Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Tuliza nafsi bibie mwanaume hawezi kuwa na mwanamke mmoja haiwezekani ikiwezekana ni yesu pekee ye hakua hata na mmoja, kwakua umejua amekucheat akakiri amekuomba msamaha jaribu usimsamehe kwa haraka bali we shusha jazba mpende zaid ya jana huku ukionyesha wivu wako wazi wazi kwake,binafsi ilo lishanikuta nilikua na girl alikua haamini hata kidogo kama namcheat yes nilimcheat mara kadhaa hakujua mpaka likaja bumburuka baada ya miaka mi tatu kupita,na alijua kwa kuambiwa na rafiki yangu ,

Alikua ivo ivo ananmbia live sijisikii kuwa na wewe ananichukia kuliko,nilimsihi sana sana akaniacha lonely akidhani nitajirekebisha,kumbe ndo kaharibu nimepanua wigo sasa ni kutafuna papuchi ila angenisamehe nisingerudia
But bado ninaact wala sijamshit
 
This is so real mkuu, Sijawahi kuelewa mwanamke ukimpa nafasi 100% anaanza mapozi ya kijinga mara akunyime chiu.

Ataanza kuku dharau na kukuchukulia poa wengine wataenda mbali zaidi mwisho ataanza kuwa na secret affairs na majamaa wengine nje huko.

Ila utashangaa mwanamke huyo huyo akipata mwanaume wa kumcheat atalalamika kana utafikiria kafukuzwa duniani.
wanasema ukiwa mstaarabu mwanamke anakuona fala
 
Pole sana mamii,
Your kids comes first, ni hali ambayo almost kila mwanamke analipitia au ameshaipitia ndani ya ndoa yake,

Tofauti ni mapokeo tu, kila mtu kuna namna anavyolipokea jambo fulani na kulikubali au kutokulikubali

Kama ulivyosema ameomba msamaha, take as much time as you can na ujaribu kukubali huo ukweli, samehe, focus, maisha yaendelee,

Ukiwaza sana utajiumiza, kumbuka mna watoto wawili, labda tu nikwambie ALL MEN cheats, wametofautiana tu style ya kucheat, wengine wakecheat wanafanya siri sana hata mke hajui wala haonyeshi tofauti yoyote nyumbani, ila wengine wakianzisha mahusiano nje unagundua maana everything change for worse

Usithubutu kuwaza kuanzisha mahusiano nje, utakua unaharibu zaidi ukizingatia watoto wanahitaji mwongozo wako

Jaribu kumwomba Mungu akupe amani ya moyo,uweze kusamehe na kusahau kabisa.

Otherwise, nakupa pole sana
Uzi umeishia hapa. Nimekosa cha kuongezea.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka had basi yaan wee acha tyuuuh, khaaaah eti n nature ya mwanaume kuchepuka, sasa why anaoa? Si awe bachelor ili awapange hao demuz km njugu.
Sio kuwapa maumivu na mateso viumbe wa watu khaaaaaah, wanakera mnoooh
bora awe bachelor hahaha na wanaume waliooa ndo wanaongoza kuchepuka
 
Wao wakisalitiwa wanavyotia huruma[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] shenzi zao

Wengine hata nguvu hawana wapo hapa wanajishaua,, 'mwanamke mmoja hatoshi'' (ukisoma hapa Soma kwa sauti ya puani)
so kwa wale wenye nguvu ni sawa kuchepuka?
 
hii mada bwana! tokea siku ile ya kwanza nilitaka kukoment nikaona nisome maoni ya wadau kwanza.

ndugu mleta mada nakupa neno la faraja kwa maana ya POLE.

maoni ya wenzetu mengi yanajitosheleza na unapaswa uyazingatie. muhimu ni kujipa muda nyakati ngumu zipite,na nyakati ngumu huwa hazidumu zinapita tena mapema mno.

