Yaliyojiri katika Mkutano wa CHADEMA - Iringa

Yaliyojiri katika Mkutano wa CHADEMA - Iringa

Leo tuna muda wa kufuatilia mkutano wa chadema kwa sababu hakuna mktano wa CCM Morogoro...

morogoro tukio kubwa lililokuepo ni tamasha la diamond, na watu walijadili kweli bixa yakealiyiwaonyesha watoto
 
Hakuna cha viti walsa nn,ni kusimama.Morogoro walijaza viti ionekane watu nmiwengi pamoja na wasnii wote.Mwakja huu magamba mtatema nyongo.
 
Kama kawaida,na ndipo utaipenda CHADEMA,Twanga kote kote,ukizingua bungeni kwa kivuli cha KANUNI wanachanwa kwa waajiri wao (wapiga kura).
Na siku tano zikiisha kama kawaida,ni kukinukisha tuu Mjengoni,mpaka na kuko mabomu ya machozi na vitu vyenye ncha kali Vihusike.
 
Lakini huyu Serukamba kwa nini hawaomba msamaha watanzania. uelewa wake unakomea wapi? nahofu kwamba yeye haelewi kama lilikuwa tusi eti.
t
ulimaanisha nini naona jazba ilikuongoza tuambie tufaidi na sie
 
Wakuu.

Mtakumbuka kuwa leo wabunge wa Chadema walio fukuzwa kiuonevu bungeni wanafanya mkutano jimbo la Iringa mjini ili kushtaki kwa umma uonevu walio fanyiwa.

Hapa ni yanayojiri mkutanoni.

• Diwani wa Iringa mjini, Nyalusi, wananchi wa Iringa wana imani na viongozi wa CHADEMA, kuliko walioko madarakani. Kapanda Sugu

• Sugu: Tutaendelea kukomaa. Kiti kinamfukuza Lissu kwa kufanya kazi yake, wakati Serukamba mbunge wa FT, akiachwa! Tusi kubwa, hakuna mbunge katika jumuiya ya madola amewahi kutukana tusi baya kama hilo, limevunja rekodi Jumuiya ya Madola

• Sugu: Kauli ya WASSIRA, Kibanda ni nani? Ubinadamu na utu kwao ni cheo!

• Kiwia: Matusi kwa Wtz ni kufanywa maskini katika nchi tajiri, akina mama kwenda na nyembe na kila k2 kujifungua, kuzungumzia madawati miaka 50 ya uhuru wakati Kenya wanazungumzia kompyuta kwa kila mtoto.

• Kiwia: Ukiona mahali kuna amani ya kweli inayotokana na haki pamoja na demokrasia, ujue kuna watu wachache wamejitoa, ikibidi kwa jasho na tone la damu! Bunge sasa limegeuzwa kuwa rubber stamp ya masuala ya CCM!

• Mnyika anasema fedha za DECI zirudishwe. Wabunge wanazuiwa kujadili suala la Deci eti liko mahakamani, mbona Magufuli aliamua kuongelea suala la samaki wake kwani aliwagawa hao samaki wakati kesi ikiendelea.

• Mnyika anatuma salamu kwa Kamhanda kuwa alisababisha mauaji ya Mwangosi. Anasema kitendo hiki hakivumiliki na hawataliacha suala hili bila hatua kuchukuliwa

• Wenje anazungumzia suala la watoto kukaa chini kwa kukosa madawati wakati mbao zinasafirishwa kwenda nje kila siku kwa dili za wakubwa.

• Wenje anasema Maige aliwajibishwa kwa upotevu wa twiga wawili iweje kwa kawambwa ishindikane?

• Suala la mfumuko wa bei na kodi zisizo za lazima. Wenje "Kama akina Lusinde ndio washauri wa serikali hasa kupandisha thamani ya pesa zetu eti kwa kuondoa picha ya nyoka na kuweka ya Nyerere na Karume basi tumeruhusu akili ndogo kutawala akili kubwa".

• Dr Slaa Anasema wabunge wake hawatatafuna maneno inapofika suala kuiwajibisha na kuiagiza serikali kwa ajili ya maslahi ya Watanzania.

• Anasema Serikalii hii ni IMPOTENT kuanzia yule wa juu hadi walioko chini.

• Ameagiza; wabunge wa CHADEMA wakaze mwendo kuwa more focused na wakali zaidi kuliko sasa, kama kiti kinaendelea na tabia ya kuminya haki.

• Ameagiza kuanzia sasa hotuba zote za Kambi ya Upinzani Bungeni zitolewe nakala na kugawiwa hadi ngazi ya kata ya chama, kupeleka taarifa na maarifa kwa wananchi, Watanzania kila mahali nchi nzima.

• Mkutano umekwisha kwa amani, wananchi wanaandamaa kwa amani wakilisukuma gari la Dr Slaa na kuimba "Raisi, raisi, raisi, ....




====== Picha =======
attachment.php


attachment.php
you are so handsome like your ........
 
Lukosi/Chilisosi upo? Tunasuburi hiyo june kama ulivyoahidi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Wakuu.

Mtakumbuka kuwa leo wabunge wa Chadema walio fukuzwa kiuonevu bungeni wanafanya mkutano jimbo la Iringa mjini ili kushtaki kwa umma uonevu walio fanyiwa.

Hapa ni yanayojiri mkutanoni.

• Diwani wa Iringa mjini, Nyalusi, wananchi wa Iringa wana imani na viongozi wa CHADEMA, kuliko walioko madarakani. Kapanda Sugu

• Sugu: Tutaendelea kukomaa. Kiti kinamfukuza Lissu kwa kufanya kazi yake, wakati Serukamba mbunge wa FT, akiachwa! Tusi kubwa, hakuna mbunge katika jumuiya ya madola amewahi kutukana tusi baya kama hilo, limevunja rekodi Jumuiya ya Madola

• Sugu: Kauli ya WASSIRA, Kibanda ni nani? Ubinadamu na utu kwao ni cheo!

• Kiwia: Matusi kwa Wtz ni kufanywa maskini katika nchi tajiri, akina mama kwenda na nyembe na kila k2 kujifungua, kuzungumzia madawati miaka 50 ya uhuru wakati Kenya wanazungumzia kompyuta kwa kila mtoto.

• Kiwia: Ukiona mahali kuna amani ya kweli inayotokana na haki pamoja na demokrasia, ujue kuna watu wachache wamejitoa, ikibidi kwa jasho na tone la damu! Bunge sasa limegeuzwa kuwa rubber stamp ya masuala ya CCM!

• Mnyika anasema fedha za DECI zirudishwe. Wabunge wanazuiwa kujadili suala la Deci eti liko mahakamani, mbona Magufuli aliamua kuongelea suala la samaki wake kwani aliwagawa hao samaki wakati kesi ikiendelea.

• Mnyika anatuma salamu kwa Kamhanda kuwa alisababisha mauaji ya Mwangosi. Anasema kitendo hiki hakivumiliki na hawataliacha suala hili bila hatua kuchukuliwa

• Wenje anazungumzia suala la watoto kukaa chini kwa kukosa madawati wakati mbao zinasafirishwa kwenda nje kila siku kwa dili za wakubwa.

• Wenje anasema Maige aliwajibishwa kwa upotevu wa twiga wawili iweje kwa kawambwa ishindikane?

• Suala la mfumuko wa bei na kodi zisizo za lazima. Wenje "Kama akina Lusinde ndio washauri wa serikali hasa kupandisha thamani ya pesa zetu eti kwa kuondoa picha ya nyoka na kuweka ya Nyerere na Karume basi tumeruhusu akili ndogo kutawala akili kubwa".

• Dr Slaa Anasema wabunge wake hawatatafuna maneno inapofika suala kuiwajibisha na kuiagiza serikali kwa ajili ya maslahi ya Watanzania.

• Anasema Serikalii hii ni IMPOTENT kuanzia yule wa juu hadi walioko chini.

• Ameagiza; wabunge wa CHADEMA wakaze mwendo kuwa more focused na wakali zaidi kuliko sasa, kama kiti kinaendelea na tabia ya kuminya haki.

• Ameagiza kuanzia sasa hotuba zote za Kambi ya Upinzani Bungeni zitolewe nakala na kugawiwa hadi ngazi ya kata ya chama, kupeleka taarifa na maarifa kwa wananchi, Watanzania kila mahali nchi nzima.

• Mkutano umekwisha kwa amani, wananchi wanaandamaa kwa amani wakilisukuma gari la Dr Slaa na kuimba "Raisi, raisi, raisi, ....




====== Picha =======
attachment.php


attachment.php


Kwa kasi kama hii kweli CCM wataiba kura tu kunako 2015.
 
Tunasubiri kontena la mitumba kutok UK mwezi June. Unadhani utatuamia malori mangapi na ubwabwa magunia mangapi na wanamuziki wangapi kuujaza huo uwanja? ili tuanze maandalizi mapema...
Mimi siendi kuchangisha watu hela,
Kama watu wanashida na unatakiwa uwasaidie usiende kuwaomba hela toa hela na kama ni mafuta na una uchungu na ukali wa maisha basi usitumie gari lenye engine kubwa kama la msigwa
 
Tukubaliane jamani, Chadema ni tishio kubwa kwa Chama Cha Mapinduzi na Serikali tawala, hilo halina ubishi.
Tunachotaka ni kupata Chama na Serikali makini itakayowatumikia vyema Watanzania wote.

Kwa vuguvugu hili la Chadema, CCM inatakiwa kuamka na kuwafanyia watanzania yale yaliyo ndani ya ilani ya chama na kukisafisha chama mara moja. Na ingekuwa hekima zaidi kwa CCM kusikiliza kero za watanzania na kuzitatua.

Jambo kubwa linalofurahisha ni kuona CCM imepata viongozi wa juu walio wazuri na werevu, wenye uwezo wa kujieleza na kujipambanua mbele ya watanzania.

Tatizo lililomo ndani ya CCM na ambalo linachangia sana kuchukiwa na watanzania ni Ufisadi, likitatuliwa hili na kuwaweka pembeni wale walio na tuhuma za ufisadi nina uhakika 1000000% CCM itatawala Tanzania mpaka siku ya mwisho wa dunia.
 
Hii ngoma Inatwanga kote kote.kuwa bungeni ni faida kutolewa bungeni ni shangwe chezea CDM ww magamba?
 
msigwa+pembe.jpg
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, Iringa. Picha na Said Ng'amilo

KWA UFUPI

"Napata uchungu ninavyoona Watanzania wakiishi maisha magumu kwa hiyo naandaa hoja binafsi ya kuwasilisha bungeni ili umma uelewe umuhimu wa suala hili," alisema Mnyika na kuongeza kwamba atagawa fomu hizo kila atakapohutubia mikutano ya hadhara.


uuzaji wa pembe za ndovu anajulikana, sasa inakuwaje Serikali inashindwa kumkamata?" alisema Msigwa na kuahidi kulipua mabomu zaidi atakaporudi bungeni kwa maelezo kuwa anao ushahidi wa suala hilo.


Huo ulikuwa mkutano wa mwendelezo wa wabunge wa Chadema waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kuwapasha wananchi sababu ya kuchukuliwa hatua hiyo.
Wabunge hao walisimamishwa na Naibu Spika, Job Ndugai kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuwazuia askari wa Bunge kumtoa nje ya ukumbi, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu. Wabunge waliosimamishwa pamoja na Lissu ni Godbless Lema (Arusha Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Joseph Mbilinyi ‘Sugu' (Mbeya Mjini), Ezekiah Wenje (Mwanza Mjini) na Msigwa.



Hata hivyo, Lema na Lissu hawakuwapo katika mkutano huo wa jana ambao pia ulihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.

Mnyika kutoa hoja binafsi
Katika mkutano huo, Mnyika aligawa fomu kwa wananchi kuomba aungwe mkono wakati atakapotoa hoja binafsi bungeni juu ya mfumuko wa bei na umaskini nchini.
Mbunge huyo alisema wananchi wanakabiliwa na maisha magumu kutokana na hali mbaya ya uchumi.


"Napata uchungu ninavyoona Watanzania wakiishi maisha magumu kwa hiyo naandaa hoja binafsi ya kuwasilisha bungeni ili umma uelewe umuhimu wa suala hili," alisema Mnyika na kuongeza kwamba atagawa fomu hizo kila atakapohutubia mikutano ya hadhara.

Dk Slaa na Usalama wa Taifa
Katika mkutano huo, Dk Slaa alidai kuwa maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa wamegawanyika kutokana na makundi ya wanaotaka kuwania Urais mwaka 2015 kupitia CCM.



Dk Slaa alisema mgawanyiko huo ndiyo chanzo cha siri nyingi za idara hiyo kuvuja.
Aliwatuhumu baadhi ya wanachama wa CCM akidai kuwa wamekuwa wakiwavuta baadhi ya maofisa katika idara yao ili kuwasaidia kwenye harakati zao.


Source: Mwananchi
 
Kweli pesa haidanganyi, Mh. Msigwa sura imetakata na amekuwa body builder.
 
Hiyo Nyomi kwa maa ya mwiso niliiona wenye mkutano wa Kufunga Kampeni kule Nairobi Kenya, ni balaa
 
Back
Top Bottom