Wasi Wasi wa Udini

Status
Not open for further replies.
Ogah said:
Hi Ngabu's Style

Where is Biggy Njabu?

Hey Ogah, what's up bro?? I'm just chillin man.
Hahahahaa Biggy Njabu sio.......
Yupo tu. Najua ataibuka tu hapa muda si mrefu. Si unayajua machachari yake we mwenyewe.
 
Nyani Ngabu said:
Ogah said:
Hi Ngabu's Style

Where is Biggy Njabu?

Hey Ogah, what's up bro?? I'm just chillin man.
Hahahahaa Biggy Njabu sio.......
Yupo tu. Najua ataibuka tu hapa muda si mrefu. Si unayajua machachari yake we mwenyewe.

Nyani
Karibu mzee. This is my new Home. Mkandara ameondoka bila kuanga, atakuja tena hawezi kuishi bila kubishana.
 
sam said:
Nyani Ngabu said:
Ogah said:
Hi Ngabu's Style

Where is Biggy Njabu?

Hey Ogah, what's up bro?? I'm just chillin man.
Hahahahaa Biggy Njabu sio.......
Yupo tu. Najua ataibuka tu hapa muda si mrefu. Si unayajua machachari yake we mwenyewe.

Nyani
Karibu mzee. This is my new Home. Mkandara ameondoka bila kuanga, atakuja tena hawezi kuishi bila kubishana.

Hahahaa ebwana Sam inakuwaje babu?? Nakuona bwana ukiendeleza yale tuliyoyaacha bcstimes. Lakini uongo mbaya hapa bado kabisa hapajafikia kiwango cha bcstimes. Pole pole ndo mwendo lakini, tutafika tu.

Kweli aisee, naona bwana Mkandara katoka baruti bila hata taarifa.....Lol. Poa mzee baadae basi.
 
Mzee Es said:
Mzee Nyani,

Heshima juu mkuu, wapi Ngabu?

AAAAAAAAAAAHHHHHHHH Mheshimiwa Mzee Es, za kupotea kaka yangu? Ngabu yupo anga za Scandinavia akijivinjari na totoz za Kiswidish.........

Siku ya siku ikifika ataibuka tu hapa na kuuwasha moto kama kule bcstimes
 
Hili suala haliendi popote. Wale wanaounga mkono wana sababu kubwa mbili, kwanza, tutafaidika kiuchumi, pili nchi nyingine ambazo si za kiislamu ni wanachama (Uganda - 1974, Msumbiji - 1994, Ivory Coast-2001). Pia wale wanaunga mkono wanaelezea mbona Tanzania ina Ubalozi Vatican ambapo ni makao makuu ya Kanisa Katoliki?

Hata hivyo wale wanaopinga wanasema, OIC ni shirikisho la kidini ambalo malengo yake yanapingana na Katiba ya Tanzania na ile ya Zanzibar.
 
Tuangalie kwanza wenzetu Mozambique wamebenefit vipi kiuchumi baada ya kujiunga kwao OIC. Maana on our side its going to be a thorny issue maana wengi wameshaingiza dini katika siasa na hiyo inagawanya watu, na if it heads in the direction that people aren't looking at it in an economical sense, we will end up with issues.
 
hii hoja imekuja wakati muafaka kwa sababu juzi rais karume akiongea kwenye maadhimisho ya mwaka mmoja tangu aanze second term alichokoza hoja mbili

moja alisema kuwa zanzibar kujiunga na OIC kama sehemu ya muungano ni priority.
mbili alisema kuna wazee waliofurahishwa na uongozi wake wameenda kumuomba abadili katiba aendelee kutawala[yaleyale ya salmin] ila yeye anasema amewakatalia.

turudi kwenye OIC sioni faida ya maana ya kiuchumi waliyopata mosambique [ambao pia wamedandia commongwealthy] na uganda.hatukubali kuvunja katiba kwa ajili ya vimisaada mbuzi,afterall nchi yetu ni tajiri so hatuwezi kuuza uhuru wetu wa imani ,utajiri wetu ukisimamiwa vema hata hiyo world bank itatusikia tu,hata hivyo mashirika ambayo tu wanachama kwa sasa yanatosha na wala hayakwazi sehemu ya wananchi wetu.