nina ushuhuda wa ndugu yangu ama ndugu wa mzazi wangu, mume wake wakati alipokuwa vizuri kiuchumi aliweza kumchukua binti mdogo na kuwa nae kimahusiano. mwanzoni ilikuwa kama siri hivi lakini vile mapenzi yasivyo na siri yaliweza kujulikana.

kwa miaka kumi na nane mwana ume yule alitumia nguvu nyingi kuihudumia ile familia ya mama mdogo, waliweza kuzaa watoto 2 wa nje. yule mke mkubwa pamoja na kukosa huduma muhimu na malezi madogo kwa wanae ailivumilia ili kuinusuru ndoa yake.

leo hii yule mzee ameachana na yule mwanamke wa pili familia imerudiwa na amani ilio kua haipo miaka karibu 20, na hivi karibuni wanakaribia kufanya sherehe ya miaka 50 ya ndoa.

nimewahi kuandika hapa jamii forum nikazodolewa kweli na wadada wakileo, narudia tena kusema wanawake wasiku hizi ni wepesi sana wa kubeba mambo kama haya!! natoa ushauri tena warejeeni bibi zenu waulizeni waliweza kuishi vipi na wanaume zao miaka 50 mpaka 70 ya ndoa nawengine mpaka 80.

vitu kama hivi walikutana navyo san na hata hio nafasi ya kuombwa msamaha hawakuweza kuipata na maisha yakaenda.

nitoe tena mfano mdogo kwangu binfsi, niko kwenye ndoa mwaka wa nne sasa, mke wangu ni mzazi wa miezi 3 sasa,tokea alipokua mjamzito wa mwezi wa 7 aliniomba tusishiriki kwa sababu hayuko frii kufanya hivyo, tokea kipindi kle mpaka sas ni mwezi wa sita sasa sijakutana nae, na mpaka sasa kuna miezi 3 mbele ndio nijaribu hivyo kwa sababu ni uzazi wa upasuaji ambao kwa ushauri walao inatakiwa kukutana baada ya miezi 6.

sasa kwa mwana ume alie mkamilifu hapo utamwambia nini akuelewe miezi zaidi ya 6 no sex, mimi sijafanya chochote lakini si kawaida ya mwanaume kukaa hivyo!

asilimia kubwa ya cheating kwa mwana ume mwanamke ana mchango mkubwa sana, lakini kwangu hii sio hoja, hoja warejeleeni wazazi wenu waulizeniwaliishi vipi na wenza wao?
 
Acha Uzinzi ni kujiendekeza na kutokuwa na kazi za kutosha unapata muda wote huo wa kuwa na wanawake zaidi ya mmoja.Wanaume wanaochiti wanakuwa maskini,wanakuwa na magonjwa yasiyoeleweka na kiroho hawaishi muda mrefu katika ulimwengu huu .Chunguza na wewe mwenyewe unayechti jichunguze na sio wanaume tu hata wanawake.Mnajiingizia maroho msiyoyajua kwenye miili yenu iliyo safi.Mungu alimwumba mwanamke na mwanaume basi.
Yaani fuatilia hata wanaume wengi wenye tezi dume ukirudi nyuma wengi wao ni wale wazinzi mno, hawasemagi tu ukweli

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Nyie mlifanya hivyo ni hasara yenu wenyewe!
Hata hivyo wanawake mnatunyanyasa Sana...siyo kwa uvaaji mnaovaa siku hizi I see! Tunajikaza Sana Ila huku mtaani wanaume tunategwa mitego ya Kila aina! Na kwa kweli tunajitahidi Sana kukwepa! Naomba wake zetu mtuelewe, muambizane na wanawake wenzenu wanayofanya sio poa! Hizi nguo za kuwashika na kutuachia fahari ya macho jamani mmh! Ndio maana ulinzi kutoka kwenu no muhimu! Ukishindwa kumlinda ndio hivyo Tena...usikimbie lindo kwa kutaka kufanya matukio...hapo ndio utaharibu zaidi...!
Kwahiyo wewe kila mwanamke akiwa na mavazi yasiyo na staha unategeka?
Basi huna kazi ya kufanya kama upo busy na kutafuta pesa sizani!

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom