Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

umenikumbusha wakati mzee kastaafu akafanikiwa kujenga kibanda last minute, kwa mara ya kwanza nikapata kusikia sauti ya mvua kwenye nyumba ya bati ambayo haijawekwa ceiling it was hard, ukizingatia nimezaliwa na kukulia kwenye nyumba za sirikali za vigae.

Anyway kwa watoto wa baba yetu, we took it positive kiasi kwamba hakuna mtoto ambaye alifikisha 30yrs bila kuwa na nyumba, so tulijifunza kutokana na makosa ya mzazi; you can do the same.

Na hapo mna 'bahati pia'
kuna wengin baba anakufa wako nyumba za serikali
na mama ni housewife
mnatakiwa muhame na hamjui mnaenda wapi....acha tu
 
wakati naanza kabisa kazi fresh from chuo, kampuni niliyokuwa nafanyia ilikuwa inatujali sana wafanyakazi wake, mikopo nje nje, baada ya mwaka wenzangu wote nilioanza nao kazi wana magari mazuri mie bado naenda job na taxi but wanajua nimechukua mkopo mzuri tu, ilikuwa maulizo kila siku, nyamayao mkopo wako umepeleka wapi, hivi kwanini huna gari jamani, bla bla kibao, wengine mawazo yetu yalikuwa kushika viwanja kadhaa wao ilikuwa magari na masimu mazuri, kupanga ni kuchagua.


Wapo wazee wengi walizishika pesa nyingi wakati ambapo hata Bakhresa alikuwa masikini
yaanni ungewachukua hao wazee na kuwaweka na Bakhresa na kuwapiga picha enzi hizo
na kuja kuwaona hao wazee walipoishia ..mtu asingeamini kabisaa
 
Tulikua tunaishi nyumba za shirika ingawa tulikua na nyumba ambayo mzee alijenga enzi zake sinza..basi dingi akasema karibu nastaafu..nikistaafu woote kijijini...nataka nikapumzike na kero za dar...mama akakomaa akamwambia utaenda mwenyewe kjijini mimi na watoto wangu tutabaki mjini..nenda mwenyewe...mmmh basi dingi kupata pesa ya mafao fastaa tafuta kiwanja na kujenga nyumba ya ukweli japo kwa haraka...akafungua ofisi na gari akanunua...uzuri ni kwamba shirika lilikua halikufukuzi ndani ya nyumba mpk baada ya miezi kadhaa...ila tunamshukuru mama kwa ukali na msimamo...bila hivyo tungeenda kijijin au kurudI kwenye nyumba ya enzi zake sinza...mama akiwa legelege..mpenda anasa na kustarehe km mumewe familia huyumba...my dad had money na alikua banker wa maana..angeamua angemiliki majumba kibao mjini ukizingatia amesomea na kukulia dar..so he had every opportunity. .but ndo hivyo anasa...
 
kiukweli wazee wetu walizingua sana,ila ukweli hawawezi kukubali kuwa walikosa,unajua nchi zilizoendelea uwa vijana wanajifunza kutokana na makosa
 
The boss kaongea point leo..sijui wanaume wanasapoti kwa kumaanisha au basi tu.sababu ukiangalia,most men wako hivo.hasa hapa mjini dar,panachanganya sana watu.maisha ya kuigana na kuendekeza marafiki wasio na maendeleo..
Unakuta mtu analipwa mshahara wa kawaida tu ila mwanaume anaenda kukata kucha saluni na kusuguliwa miguu,kweli??ilimradi aonekane nae wamo kitaa.hana kiwanja wala maendeleo ya msingi,gari kakopa benki na kutwa wanawake.
Hivi mwanaume kuwa mhuni ni lazima eeh?its like imekuwa desturi mwanaume lazima apitie kipindi cha kuhangaika hovyo na women.wanaita 'phase ya ujana' wasijue hiyo ndo inadetermine uzee.ndomana maryoo wamezidi.janaume lipo lipo tu,akimuona kwenye gari utasema wa maana kumbe mkewe ndo anamuweka mjini.hana mipango,mshahara haileweki unapoishia.
mtu anaendekeza pombe,akitoka kazini lazima apitie bar.ukiwaona humu jf wanajitetea eti mbona mwanaume unakunywa bia na watoto wanaenda shule.we kila siku unaache elf 10 bar,kwa wiki ni elf 70.bado hujafanya tu kitu cha maana nayo?hapo familia yake haijatoka out karibu mwaka.ukidunduliza hizo elf 10 ukaenda vacation hata hapo ufukweni na familia,bado hujajenga kitu kweli??..
Men get serious...

