Augustine Moshi
JF-Expert Member
- Apr 22, 2006
- 2,556
- 1,385
Haya mawazo hapa chini niliyaposti kwenye Maoni.org, lakini kwa vile haifukuti, hakuna aliyejibu. Kwa vile nataka mawaidha kuhusu hili dukuduku langu, nimeona niposti hapa. Kumradhi kama nimefanya kosa.
====================================
Naona viongozi wa ngazi za juu za CCM sasa ni used soldiers. Mwenyekiti ni Kanali Kikwete, Katibu Mkuu ni Luteni Makamba na Naibu Katibu Mkuu ni Kapteni Mwanri. Haina neno.
Nina duku duku kuu: JK anapoteua viongozi, lazima aangalie asije akafanya watu wadhani ni mdini. Au JK ni mdini? Mbona safu karibu yote ya viongozi wa CCM alioteua ni wa dini moja? Kwa sasa, Mwenyekiti (JK) ni Muislamu, Katibu Mkuu (Makamba) ni Muislamu, Naibu Katib wakuu wawili (Jaka Mwanri na Saleh Feruz) ni Waisalamu, Mweka Hazina (Rostam Aziz) ni Muislamu, Organizing Secretary (Kidawa Hamad) ni Muislamu, Publicity Secretary - Internationa Affairs (Asha-Rose), nadhani naye ni Muislamu.
Huenda JK sii mdini, bali amejikuta tu akiteua watu wa dini moja. Na alipochagua mabalozi wapya alijikuta vile vile anakumbuka tu zaidi watu wa dini moja?
Si vema JK akaleta hisia za kidini. Huenda hakukusudia kupendelea dini moja, lakini ameleta hisia hizo. Ni vema akawa makini, ili hisia hizo zisiendelee.
Naamini kwamba ni vema kusema matatizo yanaweza kutokea wapi, kabla hayajatokea. Lazima tulinde amani tuliyo nayo kwa kusema yale ambayo tunadhani yanaweza kuleta matatizo baadaye.
Augustine Moshi
====================================
Naona viongozi wa ngazi za juu za CCM sasa ni used soldiers. Mwenyekiti ni Kanali Kikwete, Katibu Mkuu ni Luteni Makamba na Naibu Katibu Mkuu ni Kapteni Mwanri. Haina neno.
Nina duku duku kuu: JK anapoteua viongozi, lazima aangalie asije akafanya watu wadhani ni mdini. Au JK ni mdini? Mbona safu karibu yote ya viongozi wa CCM alioteua ni wa dini moja? Kwa sasa, Mwenyekiti (JK) ni Muislamu, Katibu Mkuu (Makamba) ni Muislamu, Naibu Katib wakuu wawili (Jaka Mwanri na Saleh Feruz) ni Waisalamu, Mweka Hazina (Rostam Aziz) ni Muislamu, Organizing Secretary (Kidawa Hamad) ni Muislamu, Publicity Secretary - Internationa Affairs (Asha-Rose), nadhani naye ni Muislamu.
Huenda JK sii mdini, bali amejikuta tu akiteua watu wa dini moja. Na alipochagua mabalozi wapya alijikuta vile vile anakumbuka tu zaidi watu wa dini moja?
Si vema JK akaleta hisia za kidini. Huenda hakukusudia kupendelea dini moja, lakini ameleta hisia hizo. Ni vema akawa makini, ili hisia hizo zisiendelee.
Naamini kwamba ni vema kusema matatizo yanaweza kutokea wapi, kabla hayajatokea. Lazima tulinde amani tuliyo nayo kwa kusema yale ambayo tunadhani yanaweza kuleta matatizo baadaye.
Augustine Moshi