Mafiningo
JF-Expert Member
- Sep 5, 2016
- 4,436
- 4,646
Kaa pembeni subiri mmeo aoe halafu uje uone haja zako utazipeleka wapi.Mwenzenu yamenikuta na kusema za ukweli nashindwa kabisa kuelewa namna ya kutoka hapa na kusonga mbele.
Ni mume nilompenda sana sana sana. Mungu katujaalia two beautifull kids na mengine ambayo am greatfull for. Tuliishi kwa upendo,furaha na amani hadi miezi 8 ilopita nilipogundua kuwa nilivyomdhania mume wangu sivyo alivyo.
Kwakuwa nampenda na kumfahamu sana mume wangu, kuna kitu nilikuwa tu nakihisi hakiko sawa kwa muda. Baadae nikagundua he was cheating. Yaani sitaki kuelezea mstuko niloupata na jinsi ninaumia jamani. Japo aliomba sana msamaha and all that ila moyo wangu umekufa ganzi wapendwa.
Mume nilompenda sana kwasasa namuona kama jirani yangu tu, hata hamu nae sina kabisa na hata tendo la ndoa ni kama ananibaka tu. Tushaongea sana, tushakwenda hadi vacation sie wawili tu ila sioni kinachobadilika. Akisafiri kikazi au mimi nikisafiri najisikia amani zaidi and i dont miss him kabisa.
Kuna wakati nilimuomba some alone time nifikirie kuhusu mustakabali wa hii ndoa, alinipa huo muda na kwa kipindi hicho cha wiki moja kichwani mwangu nilishangaa kunazunguka watoto wetu tu na sio mume wangu. Sijamueleza mtu yeyote kuhusu hili hata mama yangu wala mshenga wetu ila linanitafuna hatari.
Wenzangu mnawezaje kusamehe wanaume wanaowacheat na kurudi katika hali zenu za kawaida? Maana mie kwasasa mume wangu namuonaje sijui, nae naona hali hii inamtesa ila ndio hivyo tena
Sijisikii kumpenda wala kumheshimu tena, naona kama hadeserve kwa kutokuithamini na kuivuruga ndoa yetu.
Nawe utakuwa ni mmoja wa wanaotembea na waume za watu.
Unajiunga kundi moja na anaechepuka na mmeo.