Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Baba Mkuu Guasa...
Kutwa nzima sina umeme.

Si kama LUKU yangu imakata, la hasha.
TANESCO kazima!

Ndiyo maana nimechelewa kuja barzani.
Ahsante umenileta kwenye, ''kubonga.''
Pole maalimu wangu tatizo hilo la umeme ni changamoto kubwa.
Kisha nikamwambia nyamaza wewe maneno yako yanayobubujika na kutugharikisha hapa kwanza lazima niseme hakuna tabia inayoniudhi kama ya Wazulu ya KUBONGA(bongering )kusifia kitu kupita kiasi tulipo achana ulikuwa mfalme katika nchi ya uzulu unafanya nini katika nchi ngeni hii ?
 
Baba Mkuu Guasa...
Kutwa nzima sina umeme.

Si kama LUKU yangu imakata, la hasha.
TANESCO kazima!

Ndiyo maana nimechelewa kuja barzani.
Ahsante umenileta kwenye, ''kubonga.''
Umslopogaaz nimekujua toka zamani wapenda uwezo na nguvu nyingi tabia hii ipo katika damu yako mwanzoni ulipofanya shauri juu ya ketswayo bin mpande nilikuonya ukanisikiliza lakini sasa umechimba shimo kwa mikono yako na kwa miguu yako mwenyewe umetumbukia kwani nani awezae kuangulia nuru iliyokuwepo mwaka jana ?au kurudisha maneno yaliyo kwisha semwa? au kuokoa roho zilizokwisha angamia ?yaliyo mezwa na wakati hayarudi na kisa chako na kisahauliwe! Tena ulijulikana shujaa na nyakati za usiku watuwalipokaa na kuuzunguuka moto na kutaja khabari za matendo yako je wamuona huyu? Jina lake inkubu nae ana nguvu kama wewe aweza kukuchukua na kukutupa begani pake tena wamuona yule mwenye rodi jina lake bougwan nae ni mtu mwema muaminifu.
Basi sisi sote tumepanga kwenda safari dongo egere kwani tumechoka kukaa mahala pamoja na kuzunguukwa na mambo yale yale kila siku zimepita tuliongozana na mtu kama wewe UMBOPA katika nchi ya ukukuana tazama tulipo achana nae alikuwa na jeshi lenye vikosi ishirini na kila kikosi kina askari elfu tatu wanasubiri amri yake ukiongozana nasi utakuwa na amri juu wa wapagazi wetu sijui kitakacho kukuta wewe je unaweza kuongozana nasi na kubahatisha ajali au unaogopa umslopogaaz ?
Maneno unayosema si ya kweli makumazahn ila ni aibu kusema ni uso mzuri wa mwanamke ndio ulio nihaini na sasa tutaona mambo kama tuliyo yaona zamani katika nchi ya uzulu tulipo winda na kupigana makumazahn ?
Ndio nitakuja ikiwa ni kwa maisha ama kwa mauti ni mamoja kwangu mapigano yaanguke upesi na damu imwagike tu.
 
Kuna baadhi ya vitu huwakutanisha watu kiroho hii post ni kimojawapo! najiona mimi wa wakati huo nikisoma hivi vitabu mstari kwa mstari
 
Kwanza nikushukuru mkuu for taking your time to respond on this. Pili kuhusu age worry not coz kama ni mmoja wa wapenzi wakubwa wa vitabu vya akina Umsolopagaas basi jua mvua kadhaa zimenipitia. Tatu nashukuru pia nimeshakipata hicho kitabu humu kuna member amekiweka hapa, asante.


mkuu hebu ni-mention kwenye hiyo link tafadhali!!!
 
Nimekumbuka mbali sana. INKUBU! Enzi zileee unaenda Maktaba ya Mkoa unapewa kadi(3)za usajili, unampelekea mzazi anakusainia kisha unapeleka shule kwa mkuu anakusainia na kugonga muhuri.
Tayari unakuwa member wa library. Kazi yako hapo ni kuazima vitabu. Kila baada ya wiki mbili unarudisha kitabu library na kuchukua kingine
 
Umslopogaaz nimekujua toka zamani wapenda uwezo na nguvu nyingi tabia hii ipo katika damu miaka ya nyuma nilikuonya juu ya ketswayo bin mpande ukanisikiliza lakini sasa umechimba shimo kwa mikono yako na kwa miguu yako mwenyewe umetumbukia kwani nani awezae kuangulia nuru iliyokuwepo mwaka jana ?au kurudisha maneno yalivyo kwisha sema? au kuokoa roho zilizokwisha kufa ?yaliyo mezwa na wakati hayarudi na kisa chako na kisahauliwe! Tena ulijulikana shujaa na nyakati za usiku watu waliuzunguuka moto na kutaja khabari za matendo yako je wamuona huyu? Jina lake inkubu nae ana nguvu kama wewe aweza kukuchukua na kukutupa begani pake tena wamuona yule mwenye rodi jina lake bougwan nae ni mtu mwema muaminifu.
Basi sisi sote tumepanga kwenda safari dongo egere kwani tumechoka kukaa mahala pamoja na kuzunguukwa na mambo yale yale kila siku zimepita tuliongozana na mtu kama wewe UMBOPA katika nchi ya ukukuana tazama tulipo achana nae alikuwa na jeshi lenye vikosi ishirini na kila kikosi kina askari elfu tatu wanasubiri amri yake ukiongozana nasi utakuwa na amri juu wa wapagazi wetu sijui kitakacho kukuta wewe je unaweza kuongozana nasi na kubahatisha ajali au unaogopa umslopogaaz ?
Maneno unayosema si ya kweli makumazahn ila ni aibu kusema ni uso mzuri wa mwanamke ndio ulio nihaini na sasa tutaona mambo kama tuliyo yaona zamani katika nchi ya uzulu tulipo winda na kupigana makumazahn ?
Ndio nitakuja ikiwa ni kwa maisha ama kwa mauti ni mamoja kwangu mapigano yaanguke upesi na damu imwagike tu.
Guasa...
Ahsante sana umenikumbusha ''Inkubu,'' Bwana Good.
 