Haa haaa hili dongo linatuhusu sote
me included ..
lakini kwa kuongea kama hivi inatusaidia woote
 
Hakuwa mama yetu, ila alikuwa baba yetu, ndiyo alimuacha mama yetu akaenda kuoa baada ya kupata pesa za EAST AFRICA zilipoisha akarudi home, na sisi tunamfanya kama mbwa wa kizungu anapata matumizi yote kasoro pesa.

Na usikute sasa hivi yuko kwenye maandamano ya wazee wa EAST Africa
kudai 'hela ingine' lol
 
Familia nyingi sana zimeokolewa na wamama
nyingi mno...zingine baba alikuwa boss mkubwa,mama ni wa nyumbani tu
au muuza vitumbua but ndo anakuja okoa jahazi baadae

yap!! unasema kweli hata familia yetu tuliokolewa ma mama.

halafu broda nimekuona mahali unawachana watu nimecheka ile mbaya wewee mbaya sana !!
 
Mimi naona ni dhana potofu tu hiyo. Nailinganisha na kitambi ambacho pia eti ni ishara kwamba mambo ni safi kumbe wapi!!

NN asante
na hii dhana pia inaumiza wengi mno
mtu hawezi ku afford gari
anajilazimisha kununua hata kwa mkopo,mwisho
hela ya mshahara yoote inaishia kwenye mafuta
ndo mwisho anashindwa fanya ya maana,sababu gari linam cost mno..
 
We acha tu, unaweza kumrukia vichwa baba yako mzazi.......unashindwa kuelewa ni kwanini mtu hakuweza kununua nyumba kariakoo na beach plot kawe au basi hata bahari beach.......ni ngumu sana kuwaelewa hawa watu. Alalfu anakuja kukusimulia ujinga wao....anakwambia mikocheni ilikua ni madimbi tu hata upewe bure hutaki.

sarikoki na muhinda i do feel your pain
nawaelewa mno
mimi na mzee wangu mmoja anapenda mno kusimulia
jinsi alivyokuwa anampelekea Bakhresa viatu vyake ashone
mwenyewe anaona sifa kuisimulia hiyo story
wakati sisi tunajiuliza ilikuwaje kashindwa hata robo ya robo ya mafanikio ya Bakhresa
kama alianza kushona viatu anamuona?wanatia hasira mno hawa
 
Last edited by a moderator:
Inajulikana sana
wamama wa kimanyema wengi walinunua nyumba Kariakoo kwa kuhongwa
miaka hiyo...unaweza kukuta wazee wetu wengi waligharamia nyumba nyiingi tu Kariakoo
lakini wakafa malofa....


inawezekana basi na mzee gurrrr... amechangia ujenzi wa kariakoo ya zamani...
 
Hongera babu Dark City kwa kufuata ushauri wa mkeo kuna wanaume vichomi hawashauriki/ushauri wa mke hauna maana kwao hata kidogo hata ukabe tena ndio unazidi mkimbiza.

Sitanii kabisa Chauro,

Kama kuna mtu hajawahi kuonja utamu wa kumshirikisha mke wake katika kila jambo la maana analotaka kufanya basi aje nimsimulie aina ya utamu ninaoupata....lol!!



Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
huu uzi umenikuna sana, ngoja nitoe my personal story labda naweza inspire vijana wa mujini

Nilipomaliza university nilibahatika kupata deal moja ambayo ilikuwa inanipa pesa nzuri sana, it was way beyong my expectations. i was just 24 yrs old. Sasa bwana nilichanganyikiwaje? yaani nilikuwa nagawa pesa kama njugu, mara nimewanunulia wazazi gari, wadogo zangu ndio usiseme walizifaidi sana pesa zangu, macousin wakija home lazima waondoke na wekundu wa kutosha, nikitoka out na marafiki mi ndio wa kulipa bill na viingilio lol. yaani ili mradi roho yangu ilikuwa nzuri kupita maelezo.

basi kumbe baba yangu mda wote huo ananichora tu. siku moja akaniita akaniambia anashida na kama 5m anaomba nimpatie. mi nikamshangaa maana haikuwa kawaida yake kuomba lakini haikuwa tabu kwangu nikampatia. Mda wote huu pia nilikuwa na ndoto ya kununua nyumba Masaki lol! Basi dingi kila akiniambia kununua kiwanja mi namjibu kuwa nazichanga za kununua nyumba masaki.

ikapita kama miaka 2 ivi, akili ikaanza kunijia huenda sitoweza nunua masaki, maana ilikuwa kila nikiuliza natajiwa malaki ya dollars lol. Basi nikamuomba baba anisaidie kutafuta kiwanja, akasema sawa. siku chache baadae akaniambia haya twende nikakuonyeshe, tukafika mahali akaniambia unakumbuka ile 5m niliyokuomba? ndio...basi nilinunua viwanja 2 na chenji iliyobaki nikanunua trips za kokoto na mawe. yaani sikuamini jamani. yaani zile kokoto na mawe nilijenga na zikabaki, mpaka leo nikiziangalia natoka machozi, maana baba alifariki miezi michache baada ya kunionyesha viwanja. thamani ya viwanja ivyo sasa ivi kama nikiamua kuuza si chini ya 80m kwa kimoja, imagine ukilinganisha na bei nilionunulia. na iyo ni baada ya miaka less than 10

yale mawe nimeamua kuyaacha hapo kama ukumbusho, na pia watoto wangu wakikua ntawambia hii adithi ili nao wawe inspired. nimejifunza kuna baadhi ya investiments ukifanya you can never go wrong, no matter what.


Baba yako alijua angekuambia kwa mdomo usinge muelewa
so alizungumza kwa vitendo...
 
Ok hizo ni kanuni za kiuchumi nazielewa vizuri sana. Mimi msingi wa maswali yangu ni kwamba hata huyo aliepata ufahamu wakielimu akajua how much to consume kulingana na income yake nae kabarikiwa akili hiyo na Mungu.

Jambo hili kama unataka maoni yangu ni HAPANA
Ungesoma maelezo yangu vizuri ungeelewa nilichomaanisha
Mungu kaweka kila kitu ni jukumu la kila mmoja kufanya juhudi kukipata alichokiweka!
Kwakuwa wapo wenye ujuzi huohuo lakini hawautumii kujipatia hayo maisha safi.

Hya ni matatizo yao
Mzee Ngurumo na watu wamfano wake waliobahatika kupata neema kipindi cha ujana wao wakazichezea wao walikosa neema ya ufahamu wa kuwekeza kwa ajili ya maisha ya baadae.
Hapana sema ukweli bana
HAWA WALIFANYA UZEMBE!
Hakuna neema za aina hii!

Nikiwa na maana kwamba umaskini na utajiri pia ni sehemu ya mipango ya Mungu.
Whaaaat?
Hii io kweli hata kidogo
Mungu gani huyu?


Mungu anajua nani atakuwa mzembe ktk utajiri alionao na mwisho ataja kuwa maskini.

Ndigu huyu mungu wa aina hii simjui kabisa!
Kama ni hivi ni kwanini tunafanya kazi?
Sema ni siri yake Mungu kwani hakuna aliezaliwa anajua kuwa yeye atakuwa tajiri au maskini.
Nimekuambia kuwa namna unavyofanya kazi ndivyo unapopata mafanikio,haya unayoniambia sijui umeyatolea wapi!

