Nipo hapa Mbeya, kada wa chama tawala. Hata hivyo pita pita ya ngu mitaani hadi kule Rungwe nimejionea mwenyewe hali ilivyo tete kwa CCM.
Ni kama CHADEMA wao wamejitayarisha vizuri, na wapo kila mahala. Huu si oungo ,maana wameteka vijana wengi na bendera hasa Ile pana ziko kila mahala.
Jana niliona magari kadhaa ya matangazo na uhamasishaji ya CHADEMA, lakini sikubahatika kuona hata moja la CCM.
Nimefika Kiwira ndo balaa! Mchana vijana walifunga barabara kwa mdundiko uliokuwa ukiongozwa na gari ya matangazo ya CDM!
CCM najionea huruma lakini tusubiri tu.