Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Habari Jf
Tukiwa tunamalizia malizia week la wanawake duniani hebu wanawake wa Jf tiririkeni kituko ulichofanya leba ulipokuwa na uchungu!!!!!


Mimi niliongea maneno yote kichwAni, mwisho nikasema namchukia ndugu yangu flAni ambaye kiuhalisia nampendaga sana

Aisee ile kitu achana nayo uchungu ulipozidi saana niliona bora nife kuliko kuendelea kuumwA namna ile,yani inafika wakati unaona kifo ndo kitu simple...

Tiririka sasa
Kwa mlivyo nadhani hayo ndo maumivu makali sana ambayo huyapitia nyie kina mama
 
Wamama nawaheshimu sana. Nakumbuka mke wangu alitaabika siku nzima akaja kujifungua siku ya pili yake tena kipindi hicho mimi nipo masomoni. Kipindi anahangaika mimi nikawa napiga simu kujua anaendeleaje yaani alikuwa mkali sijawahi kuona nilikuwa nachimbwa biti si la nchi hii.
 
Wamama nawaheshimu sana. Nakumbuka mke wangu alitaabika siku nzima akaja kujifungua siku ya pili yake tena kipindi hicho mimi nipo masomoni. Kipindi anahangaika mimi nikawa napiga simu kujua anaendeleaje yaani alikuwa mkali sijawahi kuona nilikuwa nachimbwa biti si la nchi hii.
Ahhaah mi nilimuambiaga marufuku kukanyaga hospitali ,,nikamchukia balaa lenyewe linalala usingizi mzuri mi nahangaika
 
Nakuambia shogaa siku mbili nikiona mwakaa
Ila mtoto akitoka tu maumivu yanaisha,,nesi akawa ananiona nahangaika mara natandika pale maana mvua ilikuwa inanyaesha nasikia baridi huku natokwa jasho hapo hapo
Kuna muda nilitamani wamvute wamtoe ili nipone
Nilizabwa makofi ya mapaja nikawaambia pigeni tu sisikiii maumivu,,niliwasumbua

Kuja kunyonyesha napo chuchu zinatoka vidonda mtoto akinyonya yaan zinachubuka ,,ulikuwa ukifika muda wa kunyonyesha nalia kwanza maana namdolishia mtoto nyonyo mpaka anazila kunyonya
Hiki kipindi sitaki kabisa,ntazaa wa pili lakin baadae
😡 😡 😡 😡

Wa pili nawaza sana itakuwaje
 
ahaha mm nakumbka hapo saa 2 usk nipo hoi..nikamuita Dk wa kiume !nikamwambia nisikilize vzr nachoumwa maana manesi hawatak kunpa panadol!heehe nikamweleza nitabirie dk ntazaa saa ngapi!akaniambia ww utazaa saa 11!jaman yale maumiv hayafai jaman!niliumwa uchung toka saa 1 asbh nikajiopen saa 11 alfajir !nilipelekwa labor na mume wangu !jaman nilikuwa namuuma mgongon ananiambia mbiti unaniumiza mie sielew ktu! asbh naitwa jina langu mume kaja niletea uji jaman niliangusha kilio sio cha nchi hii !bas mwenzangu akawa anacheka tu!

nilianza kutembea fresh baada ya miez 2 nilikua natembea km narudi nyuma !nikaambiwa mtoto alikalia 'masozi 'za miguu !yaan huwa tunakumbshiana na Mr nacheka hatari !najipanga nirudi tuu tena siwez ishi bila ya bbygal jaman!
 
Mmmhh shikamooh mama mie nilivyoenda leba nasikia nilisema "uwiii wanaume wote wafe" manesi wakanijibu afe wa kwangu tu maana waume zao bado wanawapenda hahahhaha sitaki kusikia leba maana akili haikuwa yangu mweehh shkamooh mama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom