Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,196
- 10,708
Hivi majuzi kumekuwa na minong’ono chini kwa chini kwenye korido za wasomi na mitandao ya kijamii. Watu wanahoji: "Kwanini teuzi za Makamu Wakuu wa Vyuo Vikuu (Vice Chancellors) hapa nchini zimekaa mrengo fulani wa kiimani?
Mbona pale SUZA pamejaa kanzu , na kule SAUT kumejaa mapadre na masista?" Wataalamu wa kulalamika wameshaanza kunyoosha vidole na kupiga kelele za "Udini pamoja na Ubaguzi!"
Lakini kabla hujabeba bango lako na kwenda kulalamikia mabaraza la Vyuo Vikuu, hebu kwanza tulia, shusha pressure, na kunywa maji kidogo. Kuna tofauti kubwa sana kati ya "Ubaguzi wa Kidini" na "Misingi ya Uanzishwaji wa Taasisi."
Kutanana na Profesa kwa majina ya Prof Mohamed Al Bilal, ameteuliwa kuwa Vice Chancellor wa Chuo Kikuu cha Katoliki cha Bugando (CUHAS). Siku ya kikao cha tathmini ya chuo majira ya saa saba kasoro, anasimama mbele ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC). Maaskofu wametulia na misalaba yao kifuani, kisha Professor Bilal anaanza ripoti yake kwa kusema, "Bismillahir Rahmanir Rahim..."
Hapo ndipo utakapogundua kuwa kuna maeneo yameumbwa kubaki na wazawa, si kwa sababu ya chuki, bali kwa muundo wa kiutawala na kiroho! Kama anavyosema mchambuzi mmoja, nafasi kama hiyo ni heri ukamuachia tu Prof. Erasmus Kamugisha, kwa sababu anaijua lugha, itifaki, na misingi ya waajiri wake bila kuwepo kwa mgongano wa kiitikadi.
Huwezi kuamka tu na kusikia asubuhi moja kuwa Sister kutoka shirika la Daughters of Charity ameteuliwa kuwa Vice Chancellor wa Morogoro Muslim University (MMU). Ukiona hivyo, ujue dunia imeisha au kuna mtu amekosea kuchapa barua ya uteuzi!
Kuna kisa cha kijana mmoja mtaani aliyekuwa akilalamika kuwa wataalamu wengi kutoka Zanzibar wananyimwa fursa za kuwa Chaplain (Mlezi wa Kiroho) kwenye vyuo vikuu vya Tanzania Bara. Alipoulizwa, "Kwani hao Wazanzibar unaowasemea ni Wakristo?" akajibu kwa kujiamini: "Kwani Muislamu hawezi kuwa Chaplain?"
Hapo ndipo unapoishia kucheka kwa sauti ya juu hadi majirani wanashangaa. Hii ni sawa na kuomba nafasi ya kuwa Imam wa msikiti wa Al-Noor huku ukiwa umeshika Rozari mkononi pamoja na Biblia. Huko si kuitafuta ajira, ni kuitafuta miujiza!
Tukiacha utani kando, ukweli wa mambo upo wazi. Vyuo kama Tumaini Makumira vilijengwa kwa jasho na maono ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (ELCT). Vivyo hivyo, vyuo kama SAUT, CUHAS, pamoja na RUCU, vyuo hivi ni matunda ya maono ya Kanisa Katoliki. Kikatiba na kiutendaji, vyuo hivi vina misingi ya kidini (faith-based institutions) ambayo lazima ilindwe na viongozi wakuu wa taasisi hizo.
Hata hivyo, tofauti na dhana ya ubaguzi, vyuo hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa Watanzania wote. Kwenye nafasi za kitaaluma—kama vile Wahadhiri, Maprofesa, na Wasaidizi wa Wahadhiri —utakutana na mchanganyiko wa kila dini. Muislamu anafundisha SAUT bila shida, ila kwa hali ilivyo ni nadra sana kuona Mkristo anafundisha MMU au SUZA, na kama wapo basi ni kwa kiwango kidogo sana.
Kuna watu hawajapata kusali makanisa ya ELCT wala Roman Catholic ila wanafanya kazi SAUT, CUHAS pamoja na RUCU. Ila vyuo kama SUZA ina asilimia 85 ya wafanyakazi Waislamu.
kumbuka tu: Kila chombo na mmiliki wake, na kila ripoti ina hadhira yake sahihi! HII NI KILA MTU ASHINDE MECHI ZAKE!
