Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, anachukizwa na kitendo cha Zitto Kabwe, mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) la kuweka sharti la kurejesha kundini.
Zitto ambaye alivuliwa nyadhifa zake zote za uongozi mapema mwaka huu, kwa sasa yuko mahakamani akitetea uwanachama wake, baada ya viongozi wenzake wakuu kutishia kutaka kumfukuza.
Habari kutoka ndani ya Chadema zinasema, karibu viongozi wote wa juu wa chama hicho, akiwamo Dk. Willibrod Slaa, wameonyesha nia ya kumsamehe Zitto ili arejee kundini, lakini tatizo lilikuja pale mwanasiasa huyo alipoweka sharti.
Inadaiwa kuwa Mbowe ameweka msimamo mkali baada ya Zitto kutoa kauli inayoonyesha kuwa anataka kuwekwa sharti la yeye kurejea ndani ya chama.
Kulikuwa hakuna tatizo Zitto kusamehewa na kurejea ndani ya chama. Lakini kauli yake kuwa anaweka sharti la kutaka kusamehewa, ndilo limeonekana kumkera mwenyekiti, ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi ndani ya chama ambaye hakupenda kutajwa.
Amesema baada ya Kamati ya Bunge ya PAC inayoongozwa na Zitto kufanya kazi kubwa ya kuchambua ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kisha kuwasilisha mapendekezo yake bungeni, baadhi ya viongozi wa Chadema akiwamo Mbowe na Dk. Slaa walionekana kuwa wako tayari kusamehe yaliyopita, lakini kitendo cha Zitto kuweka sharti kimewaudhi baadhi yao na kumuona kama mtu anayetaka kuabudiwa.
Mapema wiki iliyopita, Zitto alinukuliwa na gazeti la Mwananchi akisema, "hajui kosa" lake na kuweka masharti kwamba pale atakapoambiwa kosa lake yuko tayari kuomba radhi na kurejea Chadema.
Wewe leo unatia aibu tu hapa. Unaelekea kuyala matapishi yako. Angalau kwasasa umeyakaribia na umeshayanusa,ila unaona aibu maana ni mapema mno. unajua ni kwanini leo upo hivo;
1. wewe pamoja na kutumika kooote huaminiki na chama kama Zitto ambaye ulishiriki kumchafua kwa kiasi kikubwa
2. Wewe umejikuta ni majeruhi wa chaguzi za chama wakudumu hivyo hakuna sababu ya kuendelea kua radical dhidi ya Zitto
3. Unalijipenyeza kupitia kichaka cha IPTL/Escrow kumsogelea Zitto na kwa bahati nzuri ana ngozi ngumu na amekusitiri tu
4. Leo ungetamani Zitto arejee CDM kama kawaida na kufanya nae kazi, lkn bado unajiuliza uso wako utauficha wapi??
Nawaza tu kwa sauti!
Wote nyie wapenzi wa zitto iwe kwa kweli au kwa kuchochea mgogoro jamaa yenu alikosa na hawezi kuombwa msamaha,yy ndio anapaswa kuomba msamaha asipoweza aendee chama chote anachotaka, amekuwa kwenye siasa muda mrefu atakuwa anajua kuendesha chama cha siasa sio kuandikwa kwenye magazeti,kama anahekima basi ningemshauri aombe msamaha bado anayonafasi ya kutengeneza alipo bomoa.CHADEMA ndio chama pekee watu wote wanapewa nafasi ya kuonyesha uwezo wao.Ifike wakati watu wote tunaongea humu tuwe wakweli, wabunge wote wa chadema kuunga mkono kamati ya zitto ilitosha kuonyesha hakuna mtu mwenye chuki binafsi naye hatima ya zitto kisiasa iko mikononi mwake mwenyewe
zitto aweke masharti ni mkubwa kuliko chama???????????Mwenyekiti nae anataka kutuaminisha hiki chama ni chake sasa, kwani kuna shida gani wakasameheana kujenga upinzani wenye nguvu, najua Zitto amejutia usaliti wake na sidhani kama atarudia tena, asamehewe tu.
Na wewe ni mpenda vurugu sana.Kundi lako hapo na wewe ni lipi?Wakuu,
1:Kuna watetezi wa Zitto hapa ambao ni genuine wanaona Zitto alionewa ingawa hawasemi kwamba alipewa barua kujulishwa makosa yakw
2:Kuna watetezi Genuine wa Chama hapa wanaotaka katiba ifuatwe na ukuu wa Taasisi uzingatiwe
3:Kuna watetezi wa Zitto hapa ambao sio genuine bali ni maadui wake na maadui wa Chadema.Ni maadui wa upinzani.Kazi ya kuchochea upande wanaoamua
4:Kuna wasiofungamana na upande wowote ila wanapenda haki na upinzani imara usio na doa na migogoro
5:Kuna wasiojua chochochote
6:Kuna ambao hawataki kabisa kuhoji ukweli wa hoja hii aliyoleta mleta mada na wapo kwenye hayo makundi yote hapo juu na hii inaweza kupelekea hata wanachama kukwaruzana
7:Kuna wahusika wakuu katika suala hili nao wako hapa hawatasema kwa ID zao halisi au wanafuatilia kwa karibu bila kujali credibility ya thread.
Kila mmoja awe genuine na azingatie haki na ubora wa mijadala sasa. I'm out!
wewe kama sio mida8 ni yericko na fake id
Kwa hiyo we ulikuwa unasemaje?