Yaliyojiri katika Mkutano wa CHADEMA - Iringa

Yaliyojiri katika Mkutano wa CHADEMA - Iringa

• Kiwia: Ukiona mahali kuna amani ya kweli inayotokana na haki pamoja na demokrasia, ujue kuna watu wachache wamejitoa, ikibidi kwa jasho na tone la damu! Bunge sasa limegeuzwa kuwa rubber stamp ya masuala ya CCM!
mara mja yenyewe ndio ihii
 
Ni kinana huyo atueleze inakuaje meli yake ilikamatwa na mzigo,alafu asimjue mwenye mzigo?..ina maana yeye anamjua mbwa lakini hamjui mwenye mbwa?
 
Mimi leo usiku nimeota Adulrahamani Kinana ambaye ni katibu mkuu au mtendaji mkuu wa ccm anakwapua pembe za ndovu akitumia kampuni yake. Sasa sijui kama Msigwa naye alimaanisha Kinana au La. Ni ndoto tu lakini.

Aweda zipo ndoto za ukweli ila kuthibitisha cha ndotoni ndiyo kazi sasa
 
ndo siasa zinazotakiwa hatutaki matusi ila siasa safi zenye maneno ya kukomboa nchi na sio kutukanana.HII ndo maana mfalme suleman aliomba hekima. keep it up chadema .freedom is coming tomorrow
 
. So tumuache na Msigwa alipeleke bungeni pengine huko atajitokeza mwenye jeuri ya kujibu
Yaani Bungeni kumekuwa sehemu ya kuupeleka upuuzi kama huu wa Msigwa? Msiwe na akili mgando kuna mamlaka husika za kushughulikia mambo kama haya, Pale apeleke kero za wananchi wake(mifugo) na kuisimamia serikali katika mambo ya msingi.
Huyu Mchungaji nae kawa mtu wa mipasho kweli!
Kundi la Jahazi Modern Taarab limepungukiwa na waimbaji wake bahada ya wengi wao kupata maternity leave so namuomba mchungaji akashike nafasi ya Leyla Rashid kwa muda.......

 
CHADEMA wanakomboa siyo kusengenya kama ccm mungu yuko nao kila waendako na cc tunawasaidia katika njanja zingine. mungu uwabariki
 
Pori lililopo kati miinuko ya Monduli(kwa Sokoine) na Longido mpaka karibu na mlima OldonyoLengai limejaa wahamiaji haramu wa kisomali ambao hawabughudhiwi na mtu yeyote. Ukiongea na wenyeji wa maeneo hayo(Wamasai) juu ya uwepo wa wasomali hao na wanafanya nini, wanakujibu kwa masikitiko kuwa shughuli yao kubwa ni uwindaji haramu wa tembo. Askari wa wanyama pori wa maeneo hayo wanajua lakini wamenyamazishwa na maafisa usalama wa serikali.

Kwa maelezo ya wamasai hao, inavyoonekana hao wasomali wana kinga fulani kutoka kwa vigogo wa serikali na wanatumia silaha nzito sana kama SMG na hata milipuko kiasi kwamba hata wamasai wenyewe wanawaogopa. Mmasai mmoja akasisitiza kuwa ili umwamini anachosema, ukipita barabara ya kutoka Monduli kwenda Longido(ambayo ni ya vumbi kote) hutakaa ukutane na tembo ama faru njiani ila wanyama wengine wote utawaona katika makundi makubwa.

wamasai hao wanazidi kudadavua kuwa tembo wanaosalimika hukimbilia Ngorongoro Crater, au Serengeti ama upande wa Kenya ambako walau ulinzi wa wanyama ni mzuri zaidi.[

Nadhani hawa Wasomali ndio vibarua wa Kinana kwa maeneo ya kaskazini.
QUOTE=kim jong un;6204078]kinana huyo[/QUOTE]
 
Yah your very right.. ila zitakutakatisha vizuri zikiwa za halali... Vipi zile za ndovu kwa kigogo wa CCM je nazo zimemtakatisha au zimegongana na maradhi maana hatuoni mtakato wa mwili??
Kuna wakati Mao Tse Tung , wa China,aliwahi kisema " bombard the headquarters" , akimaanisha hata kwenye chama chake cha kikomunisti.wabadhirifu wapgwe vita.
Na mimi nasema kama ushahidi wa vipusa,, bombard Lumumba.
 
Kusema tu jamani mumesema sana lakini hakuna anayesikia. Tafuteni mbinu mbadala ya kuwaletea wananchi maendeleo sio kuendeleza siasa. Siasa zinatakiwa wakati wa kampeni, sasa nyie mnakalia siasa miaka yote mitano hayo maendeleo yatapatikana kweli? Ni wakati sasa wa kukaa na kutafakari malengo yenu, na kama hamna jiwekeeni malengo. Kuwa na malengo kutawasaidia kutokuendeleza mijadala bila kufuata utaratibu kama ilivyosasa. Mana kinachoendelea hivi sasa kwa vyama vyote vy siasa ni maneno na malumbano tu suala ambalo linadhihirisha kuwa vyama havina malengo zaidi ya kuzoa tu hoja kila inapojitokeza. Mijadala yote inayoendelea hivi sasa ikiwa ni ccm basi wataongelea chadema hadi mkutano uishe, wakija chadema nao watafanya hivyo hivyo hadi mkutano uishe. Hayo maendeleo mnayowadanganya wananchi yatapatikana lini?
msigwa+pembe.jpg
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, Iringa. Picha na Said Ng’amilo

