Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,483
40,500
Kuna mzee mmoja nilikutana naye eneo moja la kazi miaka 12 iliyopita, na katika mazingira ya kazi tulikuwa tukiheshimiana sana, na tulikuwa tukiishi kama familia; leo tukale wapi au kunywa wapi, mara moja moja ilikuwa ni kitu cha kawaida.

Baada ya muda kupita aliamua kung’atuka na kwenda kujikita kwenye biashara zake katika mkoa mwingine.

Miezi miwili iliyopita, nilipata kasafari katika mkoa aliopo; nikaamua kumtafuta huyo mzee kwa njia ya simu, ili angalau niweze kuonana naye na tuweze kuzungumza mawili matatu; kama binadamu wanavyotakiwa kuishi.

Bahati nzuri, ilikuwa ni siku ya jumapili.

Mzee alifurahi sana, kupokea simu yangu na tukakumbushana mengi, na pia nikamwambia nipo hapa mkoani, naomba kama inawezekana angalau nije nikujulie hali.

Mzee akanijibu, samahani sana mambo yameingiliana, ndio najiandaa hapa kuelekea kwenye biashara yangu, kukagua mapato.

Alivyoniambia hivyo nikajiongeza na kumuambia, ‘’basi siku nyingine kama nafasi itapatikana, tutaonana tuombe uzima’’

Baada ya hapo nikasoma kitabu cha maandiko kama aya mbili hivi, ndipo nikahitimisha kwa kusema, maisha ya sasa hayahitaji kutembeleana kwa ajili ya kupiga stori; bali ni kutembeleana kwa malengo ya kwenda kupeana fursa za ‘win/win situation’

We una mtazamo gani?​
 
Sio watu hawataki mkuu.

Minaona kama maisha yamebadilika sana, pesa imekua mbele kwenye kila kitu.

Dunia imekua uwanja wa fujo na hata hata wazazi wamekua bize na kufanya kazi kuliko kufanya malezi.

Teknolojia nayo imerahisisha salam ambayo zamani tuliita ni nusu ya kuonana.
 
Inasikitisha sana, kwa mazingira hayo kitakachokuja kuwakutanisha ni misiba tu. Kama inawezekana, kuwa wa kwanza kuwatembelea ili kuonyesha njia.

Unawatembelea mda gani? Natika home saa 11 alfajiri, narudi saa 3 usiku, watoto na mke wamelala.

Weekend:
  • Gari service
  • Shopping.
  • Ibada.
  • Kukaa na watoto.
  • Kukaa uchi na shemeji yako...
Nitembelee ndugu saaa ngapi?
 
Hiyo ipo sana watu wanakukataa. Mwanangu nilimbeba maghetoni kwa muda life likasonga akaenda mji mwengine, wakati tukiwasiliana ananiambia ukija huku we nicheki tu mwanangu we damu yangu.

Mungu si Athumani nikatia timu ule mji kwa mishe zangu baada ya siku kadhaa pale one day nikamcheki tukaongea fresh tu. Ile kumjulisha tu nipo maeneo ya ule mji mwana akanikataa.
 
Kuna mzee mmoja nilikutana naye eneo moja la kazi miaka 12 iliyopita, na katika mazingira ya kazi tulikuwa tukiheshimiana sana, na tulikuwa tukiishi kama familia; leo tukale wapi au kunywa wapi, mara moja moja ilikuwa ni kitu cha kawaida...​
Naona alikuwa busy kweli. Next time moe.muda wa kutosha na uende wakati hana kazi.

Binafsi sijaona tatizo lolote hapo, hakuwa na nafasi hiyo siku.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom