Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Bunda hakuna Uchaguzi Kata 6 hadi sasa. Kata ya mihingo vijiji 4. Kata ya Salama vijiji 3 Kata ya Kabasa vijiji 2 Kata ya Mcharo Vijiji 4 Kata ya kuzugu Vijiji 3 Kata Sazira Vijiji 3. Kata ya Nyamuswa Vijiji 2.

Nimefika Ofisi ya Mkurugenzi imefungwa. Watendaji wote Wako Ofisi ya DC wanapiga story. Wako pamoja Na viongozi wa CCM wa Wilaya.
 
Hapa wilayani mwanga kata ya lang'ata (dimbwi) kimeshanuka tayari kata nzima inanuka baruti ! Maccm yameshikiwa chin mapma asubuh yanataka kuvuruga uchaguzi!yamethibitiwa na vijana
 
Kata ya Mtindiro wilaya ya Muheza masanduku ya kura na karatasi za kura mpaka sasa havijafika vituoni.

Ndugu zetu himizeni watu wasiondoke hii siku watu waitoe sadaka mpaka ifike saa10 vinginevyo mkiondoa tu miguu mmeliwa,wataleta vifaa hata kwa saa1 kura zitapigwa na matokeo yatatangazwa mmeshindwa ..komaeni hapo hapo nunueni viazi,mihogo,na kila kinachowezekana kuleni pamoja kama wajeshi walioko vitani,hii ni vita wakuu hakuna kulala mpaka kieleweke
 
Same mjini mitaa mingi hakuna uchaguzi, hii ni baada ya wagombea wa Chadema kuenguliwa kihuni na mawakala wa shetani ccm
 
Hawa jamaa mpaka warudishe pesa zetu za ESCROW at least upepo utatulia la si hivyo kihama chao kimewadia.....
 
Hapa ni Mkuzo Songea.

Uamuzi wa sasa ni kuingia wanne kupiga kura. Atayebainika kurudia atabakizwa ndani au wapiga kura wataamua nini atendewe.

Nahofia hili la pili.
 

Attachments

  • 1418550764756.jpg
    1418550764756.jpg
    112 KB · Views: 340
Jamani magamba wameharisha uchaguzi manispaa ya ilala mpaka wiki ijayo badakuona hali mbaya
 
Inakuwaje wilaya nzima ya Kilindi CCM ipite bila kupingwa???
Hili lazima lihojiwe na kama kuna taratibu zilikiukwa basi ni lazima tuchukue sheria mikononi kuwateketeza wote waliohujumu!!!
 
Tayari jamani nimeshaweka alama ya vema kwa Chadema..

Kuna mamluki wa CCM waliletwa hapa kituoni
lakini nimefurahi sana.
mkuu wa uchaguzi hapa amewatema..
Makada wachache wa CCM kitongoji hiki wanahaha sana.

People's powerrrrrrrr

Mkuu,endeleeni Kukomaa Kwani Hayo Maccm yanaweza rudi na kupiga kura isivyo halali
 
Inakuwaje wilaya nzima ya Kilindi CCM ipite bila kupingwa???
Hili lazima lihojiwe na kama kuna taratibu zilikiukwa basi ni lazima tuchukue sheria mikononi kuwateketeza wote waliohujumu!!!
ule uhuni wa kuweka pingamizi ulifanikiwa 100%
 
Na wataendelea kujiliza kutafuta huruma ila kichapo kiko palepale!

Endeleeni kufarijiana kana kwamba chaguzi zote mtatumia kete na hujuma hizi za kuengua wagombea mlizotumia! Wananchi tuna hasira na nyie na uchaguzi mkuu mtatukoma wezi nyie
 
Mkuranga hapa mpaka sasa hivi saa 7 mchana zoezi la upigaji kura halijaanza.Vifaa vimeletwa saa 6:54 mchana.

Nahisi hizi ni mbinu chafu tu.Kwa nini vifaa vichelewe wakati uchaguzi umeandaliwa kwa muda mrefu tu?
 
Hadi sasa naandika uzi huu vijiji vya salama kati,salama A,na kurusanga wananchi hajaanza kupiga KURA.
Tatizo ni kucheleweshwa kwa masanduku ya kupigia kura.
Ziko taarifa CCM wanafanya hujuma kuvuruga uchaguzi kwa maslahi yao binafsi kwani ushahidi wa mazingira unaonesha UKAWA wanaongoza KURA za MAONI kama ilivyo kwenye kata za MSOMA MJINI NA SERENGETI.
Nawaomba wananchi,serikali,tume ya uchaguzi pamoja na wadau wote wa amani na maendeleo ya taifa letu kupigia kelele na kukomesha hujuma zozote dhidi ya haki mahali popote kunakofanyika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Aidha kwa umhimu mkubwa niwasihi wananchi wa kata ya salama kuwa wavumilivu ili kuepusha machafuko kwani mpaka sasa kuna kila dalili za ukosefu wa utulivu wa kisiasa.
 
Watu watatu wa CCM; Mgombea wa Uenyekiti wa Mtaa Kinondoni Mjini na mawakala wawili wamekamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay baada ya kuvunja masanduku ya kura na kuingiza watu kituoni kwa nguvu wengine wakiwa na mapanga, baada ya kuanza kuona upepo unawaendea vibaya. Polisi wa FFU walio full geared wamefika kituoni hapo na kuondoka na watu hao.
 
Back
Top Bottom