Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Jamani tujifunze kusamehe. Hata kama alikukosea bado ni baba tu kuna mengi aliyokufanyia bila hata wewe kujua, ndio maana umekuwa na kufikia hapo ulipo.

Nimeshamsamehe ndiyo maana tunamtunza kwa hali yote, kuanzia mavazi mpk chakula, ila dururu hatumpi zake si kachezea, aende kwa huyo hawara yake na yeye ampe chenji iliyobakia.
 
Nami nimewaza the same, tena nikasema suppose uzi huu (word to word) angekuwa ameuweka lara 1 ni kiasi gani angeshambuliwa na kupingwa na lawama zote zingepewa wanawake (mke to be soecific) kwa kushindwa kumake the home kama ambavyo hili jukumu tulivyotwishwa 100%.

Sidhani kama uko sahihi Kaunga, dunia imebadilika, challenge za maisha ni nyingi, uzuri mmoja unaona kabisa unavyoachwa ama na class/college mate, majirani nk so hakuna anayekubali kuachwa kwa mbali kirahisi...Alichoelezea The Boss tena kwa mfano dhahiri hakina ubishi so ukiona anayepingana na huu ukweli basi atakuwa mwendawazimu..... Hiki kizazi cha kina Gurumo na baba zetu ndio kinaishia na ukiona mwanaume anaishi maisha waliyoishi baba zetu karne hii ndoa inaishia kuvunjika kwani ni wanawake wachache wanaoweza kuvumilia ujinga wa namna hii. So sidhani kama wanaounga mkono wanafanya hivyo kiunafiki. Yawezekana baadhi tukawa bado kwa kiasi fulani hatujitambui kama hawa tunaowasema lakini hii haizuii mtu kusema hiki ni sawa na kile si sawa!
 
Last edited by a moderator:
Kuna Uncle yangu alinipa story, eti miaka ya 70s alipewa kiwanja Upanga akakataa, eti mbali duh! kipindi icho yeye anaishi kariakoo nyumba ya msajili. mpaka kesho nashindwa kumsamehe huyu jamaa. Ni kati ya wazee waliostaafu na kuondoka na mabegi yake kwenye nyumba ya serikali. alikuwa ni mtu mkubwa tu na very influential. watoto wake wanahangaika, elimu pia hakuwapa. wamebaki tu kusimulia baba yetu alikuwa ivi na vile.

Ninachomkubali baba yetu, ni suala la elimu. Vyote alipuuzia lakini elimu yetu hakuisahau; imagine mimi sijui nguo wala viatu nilivyonunuliwa na baba zaidi ya uniform; kweli na kiwanja alininunulia nilikuwa nimesahau.
 
Sidhani kama uko sahihi Kaunga, dunia imebadilika, challenge za maisha ni nyingi, uzuri mmoja unaona kabisa unavyoachwa ama na class/college mate, majirani nk so hakuna anayekubali kuachwa kwa mbali kirahisi...Alichoelezea The Boss tena kwa mfano dhahiri hakina ubishi so ukiona anayepingana na huu ukweli basi atakuwa mwendawazimu..... Hiki kizazi cha kina Gurumo na baba zetu ndio kinaishia na ukiona mwanaume anaishi maisha waliyoishi baba zetu karne hii ndoa inaishia kuvunjika kwani ni wanawake wachache wanaoweza kuvumilia ujinga wa namna hii. So sidhani kama wanaounga mkono wanafanya hivyo kiunafiki. Yawezekana baadhi tukawa bado kwa kiasi fulani hatujitambui kama hawa tunaowasema lakini hii haizuii mtu kusema hiki ni sawa na kile si sawa!

I am so happy to hear this; kumbe sio all is lost. U are right l guess; ugumu na mbio za maisha naona zimekuwa better teacher kwa vijana wa leo. Safi sana Kikwete na sirikali ya waoemu (CCM).
 
Itakuwa alikuwa akipata hela nyumbani wanakula kwa siku moja kuku wa kuchoma, wa mchuzi, wakuhoka, wakukaanga na mwingine mchemsho halafu anamnunulia wife dot 20 za vitenge kutoka Zaire(DR Congo ya sasa), na yeye ananunua mashati 20 ya uju uji na viatu pea 10 halafu kila mwezi kwake kuna shughuli.....hivi unadhani huyo mtu GRAND FINALE yake itakuwaje.
 
Respect mkuu ni kweli mkuu. Hata kma ushawahi sikia story ya jamaa waliitwa Les Wanyika nao walikufa kimaskin lakin waliishi kifalme...
Vijana tujifunze kwa hawa wazee.
 
Ni kweli kabisa "vijana wa zamani" wengi wamezeeka bila kitu. Na wengi wao ni kwa sababu ya ujinga wao (ndio lazima niseme). Walikuwa wanapata kila kitu bure, nyumba, usafiri, furniture mpaka vijiko. Socialism iliwalaza akili. Hii imejenga dhana potofu mpaka kwa vizazi vya sasa kuwa serikali ina jukumu la kutunza watu na familia zao. Kuna wazee waliokuwa na nyadhifa kuu kuu lakini wamestaafu hawana hata kibanda. Halafu wanailaumu serikali. Wengi wa hawa walikuwa busy kustarehe na pombe na uchafu mwingine kila kona wakasahau kuwekeza, halafu they have the audacity kuilaumu serikali. Na wengi huwa wanashindwa kuhimili maisha baada ya retirement, wanakuwa frustrated mpaka wanavuta masikini viumbe wa Mungu. Inabidi tubadilike.
 
Hongera babu Dark City kwa kufuata ushauri wa mkeo kuna wanaume vichomi hawashauriki/ushauri wa mke hauna maana kwao hata kidogo hata ukabe tena ndio unazidi mkimbiza.

Kwenye hili sina ubishi mkubwa mwenzangu....

Mwenzenu hadi sasa, karibia vitu vingi sifanyi bila ruhusa ya bibi....ila wakati mwingine anakaba sana hadi natamani kukimbia nyumba....

Mwanamke wa hovyo ni zaidi ya kiroba cha misumali.....

Ndiyo maana nawakubali na kuwaheshimu akina na mama wenye busara zao, wakiongozwa na Bibi DC, mama yangu mazazi na wengine kibao....!!

Babu DC!!
 
ha haaa, umenichekesha tunapoongea pale nyumbani (mbele ya watoto wetu) kuwa tunajiandalia maisha yetu ya baadae....
Tukiwa tunapanga kitu tunajiambia "unajua tutabaki wawili tu", kwa hiyo tunaandaa kwa ajili ya wawili..... sasa wanatuambia yaani wao tunawatenga?
Babangu (RIP) namkumbuka sana wakati alipokuwa analipa ada za shule na kutuzungumzia kuhusu maisha alikuwa anatuambia tujitahidi ili asije akaendelea kulipa na ada za wajukuu zake. nakumbuka siku mdogo wangu alimkorofisha sana akamwambia unafikiri nakuambia kila siku kuhusu maisha ili uje kunisaidia? sitakuja kutegemea msaada wako baadae maana nina uwezo wa kujitegemea mpaka nakufa, ila sitapenda nikiwa nimezeeka bado nitakiwe kulipa ada za wajukuu ambao wazazi wao hawataki kukazana ili wajikwamue na maisha. Huwa nakumbuka sana hiyo statement yake
Huyo baba nampongeza ni miongoni mwa wazee wachache waliokua na hekima na busara na tena alikua anaona mbali sana. Usipoangalia unaweza somesha na wajukuu , basi hata mimi huwa nawaambia hivi hivi wanangu. Huwa nasema nime- sacrifice kwa ajili yao. Ijapokua wazee wetu muda wao umepita na haiwezekani kurekebisha makosa yao basi sisi wazee wa kesho tuliangalie hili na tufanye kitu ili nasi tusiongelewe namna hii.
 
Kuna Uncle yangu alinipa story, eti miaka ya 70s alipewa kiwanja Upanga akakataa, eti mbali duh! kipindi icho yeye anaishi kariakoo nyumba ya msajili. mpaka kesho nashindwa kumsamehe huyu jamaa. Ni kati ya wazee waliostaafu na kuondoka na mabegi yake kwenye nyumba ya serikali. alikuwa ni mtu mkubwa tu na very influential. watoto wake wanahangaika, elimu pia hakuwapa. wamebaki tu kusimulia baba yetu alikuwa ivi na vile.

We acha tu, unaweza kumrukia vichwa baba yako mzazi.......unashindwa kuelewa ni kwanini mtu hakuweza kununua nyumba kariakoo na beach plot kawe au basi hata bahari beach.......ni ngumu sana kuwaelewa hawa watu. Alalfu anakuja kukusimulia ujinga wao....anakwambia mikocheni ilikua ni madimbi tu hata upewe bure hutaki.
 
Hakuwa mama yetu, ila alikuwa baba yetu, ndiyo alimuacha mama yetu akaenda kuoa baada ya kupata pesa za EAST AFRICA zilipoisha akarudi home, na sisi tunamfanya kama mbwa wa kizungu anapata matumizi yote kasoro pesa.

nilikuelewa my daughter (kifupi cha jina la binti yangu ni Lisa), hapo mie nilichangia tu kuhusu mama, but kwa upande wako nilielewa ulimzungumzia baba.
 
Kuna Uncle yangu alinipa story, eti miaka ya 70s alipewa kiwanja Upanga akakataa, eti mbali duh! kipindi icho yeye anaishi kariakoo nyumba ya msajili. mpaka kesho nashindwa kumsamehe huyu jamaa. Ni kati ya wazee waliostaafu na kuondoka na mabegi yake kwenye nyumba ya serikali. alikuwa ni mtu mkubwa tu na very influential. watoto wake wanahangaika, elimu pia hakuwapa. wamebaki tu kusimulia baba yetu alikuwa ivi na vile.

Aisee.....Yaani Upanga alisema ni porini? Duh! Maisha yanakwenda kasi sana!
 
Hakuwa mama yetu, ila alikuwa baba yetu, ndiyo alimuacha mama yetu akaenda kuoa baada ya kupata pesa za EAST AFRICA zilipoisha akarudi home, na sisi tunamfanya kama mbwa wa kizungu anapata matumizi yote kasoro pesa.

Ila kina mama wakiamua kukushghulikia? Kaazi kweli kweli.
 
The boss kaongea point leo..sijui wanaume wanasapoti kwa kumaanisha au basi tu.sababu ukiangalia,most men wako hivo.hasa hapa mjini dar,panachanganya sana watu.maisha ya kuigana na kuendekeza marafiki wasio na maendeleo..
Unakuta mtu analipwa mshahara wa kawaida tu ila mwanaume anaenda kukata kucha saluni na kusuguliwa miguu,kweli??ilimradi aonekane nae wamo kitaa.hana kiwanja wala maendeleo ya msingi,gari kakopa benki na kutwa wanawake.
Hivi mwanaume kuwa mhuni ni lazima eeh?its like imekuwa desturi mwanaume lazima apitie kipindi cha kuhangaika hovyo na women.wanaita 'phase ya ujana' wasijue hiyo ndo inadetermine uzee.ndomana maryoo wamezidi.janaume lipo lipo tu,akimuona kwenye gari utasema wa maana kumbe mkewe ndo anamuweka mjini.hana mipango,mshahara haileweki unapoishia.
mtu anaendekeza pombe,akitoka kazini lazima apitie bar.ukiwaona humu jf wanajitetea eti mbona mwanaume unakunywa bia na watoto wanaenda shule.we kila siku unaache elf 10 bar,kwa wiki ni elf 70.bado hujafanya tu kitu cha maana nayo?hapo familia yake haijatoka out karibu mwaka.ukidunduliza hizo elf 10 ukaenda vacation hata hapo ufukweni na familia,bado hujajenga kitu kweli??..
Men get serious...

hapo tuuu, hawa wanaume wa kisasa ndipo wanaponimaliza kabisaaaa, nachukia sana hiyo kitu, mie mwenyewe siendi kusafisha miguu saloon ndio aende mwanaume? mwanaume mzima unadhubutu kwenda saloon kukata kucha, nae anavaa pensi ili aweze kuoshwa miguu vizuri hadi magotini, aiseee wenye waume wa hivyo niwape pole kubwa sana, na kama unavyosema hawanaga kitu kabisaaa, mshahara laki 8 sijui una mambo kibao ya anasa, saa ngapi atakumbuka maendeleo/mahitaji ya familia yake? huo mwenyewe haumtoshelezi kutokana na anasa, loo wanawake tuna kazi kweli kweli.
 
