Poleni sana mama zetu , nawaheshimu sana, ndio maana huwa nikimkwaza mama au mama akinikosea mimi ndio huwa nawahi kumuomba msamaha.
(1)Nakumbuka mwaka 1996 kabini kwa wakimbizi nchi fulani hapa jirani, nikiwa mfanyakazi wa kada inayofanana na Afya dawa.. niko njiani nakwenda zangu field , ghafla namuona mama anahangaika sana ananiita kwa jian... H... ntabale , ndafuye!! means H.. nisaidie nakufa , niifika hapo na kuanza kumusaidia japo mimi sio mkunga , huku nikiita akina mama waliokua wanapita njiani , tulifanikiwa kumzalisha huyu mama na nilipokea mtoto kwa mara ya kwanza ...mama alinishukuru sana hakujali kabisa kama niliona visivyoonwa....
( 2) Kesi ya pili ni wakati tunafanya repatriation ya wakimbizi tena kesi mfano wa hii ulinitokea tena kipindi hiki huyu mama alikua mbioni akikimbia mamlaka lakini uchungu ulipomzidia hakujali tena na hakuogopa kupigwa na mamlaka alikaa chini nikawahi kumsalidia na akina mama waliokua nao wanapita mbiombio kunusuru maisha yao ... lakini walikubali kumsadia huyu mama ..mimi nikiwa mmoja wao kwa curtain ya vitenge vilivyozunguushwa tu tu kwa kushikana mikono. Allah awajaalie mama zetu