Asante mkeAsante mzigua mwenzangu. Karibu baba wa kambo.
....huyo dogo akiwa raisi au waziri atajua mwenyewe
Itakua kuna sababu. Hawezi kua mwehu kiasi icho hadi akatae mtoto.Asante kaka. Tatizo sio hilo, kuna watoto wamezaliwa utasema ni copy ya baba zao lakini huyo baba bila aibu anashindwa kumuhudumia mwanae.
Kuzalisha ni kitu kingine na kulea ni kitu kingine pia, pole sana ila lea na mtoto akianza kuwa na akili mwambie ukweli kuwa unababa lakini no matunzo ili akikua ajijue kabisa mtu pekee alonae ni mamaNikiwa kama mhanga wa mwanamke alieachiwa matunzo ya mtoto bila msaada wa baba naumia sana. Hivi wanaume huwa mnawaza nini mnapotupa adhabu ya kulea watoto peke yetu na wewe baba ukiwa hai na unajiweza? Hata kama hujiwezi basi kumjali mtoto wako japo kwa kuulizia maendeleo yake mtu anashindwa kabisa.
Hivi kina kaka mmejiuliza nyie baba zenu wangewakimbia mngekuwa wapi sasa hivi? Mnajua ni chuki gani mnaweka kwa watoto wenu mliowakataa? Mnajua ni laana gani mnapata kwa Mungu kwa kukataa kutimiza wajibu wenu kama wazazi? Au mnatukomoa kwa sababu mama hawezi kumuacha mtoto wake nyuma hata apate tatizo gani?
Labda wewe na mama wa mtoto hamko sawa lakini ile hasira ya ninyi kutokua sawa baba usimkomeshe mama kwa kuacha kumtunza mwanao ukijua unamkomoa mama, pale unaemkomoa ni mtoto wako ambae ulimtafuta kwa mapenzi/tamaa zako mwenyewe.
Naandika nikiwa na uchungu mwingi sana moyoni. Mwanaume usiemtunza mwanao ona aibu na muogope Mungu wako kwa kitendo unachokifanya.
Jiulize ingekua ni dada yako au mwanao ameachwa na mwanaume alee mtoto peke yake ungejisikiaje?
KARMA IS A BITCH. Ukinifanyia mimi leo wakati unao dada na watoto wa kike jua itakuumiza na wew kwa mmoja kati ya hao kufanyiwa kama unavyofanyia wengine.
Baba mtoto wangu nimeshamlilia Mungu juu yako na nina hakika huyu mtoto ulieniachia nimlee peke yangu atanifuta machozi siku moja na utatamani akutambue kama baba yake utakua umeshachelewa.
Kaka/baba zangu baba Diamond akawe mfano kwenu, Obama aliekataliwa na baba yake mwishoni alikuja kuwa Rais wa Marekani/dunia.
Mnaowapenda au wenye hela na waume za watu?Cha ajabu mimba zetu zinakamata haraka kwa wale tunaowapenda.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] aiseeee wanawake wengne bhn![]()
Katika mazingira kama haya unampendaje mtoto wako?
Rashid ni rafik yangu aliyenipa taarifa za kujifungua kwake
Wanawake hasa wenye ajira wana matatizo sana