Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Diversion >>>

Ukiangalia 'series' ya 'Prison Break', utaona ni kiboko ya 'series...'

Nafananisha (si kimaudhui) na Kitabu cha Mashimo ya Mfalme Suleiman (King Solomon Mines)

Lakini ukiangalia 'series' ya 24 ndio utajuwa kuwa kumbe 'prison break' ni kama 'intro' tu...

Nafananisha na Kitabu cha Hadith za Allan Quatermain (si kimaudhui)

Hakika ni utunzi ulio bora kabisa.
 
... Perfumed Garden!!! Hiki kitabu niliwahi kusikia sifa zake but sijawahi kisoma, hebu funguka kiduuchu mkuu..



Duh...nasita kidogo kueleza kwa kina, kwani kwanza sijui umri wako na pili ni kwamba nadhani upo wakati kitabu hiki kama kumbukumbu zangu ni sahihi kiliwahi kupigwa marufuku...yaani Enzi zile za miaka ya 70 na kuendelea kidogo...Lakini kwa ufupi kitabu hiki kimeandikwa nadhani kwa lugha ya Kiaarabu lakini kimetafsiriwa in English na Sir Richard Burton...katika cover yake ya juu kimeandikwa title ya kitabu yaani THE PERFUMED GARDEN na pia maneno yafuatayo: '...The most daring book ever written on the THE ARABIAN ART OF MAKING LOVE'....sasa baada ya maelezo haya sasa kazi kwako...mimi siendelei zaidi, labda nigusie jambo moja pia nalo ni kwamba huyu SIR RICHARD BURTON aliyetafsiri kitabu hiki ndiye mtunzi (but , Iam not so sure) wa kitabu kingine maarufu kwa mambo ya mapenzi cha KAMA SUTRA (ambacho nadhani kinaelelezea mapenzi ya kihindi)...ila kumbuka kuna videos za KAMA SUTRA... Kumbuka pia kuwa vitabu hivi ni vya zamani, lakini kwa hakika bado ni vizuri kweli kweli, na havifai kwa watoto wadogo (kwa maoni yangu) ila kwa kweli ni vizuri...na miaka hiyo ya wakati wetu (yaani miaka ya 70 na miaka ya 80) vitabu hivi vilikuwa 'maarufu' kwa vijana (teenagers na wale wenye miaka ya 20 hadi 30) ....
 
1954! KAMA SUTRA nilikisoma 1980's. Nilikuwa kijana barubaru. Machejo niliyo yapata mule nili apply kwa GF wangu. Alichanganyikiwa. Vitabu vya zamani SHIKAMOO
 
Duh! Kisa kilianzia pale lamu baada ya kuongea na bwana balozi ndie aliwapa maelezo ya kwenda kuonana na bwana makenzie aishie mwishoni mwa mto tana akawaamibia inabidi muwe na wapagazi wa kuwabebea vitu vyenu nje ya mji kuna wakazi walikuja na bwana wao alie kuwa amekwenda kuupanda mlima kilimanjaro lakini wakati wa kurudi akapata maradhi ya homa na kufariki nendeni mkawaone .
Asubuhi kuliko pambazuka tukaenda tuliwakuta watatu wamekaa nje nao sura zao zilikuwani zenye kutumainiwa lakini loh !tulipo waeleza shauri letu walikataa kabisa wakasema bado wana uchungu wa kufiwa bwana wao nikawauliza nimeambiwa mpo sita wengine wapo wapi?
Wakajibu wamelala kwani usingizi huondoa uchovu na pia huleta usahaulifu lakini walikubali kuwaamsha.
Wale wawili kati ya wale watatu walikuwa wanafanana na wale watatu niliosema nao mwanzoni ila yule wa tatu nikasema huyu si mkazi ni mzulu halisi alitoka huku ameuweka mkono wake mdomoni labda apige mwayo alipotoa mkono nikaona kinywa cha ucheshi cha kizulu na macho madogo ila makali kama mwewe.
Japo kuwa nilikuwa sijamuona kwa muda wa miaka 12 nilimtambua na kumsalimia kwa sauti ndogo kwa lugha ya kizulu
Hujambo umslopogaaz?
Yule mtu mkubwa nusura shoka lake la vita lianguke
Mkuu !mkuu baba! Makumazahn! Mzee mwindaji! Akeshae! Hodari mwepesi! Rafiki mwaminifu! Muuwaji wa simba mla tembo! Mkuu mkuu baba! Ama kweli ile methali ya kikwetu isemayo milima yaikutani ila wanadamu hukutana ni ya kweli kabisa na tena ni yenye busara! Tazama alikuja tarishi kutoka natal na kusema makumazahn amefariki na nchi haitomuona tena! maneno haya yameongewa zamani ila tizama leo baba yangu katika nchi ngeni kama hii namuona tena makumazahn hakika ndie yeye bila shaka! Manyoya ya mzee simba yamekwisha ingia mvi! Lakini macho na meno yake ni makali vilevile kama zamani! Mkuu baba unakumbuka namna ulivyo pitisha risasi penye jicho la nyati aliekuwa akishambulia?
Baba Mkuu Guasa...
Kutwa nzima sina umeme.

