Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Huku kwetu kiburugwa mitaa 5 cuf 4 ccm 1..mgombea mmoja wa kiburugwa no 3 alihaidi akishindwa atatoa 0713 vijana wamemfuata kakimbilia polisi
.
 
Mimi ushauri wangu kwa watz ni,sio CCM au CDM inaweza kuleta maendeleo. Maendeleo yanaletwa na sisi wenywe kuweka maslahi ya nchi kwanza.
Kwa sasa inabidi tuitoe CCM kwa hali na mali. Hata ikibidi kuichagua CDM na sio kwamba hawa manyan'gau CDM ni bora sana.
Ila tutakuwa kwenye nafasi ya kuunda mfumo mpya,katba mpya ambayo itakayolinda nchi.

Mwenyezi Mungu ibariki Tanzania!
 
Katika uchaguzi wa serikali za Mitaa unaofanyika leo Jumapili, tarehe 14/12/2014 kuna dosari/mapungufu mengi yaliyojitokeza katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo. Dosari hizi ni za makusudi kabisa.

Mpaka sasa dosari zimeonekana katika maeneo yafuatayo;


Na. KATA Mtaa Mapungufu/Dosari
1 KIBAMBA Kiluvya · Hakuna wino
Gogoni · Hakuna wino
Kibamba · Hakuna Wino
2 KWEMBE Mji Mpya · Hakuna Wino
Kwembe · Hakuna Wino
3 MBEZI Msumi · Vifaa vya uchaguzi vilichelewa mpaka saa 4:30 asubuhi · Mpigakura amekamatwa na karatasi ya kupigia kura akielekea kituoni kupiga kura
Mshikamano · Vifaa vya uchaguzi vilichelewa mpaka saa 3:30 asubuhi
Luis · Hakuna wino · Hiace ya mjumbe wa CCM inawabeba wapiga kura. Hiace hii inaendeshwa na dereva anayeitwa Salum ambaye ni kada wa CCM.
4 GOBA Kunguru · Wajumbe wa CHADEMA waliwekewa nembo ya CCM · Wajumbe wa CHADEMA-Viti maalum waliwekewa nembo ya CUF · Karatasi za kupigia kura zilichapwa upya na zoezi la uchaguzi lilianza saa 6:00 mchana
Goba · Mwenyekiti wa UKAWA kupitia CUF, jina lake lilikosewa, wakaamua kuandika kwa mkono na zoezi la uchaguzi likaendelea.
5 SARANGA Ukombozi · Uchaguzi ulianza saa 3:30 asubuhi badala ya saa 2:00 asubuhi kama ilivyopangwa kwa sababu CCM walifanya vurugu walikuwa wanamzuia mgombea wa CUF asipige kura.
Matangini · Hakuna wino · Uchaguzi ulianza saa 3 asubuhi · Kura zinapigwa katika ofisi ya MEO ambayo ni ndogo sana ulinganisha na wapiga kura 3169. · MEO alikataa kufanya uchaguzi katika majengo ya Shule ya Msingi ya Matangini ambayo yana nafasi ya kutosha. · Wapiga kura wanapata tabu kuhakiki majina yao katika mbao za matangazo kwa sababu eneo ni finyu
6 KIMARA Kimara-Baruti · MEO amewaambia wapigakura wamchague mjumbe mmoja tu badala ya watatu · Wino ulifika saa 5 asubuhi
Golani · Majina ya wapigakura yaliopo ukutani yamepauka kwa hiyo wapigakura wanashindwa kuhakiki majina yao
Mavurunza · Hapakuwa na wino mwanzoni, baadae na Mgombea wa CHADEMA aliamua kununua wino mwenyewe. · Askari/Polisi walikuwa wanawapigia kura wapigakura katika Kituo cha Millenium baada ya kushutukiwa na Mgombea wa CHADEMA waliamua kumkimbiza ili wamkamate kwa kisingizio kwamba anafanya vurugu katika kituo cha kupigia kura.
7 UBUNGO NHC · Kulikuwa na vurugu asubuhi wakati mamluki alipokamatwa.
Chuo Kikuu · Mpigakura aliyejiandikisha katika vituo viwili tofauti alikamatwa · Kulikuwa na mtu anayegawa fedha ala baadae alitokomea kusikojulikana
Kisiwani · Mpigakura alikuta jina lake limeshapigiwa kura na mtu mwingine.
Kibo · Hakuna wino
8 MAKUBURI Mwongozo · Jina la mgombea Uenyekiti wa CHADEMA limekosewa · Kuna mazingira ya vurugu
Makuburi-Kibangu · CCM walifanya vurugu asbuhi
9 MSIGANI Kwa Yusufu · Kuna kundi la CCM limeandaliwa kuharibu uchaguzi · Hakuna wino
10 MABIBO Mabibo · Uchaguzi umeahirishwa kwa sababu karatasi za kupigia kura ziliandikwa mtaa wa Kanuni badala ya Mabibo
11 MAKURUMLA Kilimahewa · CCM wamefanya vurugu na kumpiga mgombea wa CUF
12 SINZA A,B,C na D · Wino uliletwa saa 6 mchana

Kwenye namba 11 yaani MAKURUMLA-KILIMAHEWA
Taarifa zilizotolewa si sahihi
Mgombea wa CUF ndiye aliyefanya fujo kwenye eneo la kura, alimpiga mgombea wa CCM bwana TOWATOWA kupiga mateke vifaa vya uchaguzi, haikuishia hapo wakati kijana MASHAKA anaamulia mtafaruku huo naye alipigwa na UBAO/GONGO. Kijana mwingine HAMZA MCHUCHULI akaenda kumuamulia MASHAKA asipigwe zaidi naye akapigwa na kusukumwa na kupata jeraha la kukatwa na bati mkononi,
Fujo zote hizo amezifanya akiwa na kundi la vijana kutoka MBEZI (anakoishi, huku kwetu alishahama na si mkazi wa huku)
Ndipo tafrani ya nguo kuchanika ilipotokea na kupelekea mgombea huyo wa CUF kupata majeraha kadhaa
 
Ukiondoa ile neno hijabu itakuwa vema. .......Tatizo una macho lakini hutaki kuona na siwezi kukulazimisha na mbaya zaidi unayemdhania wewe kuwa ndo nafuu kwa bahati mbaya ndo hatari so better zimwi tulijualo
haujaenda shule jibu kwa fact kama nilizokupa hapo juu...
 
daaah ccm mnalo mwaka huu manaa hapaa ruaha vitongoji 22 hawajapata hataa kimoja
 
DSC071292.jpg
DSC071272.jpg
 
Dar Ngome ya CCM imedhihirishwa wazi
ccm mitaa 359
cuf mitaa 44
chadema mitaa 72 :smow:
 
Back
Top Bottom