Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Guasa...
Mwaga vitu...
Naisubiri ile ya ''kubonga.''

We mtu hatari sana kaka.
Hizi hazina za kale ndugu yangu.
Duh! Kisa kilianzia pale lamu baada ya kuongea na bwana balozi ndie aliwapa maelezo ya kwenda kuonana na bwana makenzie aishie mwishoni mwa mto tana akawaamibia inabidi muwe na wapagazi wa kuwabebea vitu vyenu nje ya mji kuna wakazi walikuja na bwana wao alie kuwa amekwenda kuupanda mlima kilimanjaro lakini wakati wa kurudi akapata maradhi ya homa na kufariki nendeni mkawaone .
Asubuhi kuliko pambazuka tukaenda tuliwakuta watatu wamekaa nje nao sura zao zilikuwani zenye kutumainiwa lakini loh !tulipo waeleza shauri letu walikataa kabisa wakasema bado wana uchungu wa kufiwa bwana wao nikawauliza nimeambiwa mpo sita wengine wapo wapi?
Wakajibu wamelala kwani usingizi huondoa uchovu na pia huleta usahaulifu lakini walikubali kuwaamsha.
Wale wawili kati ya wale watatu walikuwa wanafanana na wale watatu niliosema nao mwanzoni ila yule wa tatu nikasema huyu si mkazi ni mzulu halisi alitoka huku ameuweka mkono wake mdomoni labda apige mwayo alipotoa mkono nikaona kinywa cha ucheshi cha kizulu na macho madogo ila makali kama mwewe.
Japo kuwa nilikuwa sijamuona kwa muda wa miaka 12 nilimtambua na kumsalimia kwa sauti ndogo kwa lugha ya kizulu
Hujambo umslopogaaz?
Yule mtu mkubwa nusura shoka lake la vita lianguke
Mkuu !mkuu baba! Makumazahn! Mzee mwindaji! Akeshae! Hodari mwepesi! Rafiki mwaminifu! Muuwaji wa simba mla tembo! Mkuu mkuu baba! Ama kweli ile methali ya kikwetu isemayo milima haikutani ila wanadamu hukutana ni ya kweli kabisa na tena ni yenye busara! Tazama alikuja tarishi kutoka natal akalia na kusema makumazahn amefariki na nchi haitomuona tena! maneno haya yameongewa zamani ila tizama leo baba yangu katika nchi ngeni tena yenye harufu mbaya kama hii namuona tena makumazahn hakika ndie yeye bila shaka! Manyoya ya mzee mbweha yamekwisha ingia mvi! Lakini macho na meno yake bado ni makali vilevile kama zamani! Mkuu baba unakumbuka namna ulivyo pitisha risasi penye jicho la nyati aliekuwa akishambulia?
 
Hicho kitabu kinaitwa " Mashimo ya mfalme Suleiman" King Solomon' s mines.
 
Legendary wa kizulu alikuwa noma sana story zake ni tamu ila zinatisha na zimejaa ukatili


Ahaaaa, sasa naelewa kwanini hawa jamaa wa South mpaka leo bado ni makatili kwao kwa wao na kwa wageni weusi pia. Yaani ni ukatili tu mpaka damu imwagike.
 
Hivi Agon alikuwa kwenye hiki kitabu au ni kile cha Mashimo ya Mfalme Suleiman?

Nafikiri huyo alikuwa kwenye kitabu cha Mashimo ya Mfalme Suleiman lakini mtunzi wa vitabu hivyo viwili alikuwa ni mmoja - Mwingereza huyo alikuwa kichwa kweli kweli, si rahisi kuamini kama adithi hizo niza kutunga!

Yote tisa, lakini binafsi naona Alan Quaterman ilikuwa kibiko zaidi, yaani tukiwa shule ya msingi unaona usiku unakawai unatanani kuche haraka uende kusoma Msolopogasi na Bwana Good na lodi yake!!

Kitabu hicho kilitafusiliwa kutoka lugha ya kingereza, Kiswahili chake kilikuwa kizuri sana, sasa sijui kwa nini Wizara ya Elimu ilikifuta badala yake wakatunga vitabu vya kusifia vijiji vya ujamaa, watendaji wakuu wa vijiji na maduka ya ushirika - ajabu kweli kweli!!! Serikali yetu ilijitumbukiza kichwa kichwa ku-copy idealogy za Warusi na Wachina za kusifia viongozi na kulaani everything Western, mpaka vitabu vya kufundisha kingereza vilivyo tungwa kwa ajili ya shule za East Africa navyo wakavipiga marufuku - wakatunga vya kwao wakiwa na lengo ka kuvuna pesa - vitabu vyenyewe ukivisoma ni sawa sawa na hakuna kabisa, alafu tunashangaa kwa nini watoto wetu kingereza kinawapiga chenga.
 
Nafikiri huyo alikuwa kwenye kitabu cha Mashimo ya Mfalme Suleiman lakini mtunzi wa vitabu hivyo viwili alikuwa ni mmoja - Mwingereza huyo alikuwa kichwa kweli kweli, si rahisi kuamini kama adithi hizo niza kutunga!

Yote tisa, lakini binafsi naona Alan Quaterman ilikuwa kibiko zaidi, yaani tukiwa shule ya msingi unaona usiku unakawai unatanani kuche haraka uende kusoma Msolopogasi na Bwana Good na lodi yake!!

Kitabu hicho kilitafusiliwa kutoka lugha ya kingereza, Kiswahili chake kilikuwa kizuri sana, sasa sijui kwa nini Wizara ya Elimu ilikifuta badala yake wakatunga vitabu vya kusifia vijiji vya ujamaa, watendaji wakuu wa vijiji na maduka ya ushirika - ajabu kweli kweli!!! Serikali yetu ilijitumbukiza kichwa kichwa ku-copy idealogy za Warusi na Wachina za kusifia viongozi na kulaani everything Western, mpaka vitabu vya kufundisha kingereza vilivyo tungwa kwa ajili ya shule za East Africa navyo wakavipiga marufuku - wakatunga vya kwao wakiwa na lengo ka kuvuna pesa - vitabu vyenyewe ukivisoma ni sawa sawa na hakuna kabisa, alafu tunashangaa kwa nini watoto wetu kingereza kinawapiga chenga.

Nilitoa comment kama hizo zako juzi wakati nachangia. Imagine mtu unalala unawaza hadithi itaendeleaje kesho. Halafu yale mashindano ya kusoma kwa sauti. Hivi vitabu wakivirudisha, kila mtoto atapenda kwenda shule na kuhudhulia vipindi vya lugha zote mbili. Nakumbuka Mr. Mtakubwa na Mr. Said the driver. Kama kuna wakubwa humu wamo, waende warudishe Bulicheka, Hekaya za Abunwasi, Alfulela ulela nk.
 
Back
Top Bottom