Hadi sasa naandika uzi huu vijiji vya salama kati,salama A,na kurusanga wananchi hajaanza kupiga KURA.
Tatizo ni kucheleweshwa kwa masanduku ya kupigia kura.
Ziko taarifa CCM wanafanya hujuma kuvuruga uchaguzi kwa maslahi yao binafsi kwani ushahidi wa mazingira unaonesha UKAWA wanaongoza KURA za MAONI kama ilivyo kwenye kata za MSOMA MJINI NA SERENGETI.
Nawaomba wananchi,serikali,tume ya uchaguzi pamoja na wadau wote wa amani na maendeleo ya taifa letu kupigia kelele na kukomesha hujuma zozote dhidi ya haki mahali popote kunakofanyika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Aidha kwa umhimu mkubwa niwasihi wananchi wa kata ya salama kuwa wavumilivu ili kuepusha machafuko kwani mpaka sasa kuna kila dalili za ukosefu wa utulivu wa kisiasa.