kuhusu VATICAN ni nchi na ni mwanachama wa UN kama iran ,kenya,china ets n wanawakilishwa sehemu kubwa duniani kama nchi,chini ya papa ambaye ndio head of state ,so waislamu pia wakitaka wanaweza kuungana kidunia wakaamua nchi ya kiislamu ambayo wataamua kiongozi wake atambulike kama kiongozi wa waislamu duniani,kama nchi haiwezekani wachague kiongozi wa waislamu duniani ,apewe heshima,mbona waanglikana .budha,dalai lama,ismailia ets wana viongozi wao wanaotambulika kidunia ,,sasa kama wameshindwa kukubaliana whos in charge ,ndio vatican isiwepo

so hoja ya vatican ni hoja ya upofu,na kwa kifupi OIC sio muarubaini wa matatizo yetu sanasana tutalemaa kama watu wazima wenye mikono wanaouza uhuru wao kwa kujipanga mbele ya maduka ya watu wapewe pesa za bure kila ijumaa,wengine na nguvu zao ,sasa mnataka kutupanga mbele ya OIC Tungojee kutwa kugawiwa bure,tutaendelea kulemaa kwa uvivu,,,

tuchape kazi na kama kukopa tukope world bank na nchi rafiki na tulipe na riba ,,tatizo liko wapi kama kweli tunataka maendeleo,,mbona na mikopo mingine tumesamehewa baada ya kuonyesha juhudi kulipa,,inawezekana tufanye kazi!!!!!!!!!
 
Article II ya OIC inasema hivi:

Objectives and Principles:

A) Objectives:

The objectives of the Islamic Conference shall be

to promote Islamic solidarity among Member States;

to consolidate cooperation among Member States in the economic, social, cultural, scientific and other vital fields of activities, and to carry out consultations among Member States in international organizations;

to endeavor to eliminate racial segregation, discrimination and to eradicate colonialism in all its forms;

to take necessary measures to support international peace and security founded on justice;

to coordinate efforts for the safeguarding of the Holy Places and support of the struggle of the people of Palestine, to help them regain their rights and liberate their land;

to back the struggle of all Muslim people with a view to preserving their dignity, independence and national rights;

to create a suitable atmosphere for the promotion of cooperation and understanding among Member States and other countries.
 
Mzee Mwanakijiji,

Ndio maana sasa hivi JM yuko Mputo for the next two weeks, ikiwa ni pamoja na kui-study hiyo issue!, kwa makini kabla ya serikali kuamua!
 
Kutokana na jinsi udini ulivyo kuwa sensitized pale kwetu tangu Nyerere aondoke madarakani, nindhani kuwa kujuinga na OIC itakuwa ni chanzo cha kuvurugana.

Faida za kiuchumi kama zipo nadhani hazina uzito kulinganisha na utaifa; at least kwa maoni yangu. kwanza kabisa, hii ndoto ya kudhani kuwa maendeleo yetu ya kiuchumi yataletwa na watu wengine ni ugonjwa mkubwa sana unaotusumbua sisi watanzania. Kila mtu anadhani kuwa kuna baraka itadondoka kutoka kusikojulikana kama tu tutasidiwa na watu au kikundi fulani kutokla nje. Chanzo cha kuuza mashirika ya umma ilikuwa ni kutokana na imani hiyo hiyo kuwa tukiwapa watu wa nje kuendesha makampuni haya tutapata maendela ambayo hadi leo sijayaona. Nashangaa kuwa bado kuna viongozi ambao wanafikiria kuwa tutapata mendeleo fulani kwa kujiunga na OIC. Hii ni ndoto kweli kweli na vile vile ni uvivu mkubwa sana wa kimawazo ambao tunatakiwa tuachane nao


Kuwapo kwa ubalozi wa vatican siyo sawa na kujiunga na OIC, bali ni sawa na kuwepo kwa ubalozi wa nchi za kiislamu kama Saudi Arabia, Irani nk. Kwanza inajulikana kuwa Vatican ina mabalozi duniani kote kwa vile ni taifa linalojitegemea. Mabalozi wa vatican wapo pia katika nchi za kiislamu na kuna nchi za kiisalamu zaina mabalozi wao Vatican. Kwa hiyo watu wasiamue tu kuwa tuingine OIC kwa vile kuna balozi wa vatican Tanzania. Tanzania siyo mwanachamana wa muuongano wowote unaopromote udini. Kikatiba swala la dini limeachwa kwa kila raia kujiamulia mwenyewe bila kushinikizwa na serikali na hilo ni jambo zuri kabisa kwetu kitaifa.
 
Swala hili pia limewekwa kule maoni.org na huu ndio mtazamo wangu kama nilivyojibu hukooo!

