Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

hii mada bwana! tokea siku ile ya kwanza nilitaka kukoment nikaona nisome maoni ya wadau kwanza.

ndugu mleta mada nakupa neno la faraja kwa maana ya POLE.

maoni ya wenzetu mengi yanajitosheleza na unapaswa uyazingatie. muhimu ni kujipa muda nyakati ngumu zipite,na nyakati ngumu huwa hazidumu zinapita tena mapema mno.

nina ushuhuda wa ndugu yangu ama ndugu wa mzazi wangu, mume wake wakati alipokuwa vizuri kiuchumi aliweza kumchukua binti mdogo na kuwa nae kimahusiano. mwanzoni ilikuwa kama siri hivi lakini vile mapenzi yasivyo na siri yaliweza kujulikana.

kwa miaka kumi na nane mwana ume yule alitumia nguvu nyingi kuihudumia ile familia ya mama mdogo, waliweza kuzaa watoto 2 wa nje. yule mke mkubwa pamoja na kukosa huduma muhimu na malezi madogo kwa wanae ailivumilia ili kuinusuru ndoa yake.

leo hii yule mzee ameachana na yule mwanamke wa pili familia imerudiwa na amani ilio kua haipo miaka karibu 20, na hivi karibuni wanakaribia kufanya sherehe ya miaka 50 ya ndoa.

nimewahi kuandika hapa jamii forum nikazodolewa kweli na wadada wakileo, narudia tena kusema wanawake wasiku hizi ni wepesi sana wa kubeba mambo kama haya!! natoa ushauri tena warejeeni bibi zenu waulizeni waliweza kuishi vipi na wanaume zao miaka 50 mpaka 70 ya ndoa nawengine mpaka 80.

vitu kama hivi walikutana navyo san na hata hio nafasi ya kuombwa msamaha hawakuweza kuipata na maisha yakaenda.

nitoe tena mfano mdogo kwangu binfsi, niko kwenye ndoa mwaka wa nne sasa, mke wangu ni mzazi wa miezi 3 sasa,tokea alipokua mjamzito wa mwezi wa 7 aliniomba tusishiriki kwa sababu hayuko frii kufanya hivyo, tokea kipindi kle mpaka sas ni mwezi wa sita sasa sijakutana nae, na mpaka sasa kuna miezi 3 mbele ndio nijaribu hivyo kwa sababu ni uzazi wa upasuaji ambao kwa ushauri walao inatakiwa kukutana baada ya miezi 6.

sasa kwa mwana ume alie mkamilifu hapo utamwambia nini akuelewe miezi zaidi ya 6 no sex, mimi sijafanya chochote lakini si kawaida ya mwanaume kukaa hivyo!

asilimia kubwa ya cheating kwa mwana ume mwanamke ana mchango mkubwa sana, lakini kwangu hii sio hoja, hoja warejeleeni wazazi wenu waulizeniwaliishi vipi na wenza wao?
Na umewahi fanya utafiti zamani kina mama walikuwa wanabambikia Sana kina baba watoto wasio wao,umejiuliza kwa nini,mwanamke ukimcheat akijua kovu lake ili lipone lazima litibiwe na jinsia ya kiume.ukiona unacheat halafu mkeo hajali Basi jua Kuna kidume kinamkuna kuliko wewe,ndio Ile inaitwa stage ya kulea watoto...mwanamke asipokuwa na mbadala hawezi kumove on endapo tabia za mume zimemchosha..sema wanawake wasiri Sana kuhofu ndoa kuvunjika.hakuna mwanamke mwaminifu kwa mwanaume mzinifu unapewa wa kufanana naye
 
Umeshasema n zamani na sio sasa, hebu tupishe hukoo bandiko lefu afu una andika utopolo wa zama za mababu, wakati tupo zama za wajukuu,
Wee baki na mkeo, na ujue ukicheat tyuuh akijua anapeleka nyapu nae nje kukunwa vema. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] poleeh sana.

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Wambie hao hakuna mwanamke mwaminifu kwa mwanaume mzinifu,
 
Mnajipa taabu bure
Maandiko ya Biblia yalishasema jukumu la mke ni kumtii mume wake na la mume ni kumpenda mke wake sasa ninyi siku hizi mmeamua kupenda [emoji23][emoji23][emoji23] yaani mlishavunja kanuni na mtateseka sana.Wewe ulipaswa ukae umwite umwulize kwa upole tu nini kilisabababisha akacheat atawambia na akikwambia ukweli wote usijekimbilia kuwa amekunanga ukazidisha hasira zako dhidi yake maana ndiyo zenu hampendi kuambiwa ukweli.
Wanaume wengi wanatazama sana utii na kujituma nyumbani kwa wake zao ukiteleza kidogo ni simple kumkuta mme keshaanzisha mahusiano ya temporary au permanent .Kila anachokataa mme wako usibishane nae utaumia maana huwa wana maamuzi ya kimya kimya sana na ndiyo hayo uliyoyaona.Ukimpata mwanamme asiyecheat hakikisha wajibu wako kibiblia upo kuanzia kumlinda kwa maombi na kumtii hapo utasalimika ila ukiwa hufuati kanuni hizo si rahisi kumweka mwanamme kwenye himaya yako peke yako.