Mbona pale SUZA pamejaa kanzu , na kule SAUT kumejaa mapadre na masista?" Wataalamu wa kulalamika wameshaanza kunyoosha vidole na kupiga kelele za "Udini pamoja na Ubaguzi!"
Lakini kabla hujabeba bango lako na kwenda kulalamikia mabaraza la Vyuo Vikuu, hebu kwanza tulia, shusha pressure, na kunywa maji kidogo. Kuna tofauti kubwa sana kati ya "Ubaguzi wa Kidini" na "Misingi ya Uanzishwaji wa Taasisi."
Kutanana na Profesa kwa majina ya Prof Mohamed Al Bilal, ameteuliwa kuwa Vice Chancellor wa Chuo Kikuu cha Katoliki cha Bugando (CUHAS). Siku ya kikao cha tathmini ya chuo majira ya saa saba kasoro, anasimama mbele ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC). Maaskofu wametulia na misalaba yao kifuani, kisha Professor Bilal anaanza ripoti yake kwa kusema, "Bismillahir Rahmanir Rahim..."
Hapo ndipo utakapogundua kuwa kuna maeneo yameumbwa kubaki na wazawa, si kwa sababu ya chuki, bali kwa muundo wa kiutawala na kiroho! Kama anavyosema mchambuzi mmoja, nafasi kama hiyo ni heri ukamuachia tu Prof. Erasmus Kamugisha, kwa sababu anaijua lugha, itifaki, na misingi ya waajiri wake bila kuwepo kwa mgongano wa kiitikadi.
Huwezi kuamka tu na kusikia asubuhi moja kuwa Sister kutoka shirika la Daughters of Charity ameteuliwa kuwa Vice Chancellor wa Morogoro Muslim University (MMU). Ukiona hivyo, ujue dunia imeisha au kuna mtu amekosea kuchapa barua ya uteuzi!
Kuna kisa cha kijana mmoja mtaani aliyekuwa akilalamika kuwa wataalamu wengi kutoka Zanzibar wananyimwa fursa za kuwa Chaplain (Mlezi wa Kiroho) kwenye vyuo vikuu vya Tanzania Bara. Alipoulizwa, "Kwani hao Wazanzibar unaowasemea ni Wakristo?" akajibu kwa kujiamini: "Kwani Muislamu hawezi kuwa Chaplain?"
Hapo ndipo unapoishia kucheka kwa sauti ya juu hadi majirani wanashangaa. Hii ni sawa na kuomba nafasi ya kuwa Imam wa msikiti wa Al-Noor huku ukiwa umeshika Rozari mkononi pamoja na Biblia. Huko si kuitafuta ajira, ni kuitafuta miujiza!
Tukiacha utani kando, ukweli wa mambo upo wazi. Vyuo kama Tumaini Makumira vilijengwa kwa jasho na maono ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (ELCT). Vivyo hivyo, vyuo kama SAUT, CUHAS, pamoja na RUCU, vyuo hivi ni matunda ya maono ya Kanisa Katoliki. Kikatiba na kiutendaji, vyuo hivi vina misingi ya kidini (faith-based institutions) ambayo lazima ilindwe na viongozi wakuu wa taasisi hizo.
Hata hivyo, tofauti na dhana ya ubaguzi, vyuo hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa Watanzania wote. Kwenye nafasi za kitaaluma—kama vile Wahadhiri, Maprofesa, na Wasaidizi wa Wahadhiri —utakutana na mchanganyiko wa kila dini. Muislamu anafundisha SAUT bila shida, ila kwa hali ilivyo ni nadra sana kuona Mkristo anafundisha MMU au SUZA, na kama wapo basi ni kwa kiwango kidogo sana.
Kuna watu hawajapata kusali makanisa ya ELCT wala Roman Catholic ila wanafanya kazi SAUT, CUHAS pamoja na RUCU. Ila vyuo kama SUZA ina asilimia 85 ya wafanyakazi Waislamu.
kumbuka tu: Kila chombo na mmiliki wake, na kila ripoti ina hadhira yake sahihi! HII NI KILA MTU ASHINDE MECHI ZAKE!