Ili tuweze kulizungumzia swala hili kwa haki inabidi kwanza tuufahamu MUUNGANO wenyewe.
Zanzibar is a distinct society na tulipoungana - sisi BARA tulikubali kutokuwa na serikali yetu. Haya ni matakwa yetu sio yao Wazanzibar na kikubwa zaidi ni kuwa Muungano wetu unakubali na kusherekea culture za hawa jamaa - Their cultural value includes obedience to the teachings of the Islamic faith...
Ikiwa tunawakubali kwa hayo waliyokuja nayo ktk muungano na kisha tumeweza kuwafanya wakazikubali hata dini nyingine kuingia kwao nje ya matakwa yao. Inakuwaje leo tuwazuie wao ku-communicate na kile wanachoamini wao kama ni moja ya tamadani yao kwa sababu tu sisi hatuamini urafiki huo!.. IOC hawajiungi na muungano wetu isipokuwa ni mpango wa kibiashara na ustawi wa jamii kwa Wazanzibar, sisi bara hatuna haja kabisa ya kuwepo ktk culture hiyo ya UPATU... huo ni mchezo wa wanawake waache wa practice kile kinachowapendeza.

Ukioa mke muislaam sidhani kama ni vizuri kumzuia kwenda msikitini ama kujiunga na waislaam wengine, kwa sababu ndoa hii imeungwa kwa makubaliano kuwa kila mmoja atabaki na dini yake... hata kama wewe yaani mume hupendi kwenda kanisani ama huchagui marafiki bado haipotoshi maana kuwa wewe ni mkristu!.. Vilevile mfano huu unakuja kwa Muislaam aliyeoa mwanamke wa kikristu kwa makubaliano kuwa dini isiwe issue ndani ya nyumba...Makubaliano haya hayamzuii mtu kupractise dini yake wala kujiunga na makanisa ama misikiti kwani hapa kuna watu wawili waliofunga ndoa (two states joined).
Kisha kuwepo kwao IOC ni advantage kwetu kwani mke huyu anatuletea rafiki yake mwenye nazo...bora kuliko urafiki na maskini wenye uchu kama South Africa -SADC, Kenya na Uganda (EAC).
What if Zanzibar hawataki jumuiya hizi, je Tanzania nzima tutajitoa?

Nadhani sisi bara tungeyajua haya toka mwanzo kabla kufunga ndoa, tukamchagua mke mkristu mwenzetu ama yule asiyekuwa na dini. Muungano ni kasheshe nchi zote duniani zinaelewa tatizo lake na ndio maana sii rahisi kukuta ndoa zikidumu.
Tukifuata katiba tu hutaweza kuona ukweli kwani katiba yetu sasa hivi ni Perspective over Reality!.. ni katiba hiyohiyo inatuambia kuwa Tanzania ni nchi ya KIJAMAA na KUJITEGEMEA. Well, sifahamu kama hili lina ukweli!
Ni katiba hiyohiyo Inayotufunga tuheshimu haki za binadamu hali leo hii tunafungamana na kuzitetea nchi zinazo kiuka haki za binadamu.
Ukweli yote haya yanatupeleka pabaya zaidi ya Zanzibar kujiunga na IOC. Wakijiunga na hiyo IOC, itaathiri nini Bara hali wao ni 99% waislaam...ikiwa IOC haitakuwa na kitengo bara.
Hata hivyo, binafsi ni bora kuwa na chombo kinachojulikana na serikali na kina ofisi yake Zanzibar kuliko ku-deal na watu ambao wanafanya mambo kichinichini.. Uhusiano kati ya Zanzibar na nchi za Kiislaam ni mkubwa sana toka miaka hiyo kabla ya uhuru na bado inazidi kukua kila kukicha. Uhusiano huu ni sawa kabisa na mke anayetembea nje ya ndoa.
Kuna mawili hapa - Tumpe talaka na ndoa ife, laa sivyo tumeumia sisi na tukubali kuwa Zanzibar ni nchi sio mkoa (mtoto).
Pia tukumbuke kuwa sheria inasema kutembea nje ya ndoa sii crime!..na haina ubaya zaidi kwani Zanzibar ni lesbian tu, leteni mke mwingine kimada huyu IOC ndani, hakika Bara itawashughulikia wote!
 