Mwanamme hata akikwambia sipendi kukuona unacheka na mtu fulani ukijibu kejeli au fyongo ukidhani ni kawaida tu unaweza kula jeuri yako kimya kimya yaani hawachelewi kuhitimisha kwamba huyo mtu umemwona ni muhimu nao wakakutafutia msaidizi nakwambia wanaume mara nyingi huamua mambo kwa kutegea kutotimiza wajibu kwa wanawake wao.Huenda uliwahi kukosea mahali ila ukapuuzia tu ndiyo maana amekutendea hivyo
 
I am a man. Huu ni uongo. Tupo wanaume waaminifu.
Wengi wa waaminifu ni kwa muda kiasi gani? Maana unaweza kujitapa wewe ni mwaminifu kumbe ndoa yako ina miaka miwili tu [emoji23][emoji23]

Ukifikisha miaka 30 kwenye ndoa yako na uwe hujacheat njoo hapa useme maana naungana nawe kwenye hilo la kukataa kwamba kila man anacheat kwa msimamo wa state inayozungumziwa ni ya muda gani pia inategemea sana mkeo yupo vipi ukikutana na asiyemjua Mungu kucheat ni asilimia kubwa tu.
 
Kuna shida ipo, inawezekana nayeye hana hisia na wewe tena. Ukiwa mjuaji au haumueshimu mumeo, thats a natural consequence. Heshima kwa mwanaume ni kitu cha kwanza. Jitathmini wewe kwanza, hatuwezi kutoa hukumu kwa kusikiliza ushaidi wa upande mmoja. Tafakari
Wewe tunaungana , wanawake wanakimbilia kulaumu tu matokeo ila mara nyingi sababu wanazianzisha bila kujua.

Ukute ndiyo wale wa mara nyingi nimechoka afu wanategemea mwanamme achukulie kweli
Wengi wa wanawake wameua ndoa zao kwa kukosa maombi na utii kwa waume zao.
 
Mwanaume mkamilifu kuwa na mke zaidi ya mmoja ni jambo la kawaida sana, rejea vitabu vitakatifu Biblia na Quran Mitume walikuwa na Mke zaidi ya mmoja, zaidi silka na maumbile ya mwanaume yako hivyo nadhan unapaswa kutafakari upya, hatakuja kukaa itokee dunia hii mwanaume aridhike na mke mmoja, ila nikwamba huwa ni suala la kujiheshimu tu. Pia jambo la msingi zaidi mwanaume anapaswa kujali familia yake. Vilevile mwanaume anaweza kutoka nje ya ndoa lakini upendo wake kwako ukabaki uleule au ukazidi zaidi.
 
Bibie kwa mwanamme hupaswi kutafsiri yeye kuchepuka kuwa ni kwa kuwa hakupendi uko wrong aisee. Anaweza akawa na mchepuko ila bado akipata taarifa na we una mahusiano mengine ukawa msala na usishangae hata ukabondwa au akakurudisha kwenu kwa muda. Kiukweli sijui tumeumbwaje.
Sisi ndiyo watawala hivyo huwa hatukubali kuyaweka mataifa yetu chini ya watawala wengine yaani heri pachimbike tu
 
Japo swali wameulizwa wanawake lakini sio mbaya kwa issue sensitive kama hii na sisi wanaume tukitoa ushauri, unaweza kupata lolote jambo la kukusaidia.

Kwanza pole sana kwa hilo ulilolipitia, ila kabla ya kukupa ushauri wangu ni vyema nirejee pale pale waliposema wanaume wenzangu wengine, ili upate ufahamu ambao huenda utakusaidia kabla ya kuchukua maamuzi yoyote.

Ni hivi "Dada yangu hakuna mwanaume wa mwanamke mmoja (hatumtetei mumeo) na tunaposema kua hakuna mwanaume wa mwanamke mmoja sio kwamba hakuna wanaume waaminifu wapo lakini badala ya assumption ni vyema tuende kiuhalisia, na kiuhalisia ndio hivyo, karibu kila mwanaume ana cheat au ata ku cheat haijalishi ni mahusiano ya kawaida ama ni ndoa. Kama mwanaume anakupenda basi hautajua kama ana ku cheat atajitahidi sana akufiche ili asikuumize, akiamua kukuonyesha kwa makusudi kua ana cheat ujue hapo mapenzi hakuna tena, ila pia unaweza kumgundua kwa bahati mbaya sababu kuna sehemu kidogo kakosea mpaka kukupa nafasi ya kumgundua.

Kutokana na hali hiyo kuna mambo kadhaa lazima ujue kabla hujaamua chochote.

1. Aina ya mwanaume unayemtaka au kumfikiria kichwani kwako kiuhalisia hayupo, hivyo ukiamua kumuacha mumeo na kutafuta mwanaume mwingine hutakua haujapata solution. Hapa unatakiwa ujiulize je kama utaamua kua na mwanaume mwingine, ambapo high probability ya ku cheat ni same (sababu wanaume wote tunajuana tabia na asili yetu), nae utamuacha? Na kama ukimuacha utakua na wanaume wangapi?

2. Japo inaumiza lakini unatakiwa uwaangalie watoto wenu kwanza kabla ya kitu chochote, ukianza kujifikiria wewe before watoto wenu huo ni u selfish, mpaka mmepata watoto (umekua mama) means you are strong enough tu handle this, "kabla ya kuchukua maamuzi jiulize unataka watoto wenu waishi maisha ya namna gani, walelewe na nyie wote au mzazi mmoja + wa kambo.

Kiuhalisia, Time doesn't heal you, you heal you (muda hautakuponya, muda utakusahaulisha tu matatizo) , hapa namaanisha usijipe muda kufikiria sana kutakumaliza pole pole, unaweza kufa ukawaacha watoto wako katika mikono isiyo salama, fanya hivi "Liweke hili swala wazi (liongee) kuongea kunasaidia sana kutokomeza maumivu, ita wazazi ndugu wote wa karibu uwajulishe, muongee, kama kulia lia sana ila make sure ukitoka hapo unatoka na suluhu na unasahau.

Kama ni kumsamehe hakikisha ukiamua kumsamehe umsamehe kweli, uwe na hamu naye, u miss, umjali kama ilivyokua awali. Kama huwezi kufanya hivyo bado itaendelea kuteseka mwisho wa siku sonona au mkazo mawazo (stress) utakuua.
Ukiona huwezi kumsamehe with your pure heart bila kubaki na kinyongo moyoni basi ni vyema uachane ili kuepuka sonona, na ukiamua kuachana nae ni vyema usitafute kua na mwanaume mwingine, watunzie heshima watoto wako, mtunzie heshima mume wako hata kama hamtokua pamoja ila still atabaki kua mume wako as long as mlikula kiapo (agano) hua alifutiki hili.

Mwisho binafsi naona ni vyema kwa faida ya watoto wenu ni bora mbaki kua pamoja, sio kwamba huwezi kua na hamu nae tena, unaweza kama ukiamua kuachana na picha ya aina ya mwanaume unayemuumba kwenye taswira yako cause he is not exist, labda (Nadhani ni Yesu peke yake)

We are not born to be perfect .. We are born to be real, kama kakosea na kakuomba msamaha this means he is real why can't you give him a second chance (every human being need and deserve a second chance) if you can't do it for you do it for your kids.

*Naposema kumsamehe namaanisha msamaha sahihi, kama bado una kinyongo na maumivu ya ndani bado ujamsahe, msamaha means kuanza upya as your early days, no chuki, no vinyongo.
 
Kifupi mwanaume aliye kwenye ndoa kucheat nje kunatokana na haya Mambo:
1. Mwaka wa kwanza wa ndoa,mapenzi yanakuwa mazuri Sana,mnapeana Kila dakika ama Kila siku ama Kila wiki.ila baada ya kuzaa tu watoto,mwanamke uliyemuoa anaanza kukuwekea Sheria kukupa tendon na inatokea mnakaa hata miezi bila sex na mwanaume akiuliza anaambiwa sijisikii.kwann asiende kwa wanaompa?
2. Kila mwanamme akirudi nyumbani analetewa kero na kesi,hakuna faraja kwa kazi alizokutana nazo siku nzima,akikutana na mtu anayemtia moyo huko nje lazima acheat

Je wewe mlalamikaji,uko kwenye kundi gani Kati ya hayo mawili?

Usiziache familia yako Kisha mwanaume kucheat.Tena ulipaswa umshauri tu awe safe pindi anacheat huko na kumuuliza zaidi ungetambua hivyo na kumwambia sijapenda Kisha upendo wako uendeleee Kama mwanzo.hapo ungeifanya akili take ijiulize maswali mengi sana.
Unapomneglet ndo unaongeza link za mkiendelea kukicheat.

POLE ndo Ndoa hizo
 
Unapoteza muda kwa jambo ambalo halibadiriki,wewe umekulia kwenu the same kwake,hio ndio tabia yake halisi na usidhani unaweza kuicontrol. Nyumba ni mwanamke na wewe ndie umekuwa mkewe na anakuheshimu hilo ndio mhimu sana.
Kama anakuomba msamaha usishupaze shingo yako,msamehe na muonye,rudisha moyo,ongeza upendo.
Wengine hata huo msamaha hawaombwi.
Ukimuonya sio ataacha angalau ataficha sana hayo makando,the less you know the better.
Ukikomaa sana unaivunja ndoa mwenyewe ila ujue hata umpate nani yatajirudia tu mambo hayo.
Mwisho. Usijaribu kulipiza, mwanaume hawezi kujari kama amekucheat au lah! Joto la jiwe utaliona na rangi zake zote utaziona.
 
Walivumilia kwasababu hawakuwa na pakusemea, halafu nikwambie wamama
wazamani walizaa sana nje ya ndoa kwa taarifa yako

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
Wanadhani hao wamama walikuwa wanavumilia burebure tena walikuwa wachepukaji matata sana tena walikuwa wanazaa nje sana tu.
 
Back
Top Bottom