa ujumla ni kubwa mno, tena lina vifaa vikali mara 100 ya huyo binti Maringo na Msaliti mkomavu... Tofauti ya Zzk na hilo jeshi ni Exposure tu! Lkn mtaniambia nini kitatokea baada ya 2015 kwa Zzk.

Me najua anachokitafuta sasa ni mahala pa kujishikiza ili angalau aendelee kuwepo kwenye ramani.

Niwakumbushe, kilichomfanya aonekane "mzuri" ni kuisoma taarifa ya kamati ya PAC ambayo ni rejea ya Ripoti za CAG na PCCB. Hivyo hana hata neno lake hata 1 zaidi ya kunukuu ya hizo taasisi.

Lakini mbaya zaidi, ni huyuhuyu Zzk aliyetamka kwamba amezimis harakati! Na akaanzia hapohapo kutafuta huruma.

Huyu ni kidudu Mtu anayetaka kuunyemelea UKAWA alete mvurugo kams aliouleta CHADEMA akakwama.

Say NO! to Traitors
 
Back
Top Bottom