Mkandara,
Kama ni Zanzibar peke yao sioni tatizo. Tatizo linakuja pale inapodhihirika kuwa Zanzibar si sovereign state tena. Could they join as observers or as what. That is my question. Lakini wasituburuze sisi bara katika hilo. Otherwise nakubaliana na kauli ya Kichuguu.
 
suala la OIC limerudi tena?
kama mtakumbuka suala hili la OIC ndio lilimuondoa malecela kwenye uwaziri mkuu,
unajua Muungano wa tanganyika na zanzibar ulikuwa na makubaliano katika mambo fulani wanaiyaita MAMBO YA MUUNGANO, hii ni pamoja na
MAMBO YA NJE
MAMBO YA ULINZI
ETC.
kwahiyo utaona kuwa zanzibar haina maamuzi yoyote katika masuala ya nje ispokuwa ni kupitia serikali ya muungano, ie kama zanzibar wanataka kujiunga na OIC basi inatakiwa Jamhuri ya Muungano ijiunge na OIC.
sasa mawazo yangu ni kuwa mimi sijui madhumuni na malengo ya OIC, na kwasababu mwalimu alisha sema tanzania isijiunge na umeoja huo, bila mashaka yeyote nitamuunga mkono Mwalimu,kwa tanzania kutojiunga na jumuiya hii.
 
Wa-Zanzibar kama wanataka kujiunga na hiyo jumuiya kwa manufaa ya kiuchumi waendeleee tu, maana kama kuna tatizo na hilo shirika na dini tungeshaiona Uganda na Mozambique,

Jamhuri nzima hatuwezi kujiunga na hiyo kitu, lakini siku zote imekuwa ni tatizo ambalo inaonekana hawa wenzetu wa visiwani wanataka kutu-blackmail nalo sisi wa bara, maana tunapowazuia kuna ambalo halisemwi nalo ni kuwapa umeme bure ili wanyamaze kama Mwinyi na Mkapa, walivyokuwa wakifanya, hatuwezi ku-afford anymore hii michezo ya siasa za kitoto,

Let them go, huko kwani what is tofauti anyway?
 
Mzee Es,
maneno yako ndio ukweli na reality yenyewe... Sisi bara hatuna haja kabisa ya kufikiria Udini kwani sio kabisa tamaduni yetu... Zanzibar wamekuwa wakisagana kwa siri na nchi za kiarabu na kuna wakati Oman iliwachukua Wazanzibar kibao kuwapa uraia na sehemu ya kuishi huko Muscat. Hakuna mtu alisimama na kulaani kitendo hicho na kudai kuwa ni uvunjaji wa sheria ya Muungano. Leo hii wengi wanaanza kurudi baada ya kugundua kuwa waarabu bado ni Waarabu KWANZA kabla ya huo Uislaam.
Zanzibar wana bajeti yao ya ndani, wizara zao na mikakati yao mingi ambayo haifanani ya bara kabisa. Hoja ya Karume kama nilivyoielewa mimi ni kutaka Zanzibar ijiunge na OIC sio Tanzania nzima. Well, yameisha tokea haya sana katika michezo na matokeo yake huwa wao wanarudi kwetu.

Nitasisitiza kuwa waache hawa wasagaji wamlete huyo binti ndani, siusi tutaangalia kama kuna manufaa ktk ndoa hii laa sivyo tutaonekana sisi kuwa bwana mwenye wivu mbaya....control freak!
Hatuwezi kabisa kuwaambia Zanzibar kuwa tunachoogopa sisi ni hawa jamaa kuleta Udini ndani ya nyumba hali wao madai yao ni maendeleo yao binafsi...
As a fact kama kweli tungekuwa sisi tuko clean kabisa hata nchi zinajitangaza kuwa za kiislaam zisingepewa nafasi ya Ubalozi ndani nchini.
Iraq na Iran zilifanya mengi ya kutisha nchini kuliko hiyo jumuiya... Na hawa jamaa zetu (Wazanzibar) hawana hata akili kwani hiyo OIC imefanya nini huko Sudan, Somalia, Msumbiji n.k zaidi ya kuwaona kuwa ni hawa ni Ma zenjbari (watu weusi) wanaojipendekeza. Hiyo hiyo OIC inaunga mkono serikali inayoshika madaraka Iraq na endorsement ya ku- promote national dialogue iliyotungwa na Marekani... Kiongozi wao mkubwa ni Saudia chini ya Marekani.
Hawa OIC ni business people, they care less about the religion. Kuwait, Bahrain na UAE ni wanachama nendeni huko mkajionee mwenyewe jinsi wanavyojirusha!
 
Napendekeza Tanzania ijiunge OIC na Sheria ya Kadhi ipitishwe na Bunge. Hili ni muhimu katika kuondoa manung'uniko ya sehemu ya jamii yetu kukandamizwa kidini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom