Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Niliumwa uchungu masaa mawili non stop ila niliona kama miaka kumi. Nimefika labor nikamwambia nesi chukua wembe unichane mtoto atoke maana nilihisi maumivu ya wembe ni nafuu kuliko niliyokuwa nayapata. Nashukru sikupewa kitanda, nikifika hosp hatua za mwisho moja kwa moja hadi labor kutoka kule na mtoto wangu.
 
Siyo shida @ Mkuu!
Kwa hiyo hayo mabadiliko ya homoni Kwa mama mjamzito Ndiyo yapelekee kumuuma meno Mume wake?
Hayo mabadiliko ya homoni yamfanye awe kama mwehu ?
Kama umefuatilia michango yangu Kwenye hii Mada utakuwa umeona kuwa nakubali kuwa Kwa sehemu ni Kweli hayo mnayosema yanatokea lakini pia Kwa upande mwingine yanachangiwa na mapokeo!
Labda hilo neno la mapokeo ndo halikukupendeza Ila ningelisema Kwa kiingereza naamini ungelielewa vizuri sana tu!
Kwa sehemu kubwa ni mapokeo huo ndo ukweli!
Mabadiliko ya homoni yafanye uchukie watu ikiwemo mumeo? hapana jamani!
Hii haina tofauti na watu wengi kuamini kuwa somo la hesabu ni gumu sana kitu ambacho siyo Kweli hata kidogo!

Mabadiliko ya hormones na psychology labda ungemueleza hvy angekuelewa maana psychological change ndyo inaweza kuonekana na mtu wa nje lkn hormonal changes zinaeza rokea ww usijue.

Kwa maana hiyo tunahitaji kuwa karibu sana na hawa wamama kwa kipindi chote tangu mimba itunge hadi kujifungua wanahitaji psychological support kubwa sana hata kama ana vituko lkn kwa wanaume kipindi hiki tupunguze wivu maana unaeza kuta mkeo anampenda zaidi rafiki yako kuliko ww na akawa anakuchukia sana hata simu yako hapokei ni mambo ya kawaida akijifungua tu aah wako huyo kama kawaida.

Psychological changes to pregnant women's,what's men's or community should do is to give them emotional and psychological support
 
Hivi mjamzito asipofanya mapenzi kipindi chote cha ujauzito,anaweza akapata shida kujifungua?
Hakuna kitu kama hicho, mie mtoto wangu wa kwanza mara ya mwisho nilifanya mimba ikiwa na miezi miwili baada ya hapo nikamchukia mhusika hadi dakika ya mwisho. Lkn sikuhangaika kujifungua
 
Wanasema eti ganzi inachelewesha kupona, ila jamani dah wanawake sisi tuna shida.
Mimi nikimaliza huyu najifanya kbs sielewi somo, yaan atakuwa anajisemea khs mtoto wa tatu ndio kwanza sijali
Haicheleweshi hata.
 
wanaume mnaosoma huu uzi muwaheshimu sana wanawake,
Mziki wa leba sio wa mchezo mchezo.hasa wale wanaowapa mimba vitoto vidogo wanapata mateso sana.

nilikutana nacho leba tulikua tunapokezana mayowe lakini yeye alikua analia kwa kumlaani huyo mwanaume,,yani nilikua hoi lkn nikikiangalia hako katoto roho inaniuma hata kanga ya kumfungia mtoto alikua hana!

Tangu nijue maumivu ya leba basi hua naumia sana roho nikiona mama na mtoto wanaoshi kwenye mazingira magumu,au mtoto aliezaa mtoto.Sinaga uwezo tu wa kutosha natamanigi ningekua tajiri nisaidie hasa watoto na wamama wanaoteseka kwa namna tofauti tofauti.
 
Wengi ni videko na wabishi hawataki kuwasikiliza maelekezo ya wakunga!
Ukishaangia leba kanuni ni moja tu fanya kila atakachokwambia mkunga huku ukimuomba Mungu wako kimoyomoyo !
Ukifanya hivyo hutachelewa nakwambia Mungu anakufanyia wepesi ajabu!
Unapopiga Makelele hayakusaidii na unajichelewesha mwenyewe!
Hapana, unajua kila mtu ana namna yake ya kupunguza maumivu. Mwingine akipiga kelele anaona kupata nafuu na wengine tunapenda ukimya tu.
Mie siku zangu zilipofika, sikupiga kelele wala mayowe hata sikuinua mdomo wangu kusema neno ila nilikuwa nauma meno balaa. Na kwa kufanya vile nilikuwa naona napata nafuu
 
haya tuweekeni na picha zenu za leba hapa...maana vimama vya siku hizi havijui ni siri kuongea mambo ya leba hadharani. hata hao watoto mliowazaa wanasoma humu.... hiki ndio kile kizazi ambacho hakijafundwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom