Nyie mitoto ya mwisho mnakera sana... mivivu hadi mnakera!
Miaka kadhaa iliyopita si nikaenda kuishi na uncle wangu... mtoto wa mwisho kwa bibi na babu yangu!! Basi yule jamaa akawa anataka hadi nguo nimfulie! Akaacha kunipatia nguo zake baada ya kugundua naziloweka tu naenda kuzianika... sipendi ujinga mimi!
Yote 9, kumi unaweza kukuta anapiga kelele kishenzi kukuita! "Chigee! Chigee... njoo mara moja!" Nakumbuka enzi hizo nishamaliza Six, kuamka mapema sio lazima! Utashangaa kelele zote hizo anataka umpe viatu vyake ambavyo vipo chini ya 10 toka alipo... yaani kwavile anakunywa chai, ndo basi tena anaona taabu kuinuka na kwahiyo anataka mtu amletee!
Hayo yakapita! Nikiwa nimeshaanza maisha yangu huku nikiwa nikiwa naenda home siku za weekend peke yake; nikawa naumwa na hivyo kulazimika ku-settle kwa muda pale kwa wazazi! Hapa napo, tuna mdogo wetu wa mwisho!
Hili nalo, likinywa chai kila kitu litaacha hapo hapo! Likija kwenye meza yangu iliyojaa makokoro kibao, basi kama ni sinia au kikombe, hesabu ataacha hapo hapo!! Hili hata kuzima taa haliwezi! Sioni anachokiweza zaidi ya kufua na kupiga pasi nguo zake mwenyewe! Ngoja liumwe sasa... hata kumeza dawa, halitaki!
Aisee, nyie watu mnaboa sana!!!