mkuu bandiko lako nimelipenda hata mimi naungana nawe 100% sio rahisi kumhujum mwanafunzi kwa kigezo cha dini"
Ndugu yangu
Cheche Mtungi
Mimi by professional ni mwalimu na nafundisha katika moja ya hizihizi shule za Sekondari za kata ktk moja ya wilaya na mkoa kanda ya ziwa.Nina miaka kumi na tano sasa (nimeanza kazi mwaka 1998). Hivyo mm niko field na ninaelewa na nakuelewa sana kwa kila unachoandika na wengine wanajaribu tu kuingiza siasa ktk hii kitu ELIMU. Ndugu yangu tunapambana na mataizo mengi sana ktk kazi yetu hii na hasa ktk awamu hii ya JK!!..
Pamoja na matatizo mengi ya msingi uliyaeleza yanayousonga mfumo wetu wa elimu, mimi pia naona kuna matatizo mengine mawili ya msingi ambayo yamekuja na kubadili kabisa mwelekeo wa elimu yetu;
- Kuifanya elimu isimamiwe na zaidi ya wizara mbili kwangu mimi kama mwalimu hili ni tatizo la msingi limetuletea matatizo zadi kuliko ufumbuzi wa yale yaliyokuwapo
- Sisi walimu tunadharauliwa sana na serikali hii na wakati huohuo tunabebeshwa lawama zote kila kunapotokea kufanya vibaya kwa wanafunzi tunaofundisha,mfano ni mtihani wa kdt cha 4 mwaka 2012 sehemu kubwa ya lawama zilitupwa kwetu kwa sbabu ndiyo sehemu ya wanasiasa kuficha udhaifu wao. Hili sisi walimu kudharauliwa limeshusha sana morali ya kazi ya walimu. Mfano ni walimu kuendelea kudai madeni yao miaka na miaka,madeni yasiyoisha ya malimbikizo ya mishahara,likizo,uhamisho nk. Na hakika mimi nilishashindwa kuelewa ni mfumo wa namna gani unaotumika kuendesha mambo ktk serikali hii. Mfano hai kabisa ni mimi mwenyewe nadai malimbikizo ya mshahara wangu ya tangu mwaka 2008. Nimeandika barua na barua, nilishafika mpaka wizara ya elimu lakini wapi bwana, nilishakata tamaa na nimeamua labda mpaka watakapokuja jisikia watanilipa. Huyu ni mimi, sasa jiulize ni walimu wangapi wako ktk hali hii? Watakuwa na moyo wa kufanya kazi? Halafu,nikuchekeshe kitu? Siku hizi hata ukiandika barua ya jambo lolote iwe unadai au kuomba kitu chochote ni nadra sana kujibiwa!!.....Ukitaka majibu basi wewe mwenyewe ufuatilie kwenye hizo ofisi na utapambana na urasimu balaa wenye kila harufu ya rushwa!
Kwa hiyo ndugu hawa ndo sisi walimu!
BEDO NYALUTOGO na
Kitaturu
1---Ni vizuri tukajadili mambo kwa hoja ambazo zinaweza kuijenga nchi yetu,ndio maana inabidi tuelimishane kidogo matatizo yetu makubwa yaliyosababisha mpaka tukafikia hapa, haya maneno ya
Ponera na Dada
FaizaFoxy hayajengi zaidi ya kubomoa,hakuna mtanzania hasa hasa huku bara ambae hana ndugu mkristo au muislamu,sasa kama tunaacha kujadili mambo muhimu humu na kuanza kuhubiri udini hautufikishi popote kila mtu afikirie tatizo la elimu kwa jicho la tatu,tuchunge sana midomo yetu na tuache ubinafsi,tuweke misingi ya upendo ili watoto wetu wakute kuna kitu tulifanya sisi kama wazazi wao.
2---Tuyajadili matatizo yetu kwa njia ambayo inatoa majibu ya matatizo yetu,sio kulalamika,tuwaeleze wanaotuongoza wapi wamekosea bila kuoneana haya,na wanaokosea wawajibike,mimi sikatai mama Ndalichako kuondoka pale maana hawezi kukaa pale maisha,kama urais unabadilishwa kwanini Ukatibu Mtendaji usibadilishwe?lakini hatupaswi kuweka viongozi wetu kwa misingi ya UDINI,hili ni kosa na kila mtanzania alikemee kwa nguvu zote,tuweke watu ambao wataweza kusimamia taratibu zilizowekwa,siasa ziondoke kwenye mambo nyeti hasa elimu,haiingii akilini mwanafunzi ameanza darasa la kwanza mpaka la saba hajui kusoma na kuandika halafu tunacheka,mwanafunzi anaanza kidato cha kwanza mpaka cha nne hajui kuandika halafu tunacheka,kibaya zaidi tunataka aongezewe daraja ili aende kidato cha nne au chuo cha ufundi,atatusaidia vipi mwanafunzi huyu?
3---Tuwaambie hawa viongozi wetu kwamba turudishe zile kali mbiu za zamani za PANDA MTI KATA MTI,na miti tunyoikata tutengeneze madawati ya watoto wetu,sio kusafirsha magogo ulaya na china,tuwaambie na tukatae haya wanayoyafanya,nchi inakuwa jangwa,mvua hazinyeshi,miti inakatwa kila siku,watoto wetu hawana madawati hivi hamuoni kuwa haya ni matatizo ya msingi ya kuwaambia hawa watawala wetu?
4---Walimu wetu hawana maisha mazuri,mazingira ya ufundishaji mabovu,hawana nyumba za kuishi,wao wameuzia nyumba zoote za serikali nchi nzima,wanakaa maeneo mazuri na watoto wao,wanakula vizuri na watoto wao wanasoma shule za bei mbaya,sisi tumekaa kimya tu,na inawezekana wanaua elimu yetu na ya watoto wetu maskini ili wawe wajinga wa kufikiri ili waendelee kutawala,kwa elimu hii ya shule za kata,interview ya kiingereza,kujuana kama kawaida,ushindani wa ajira unaanzia kwenye matokeo ya kidato cha nne mpaka chuo kikuuu,unafikiri mtoto wangu anaesoma shule ya kata atapata kazi
BOT au TRA?,ataisia kufanya kazi kwenye makaampuni ya ulinzi basi.
5---Wana JF tuwe na hoja na tuache udini,nchi hii ni yetu sote.