Huwezi ukakaa tu chini ukawa na fikra kuwa utapata tu kwakuwa Mungu ndie anaejua wewe utakuwa tajiri

bali mtu unapaswa kuhangaika na kujitafutia ila ikitokea umekosa pamoja na juhudi zote ulizoonyesha katika kutafuta unapaswa kuamini kuwa Mungu ndie aliepanga hayo na hapo itakusaidia pia Kumshukuru kwakila jambo la furaha au la shida.

Napata shida sana kukuelewa na kauli zako hizi
Sijui unajua kama unajikinza!

Ndio maana as a human being we do our best and God do himself the rest. Unapokuwa unasema Mungu hajui nani atakuwa maskini au tajiri manake wewe unakuwa mpingaji wa kwamba Mungu hajui mambo ya siri.

Mh! haya nani ameyasema?

Wakati yeye ndio anaejua yaliokuwa, yanayotokea sasa na yatakayotokea kesho tusioijua wewe na mimi. Cc Kibibi Jongo.

Kujua ni kupanga?
 
umenikumbusha wakati mzee kastaafu akafanikiwa kujenga kibanda last minute, kwa mara ya kwanza nikapata kusikia sauti ya mvua kwenye nyumba ya bati ambayo haijawekwa ceiling it was hard, ukizingatia nimezaliwa na kukulia kwenye nyumba za sirikali za vigae.

Anyway kwa watoto wa baba yetu, we took it positive kiasi kwamba hakuna mtoto ambaye alifikisha 30yrs bila kuwa na nyumba, so tulijifunza kutokana na makosa ya mzazi; you can do the same.
thax dia kwa ushauri mzuri. kitu ambacho namshukuru ni kutusomesha ki ukweli pamoja na mapungufu yake hajawahi kuwa mbishi when it comes to school fees, au kitu chochote kinachohusiana na shule. i'm working so hard so that i can get my own propeties.
 
Inatakiwa mchukue hatua za kujenga mapema ili kufidia hilo pengo la mzee wenu. Nasema hivyo kwa sababu, in case lolote likitokea mzee akashindwa kufanya kazi, basi ujue mnatimuliwa within no time kwenye hio kota. Tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa Gurumo na Marehemu mzee Kipara

thax, but I'm the first born na wadogo zangu bado wako secondary, ni ngumu kwa sasa coz mi ndo kwanza nimeanza maisha. ila ntakuja nifanye kitu mambo yakienda vizuri.
 
Hakikisheni mnambana awe na vitega uchumi atakuja kuwasumbua na kuwatia aibu. Wazee wa aina hii huwa wepesi sana kulaumu watoto wao. Jitahidini na mshirikiane ktk kumshauri juu ya future yake ili asiwaaibishe.

nitajitahidi kuongea nae dia japo wakati mwingine anakuwa mkali hadi namuogopa
 
Jambo hili kama unataka maoni yangu ni HAPANA
Ungesoma maelezo yangu vizuri ungeelewa nilichomaanisha
Mungu kaweka kila kitu ni jukumu la kila mmoja kufanya juhudi kukipata alichokiweka!


Hya ni matatizo yao

Hapana sema ukweli bana
HAWA WALIFANYA UZEMBE!
Hakuna neema za aina hii!


Whaaaat?
Hii io kweli hata kidogo
Mungu gani huyu?




Ndigu huyu mungu wa aina hii simjui kabisa!
Kama ni hivi ni kwanini tunafanya kazi?

Nimekuambia kuwa namna unavyofanya kazi ndivyo unapopata mafanikio,haya unayoniambia sijui umeyatolea wapi!





Napata shida sana kukuelewa na kauli zako hizi
Sijui unajua kama unajikinza!



Mh! haya nani ameyasema?



Kujua ni kupanga?

Ngoja tusianzishe mjadala ndani ya mjadala.
 
sisi hatujawahi ishi kota na mimi siishi kwa wazazi Asprin nitake radhi .ila baba yetu alilipwa mafao meengi baada yakustafu hatujui hela alihonga wapi na alianza kazi akiwa na 17 yrs serikalini hahahahaahahah
afadhali nyie angalau you have a place to call it home
 
Back
Top Bottom