Tommorow or today
Member
- Jan 4, 2024
- 46
- 130
Niite Mimi ndyo jina langu(sio jina langu halisi. Nimezaliwa Miaka 30 iliyopita Kanda ya ziwa.Nina elimu ngazi ya Shahada.
Nikiwa nina Miaka 10,siku moja jioni ghafla nikasikia kitu kinatembea machoni kama mtu aliyemwagiwa mchanga.Nikajua ni mchanga umeingia tu,Kumbe!Nikaanza kufikicha na kufikicha..nilinawa na maji pasi na mafanikio.Mchanga haukutoka!
Ikawa Kila nikienda shuleni mchanga unazunguka machoni,nikitoka ni mzma hovyo humalizia mchana na alasiri salama.Machweo itakapofika mchanga unazunguka machoni.Ilikuwa Ikifika saa moja nalala.Hali iliendelea Kwa muda Hadi ikaisha yenyewe.Macho yangu yakaanza kupoteza uwezo wa kuona kidogo kidogo.Tulipoenda hospitali ya mkoa ya .....Nilipimwa nikapewa miwani nikiwa darasa la nne.
Turudi nyuma, Kwa wazazi wangu tumezaliwa sita,Mimi ni mtoto wa pili kuzaliwa.Nilisifika Kwa tabia njema na maadili mtaani nilipoishi na akili za darasani Kwa kipindi hiko.
Hapo mtaani kwetu tupaite Kwembe kulikuwa na babu mmoja ambaye ni jirani yetu.Tumuite Mzee Musa.Mzee Musa na Sisi tulikuwa ni majirani .Hivyo Kila nitokapo shule lazima nipite kwenye uga wa nyumba yake ndyo nifike kwetu.Nipitapo huniita na kiniuliza nilochosoma shuleni.Na Mimi humwambia muda mwingine huomba nimpe madaftari yangu.Nami humpatia na huanza kunisifia mwandiko na Kila kitu!
Itaendelea...
Nikiwa nina Miaka 10,siku moja jioni ghafla nikasikia kitu kinatembea machoni kama mtu aliyemwagiwa mchanga.Nikajua ni mchanga umeingia tu,Kumbe!Nikaanza kufikicha na kufikicha..nilinawa na maji pasi na mafanikio.Mchanga haukutoka!
Ikawa Kila nikienda shuleni mchanga unazunguka machoni,nikitoka ni mzma hovyo humalizia mchana na alasiri salama.Machweo itakapofika mchanga unazunguka machoni.Ilikuwa Ikifika saa moja nalala.Hali iliendelea Kwa muda Hadi ikaisha yenyewe.Macho yangu yakaanza kupoteza uwezo wa kuona kidogo kidogo.Tulipoenda hospitali ya mkoa ya .....Nilipimwa nikapewa miwani nikiwa darasa la nne.
Turudi nyuma, Kwa wazazi wangu tumezaliwa sita,Mimi ni mtoto wa pili kuzaliwa.Nilisifika Kwa tabia njema na maadili mtaani nilipoishi na akili za darasani Kwa kipindi hiko.
Hapo mtaani kwetu tupaite Kwembe kulikuwa na babu mmoja ambaye ni jirani yetu.Tumuite Mzee Musa.Mzee Musa na Sisi tulikuwa ni majirani .Hivyo Kila nitokapo shule lazima nipite kwenye uga wa nyumba yake ndyo nifike kwetu.Nipitapo huniita na kiniuliza nilochosoma shuleni.Na Mimi humwambia muda mwingine huomba nimpe madaftari yangu.Nami humpatia na huanza kunisifia mwandiko na Kila kitu!
Itaendelea...