KWA UFUPI

“Napata uchungu ninavyoona Watanzania wakiishi maisha magumu kwa hiyo naandaa hoja binafsi ya kuwasilisha bungeni ili umma uelewe umuhimu wa suala hili,” alisema Mnyika na kuongeza kwamba atagawa fomu hizo kila atakapohutubia mikutano ya hadhara.


uuzaji wa pembe za ndovu anajulikana, sasa inakuwaje Serikali inashindwa kumkamata?” alisema Msigwa na kuahidi kulipua mabomu zaidi atakaporudi bungeni kwa maelezo kuwa anao ushahidi wa suala hilo.


Huo ulikuwa mkutano wa mwendelezo wa wabunge wa Chadema waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kuwapasha wananchi sababu ya kuchukuliwa hatua hiyo.
Wabunge hao walisimamishwa na Naibu Spika, Job Ndugai kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuwazuia askari wa Bunge kumtoa nje ya ukumbi, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu. Wabunge waliosimamishwa pamoja na Lissu ni Godbless Lema (Arusha Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Mbeya Mjini), Ezekiah Wenje (Mwanza Mjini) na Msigwa.



Hata hivyo, Lema na Lissu hawakuwapo katika mkutano huo wa jana ambao pia ulihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.

Mnyika kutoa hoja binafsi
Katika mkutano huo, Mnyika aligawa fomu kwa wananchi kuomba aungwe mkono wakati atakapotoa hoja binafsi bungeni juu ya mfumuko wa bei na umaskini nchini.
Mbunge huyo alisema wananchi wanakabiliwa na maisha magumu kutokana na hali mbaya ya uchumi.


“Napata uchungu ninavyoona Watanzania wakiishi maisha magumu kwa hiyo naandaa hoja binafsi ya kuwasilisha bungeni ili umma uelewe umuhimu wa suala hili,” alisema Mnyika na kuongeza kwamba atagawa fomu hizo kila atakapohutubia mikutano ya hadhara.

Dk Slaa na Usalama wa Taifa
Katika mkutano huo, Dk Slaa alidai kuwa maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa wamegawanyika kutokana na makundi ya wanaotaka kuwania Urais mwaka 2015 kupitia CCM.



Dk Slaa alisema mgawanyiko huo ndiyo chanzo cha siri nyingi za idara hiyo kuvuja.
Aliwatuhumu baadhi ya wanachama wa CCM akidai kuwa wamekuwa wakiwavuta baadhi ya maofisa katika idara yao ili kuwasaidia kwenye harakati zao.


Source: Mwananchi
 
Sijui kama tembo walisalimika wakati Kinana alitumi treni kwenda Kigoma na kujifanya anafanyakazi za kichama kumbe alikuwa anaangalia ni mbuga gani zenye tembo wengi.

Kinana ni wakufunga Jela pamoja na Mafisadi wenzake hawa watu sio wakuwaachia kabisa Kinana, Kikwete, Mkapa na Mafisadi wenzao ni kutupa Jela wote na wafie huko
 
Kuna wakati Mao Tse Tung , wa China,aliwahi kisema " bombard the headquarters" , akimaanisha hata kwenye chama chake cha kikomunisti.wabadhirifu wapgwe vita.
Na mimi nasema kama ushahidi wa vipusa,, bombard Lumumba.

Vipi leo? hukulipwa posho wiki hii? mbona unawageuka viongozi wako tena
 
Mkuu nasikitika kukuarifu kuwa sijakuelewa, bombard Lumumba?? ni nani huyu, mi nilidhani ni Abdu

Mkuu maana yangu ni kwamba kama kuna mtu ambaye ana ushahidi wa hivyo vipusa vinavyo mhusisha kigogo wa CCM , viwekwe hadharani, ili watu wajiamulie ukweli ni upi.
Ubadhirifu na ujangili hata ukifanywa na nduguyo unakera na ni kosa.
Tatizo lililopo wengi wanalitumia hilo " tatizo la vipusa" kipropaganda na hakuna ushahidi wake.
 
Wakuu ile nyomi ya watu kwenye mkutano wa chadema iringa ni kufuru, hyo ni msg tosha kwa walanchi. Morogoro pamoja na kugata tshet, kusombwa na malori na bus za abood na uwepo wa Diamond na Chege ila mambo bado duh? Kwel kazi ipo.. Big up wanacdm. Ile nyomi mara ya mwsho nimelichek mazish ya the great kanumba pale leaders club.
 
hata uwe na kichaa ukiona hii picha utajua tu chadema imekubalika na pasipo kuwa na wizi wa kura 2015 ccm bye bye. kuna mtu amehoji chadema kuchangiwa pesa mikutanoni wakati kuna ruzuku lakini nia ya wananchi ni kuhakikisha chadema inaingia ikulu. Lakini pia mchango wa mkutanoni halazimishwi mtu ni wa hiari
 
Back
Top Bottom