Si kama LUKU yangu imakata, la hasha.
TANESCO kazima!

Ndiyo maana nimechelewa kuja barzani.
Ahsante umenileta kwenye, ''kubonga.''
 
Guasa! Kitabu hiki unacho au maneno haya unayatoa kichwani (creaming)? Hii kweli Cambridge kama ya Mohamed
 
Duh...nasita kidogo kueleza kwa kina, kwani kwanza sijui umri wako na pili ni kwamba nadhani upo wakati kitabu hiki kama kumbukumbu zangu ni sahihi kiliwahi kupigwa marufuku...yaani Enzi zile za miaka ya 70 na kuendelea kidogo...Lakini kwa ufupi kitabu hiki kimeandikwa nadhani kwa lugha ya Kiaarabu lakini kimetafsiriwa in English na Sir Richard Burton...katika cover yake ya juu kimeandikwa title ya kitabu yaani THE PERFUMED GARDEN na pia maneno yafuatayo: '...The most daring book ever written on the THE ARABIAN ART OF MAKING LOVE'....sasa baada ya maelezo haya sasa kazi kwako...mimi siendelei zaidi, labda nigusie jambo moja pia nalo ni kwamba huyu SIR RICHARD BURTON aliyetafsiri kitabu hiki ndiye mtunzi (but , Iam not so sure) wa kitabu kingine maarufu kwa mambo ya mapenzi cha KAMA SUTRA (ambacho nadhani kinaelelezea mapenzi ya kihindi)...ila kumbuka kuna videos za KAMA SUTRA... Kumbuka pia kuwa vitabu hivi ni vya zamani, lakini kwa hakika bado ni vizuri kweli kweli, na havifai kwa watoto wadogo (kwa maoni yangu) ila kwa kweli ni vizuri...na miaka hiyo ya wakati wetu (yaani miaka ya 70 na miaka ya 80) vitabu hivi vilikuwa 'maarufu' kwa vijana (teenagers na wale wenye miaka ya 20 hadi 30) ....
Kwanza nikushukuru mkuu for taking your time to respond on this. Pili kuhusu age worry not coz kama ni mmoja wa wapenzi wakubwa wa vitabu vya akina Umsolopagaas basi jua mvua kadhaa zimenipitia. Tatu nashukuru pia nimeshakipata hicho kitabu humu kuna member amekiweka hapa, asante.
 
Guasa! Kitabu hiki unacho au maneno haya unayatoa kichwani (creaming)? Hii kweli Cambridge kama ya Mohamed
Kichwani ndugu yangu miaka imebaki kulikumbuka kava lake lilikuwa rangi ya zambarau na weupe katikati kwa kweli mshana katurudisha katika kumbukumbu tamu.
 
Back
Top Bottom