Nimekumbuka mbali sana. INKUBU! Enzi zileee unaenda Maktaba ya Mkoa unapewa kadi(3)za usajili, unampelekea mzazi anakusainia kisha unapeleka shule kwa mkuu anakusainia na kugonga muhuri.
Tayari unakuwa member wa library. Kazi yako hapo ni kuazima vitabu. Kila baada ya wiki mbili unarudisha kitabu library na kuchukua kingine
Ipogolo,
Nami umenisafirisha hadi 1967 St. Joseph's Convent, Dar es Salaam.
Mwalimu wetu wa English Mrs. Grant.

Mumewe na yeye alikuwa mwalimu vilevile Chang'ombe Teacher's
College.

Hawa walikuja katika mradi maalum wa British Council wa kusomesha
Kiingereza.

Mrs. Grant ndiye aliyetuambia kuwa ili tukijue vyema Kiingereza ni lazima
tuwe tunasoma vitabu hivyo akatuambia tujiunge na Tanganyika Library.

Hii ilikuwa Mtaa wa Makunganya mbele ya Bilicinas.
Siwezi kueleza raha niliyopata katika maktaba ile.

Siku zile serikali ilikuwa na uwezo.
Maktaba ilikuwa na kila aina ya vitabu.

Hapa pakawa ni ''second home.''
Nikiingia saa nane nashtuka saa 12 jioni naangalia nje taa zinawaka.

Mimi nikiishi Libya Street Kisutu.
Kwa hiyo natembea kurudi nyumbani nina vitabu nimechukua.

Haya ndiyo yalikuwa maisha yangu.

Kokote duniani niendapo nahakikisha kuwa nimekwenda bookshop kuangalia
kuna kipi kipya.

Nikiwa Uwanja wa ndege pia nitaangalia bookshop mna kipi.
Msiba wanetu wanakusanya DVD.
 
Pole maalimu wangu tatizo hilo la umeme ni changamoto kubwa.
Kisha nikamwambia nyamaza wewe maneno yako yanayobubujika na kutugharikisha hapa kwanza lazima niseme hakuna tabia inayoniudhi kama ya Wazulu ya KUBONGA(bongering )kusifia kitu kupita kiasi tulipo achana ulikuwa mfalme katika nchi ya uzulu unafanya nini katika nchi ngeni hii ?
Guasa...
Wewe mtu una ghasia sana wewe!
 
Pole maalimu wangu tatizo hilo la umeme ni changamoto kubwa.
Kisha nikamwambia nyamaza wewe maneno yako yanayobubujika na kutugharikisha hapa kwanza lazima niseme hakuna tabia inayoniudhi kama ya Wazulu ya KUBONGA(bongering )kusifia kitu kupita kiasi tulipo achana ulikuwa mfalme katika nchi ya uzulu unafanya nini katika nchi ngeni hii ?
Jamani nitapata wapi hiki kitabu.?
 
Maalimu hata pilipili huwasha lakini ndio raha yake hiyo si waona faida tunayo ipata jinsi unavyofunguka na kutoa khabari mbalimbali mungu akubariki.
Guasa...
Sikiza bwana.
Ukishafika umri wa uzee kama wangu kuna vitu viwili havikushindi.

Cha kwanza kulala na cha pili kuzungumza.

Mimi mwenyewe uwezo wa kuja na jipya umepungua sana lakini
mtu akinishtua ndipo kumbukumbu zinarejea.
 
Pia kuna mdau humu katuletea kile cha kingereza pana tofauti kubwa kuanzia majina badala ya wakazi muandishi katumia wakwafi na badala ya wajivuni katumia maasai na kikubwa kuna character aitwae Alphonse hayupo katika kitabu cha kiswahili.
Ila cha kwetu ni chetu cha kiswahili kina swagger (swaga )flan hivi inasisimua sana.
 
Guasa...
Sikiza bwana.
Ukishafika umri wa uzee kama wangu kuna vitu viwili havikushindi.

Cha kwanza kulala na cha pili kuzungumza.

Mimi mwenyewe uwezo wa kuja na jipya umepungua sana lakini
mtu akinishtua ndipo kumbukumbu zinarejea.
Twalijua hilo maalimu ndo maana huanzisha vita japo twajua silaha hatuna ila twachokoza mbabe atoke huko na kutupa mbinu.Maalimu huburudika sana kwa historia ambayo humwaga humu jf ni barza kubwa na adhwimu.
 
Back
Top Bottom