Aisee.....Yaani Upanga alisema ni porini? Duh! Maisha yanakwenda kasi sana!

kuna wakati nilimwambia rafiki yangu nataka kwenda kutafuta kiwanja sehemu fulani, akaniambia huko mie siwezi kuishi hata kidogo kwanza nitakuwa natupa hela bure mana siwezi kuishi mbali kote huko, nikamwambia najua sasa hivi una hela nunua tu ukiache coz hata mie mwenyewe sina plan ya kukijenga leo wala kesho, baada ya miaka miwili alienda kununua kiwanja eneo hilo hilo tena chini kabisa na kwangu kwa bei mara 4 na nilivyonunua mie wakati huo, maisha yaharudi nyuma, tuwekeze jamani.
 
Mkuu juzi kwenye mikasi ilikuwa ni marudio tu, alishawahi kuhojiwa katika kipindi cha zilipendwa na Redio one jumapili moja.

Huyo mzee Gurumo pamoja na kukiri kumtungia rafiki yake wimbo wa Kassimu kwa kutapanya pesa kwa anasa lakini na yeye alikuwa mule mule kama rafiki yake Dokta Remmy Ongala (naye kama siyo watoto wake kumpiga tafu angeumbuka)

Matokeo yake wazee wa leo wakiona vijana wanafanya mambo mapema wanaanza kusema eti wameiba mara ooh freemanson na maneno mengi ya kukera.
 
Huwezi kufaidi kila kitu,
Mzee Gurumo wa Msondo Ngoma alifaidi totoz, maisha ya starehe na anasa;
Mwisho amekosa mali, sijui hata kama nyumba anayo na kama ipo ni kibanda tu.
........Wanasema ..........mwache aponde mali ...........
 
The Boss.. Umesema vyema. Lakini najiwazia tu tuwasamehe hawa wazee wetu, coz zamani hizo kulikuwa hakuna changamoto nyingi za kuwafanya wakune sana vichwa vyao kuyapanga maisha ya baadae. Sababu hiyo iliwafanya wajisahau sana.

Ukiacha wasanii angalia wazee wanaostaafu sasa mfano watumishi wa umma..wengi wao (si wote) hakuna lolote walilofanya kuna ambao hata kibanda hawana, anastaafu anarudi mkoa.. hili nimeshuhudia ninapofanyia kazi. Hata sasa hivi wapo baadhi ya vijana wasiowaza kesho itakuwaje, kuna uzi mmoja alipost bibie lara 1 katika business forum.. link yake hii
https://www.jamiiforums.com/busines...-mikoani-ni-didimizo-la-uchumi-binafsi-6.html

Kama unaishi maisha ambayo hayakupi changamoto, mazingira ambayo hauna mtu wa kushindana nae.. haupati hasira za kujiendeleza kiuchumi, kielimu n.k... Mategemeo yatakuwa na yale yale kama ya huyo mzee kuendelea kulalamika, hebu tutumie fursa (source Ruge ..hahaa )tulizonazo kujipanga kimaaisha.
 
Last edited by a moderator:
yaani The Boss umetugusa wengi, babangu anaelekea kustaafu lakini hata nyumba hana. halafu sioni kama hili linamuumiza yaani sie tumekuwa wa kuishi kotta wakati mzee ana uwezo wa kujenga lakini anaendekeza starehe hadi uzeeni. sas sijui atamlaumu nani.

Inatakiwa mchukue hatua za kujenga mapema ili kufidia hilo pengo la mzee wenu. Nasema hivyo kwa sababu, in case lolote likitokea mzee akashindwa kufanya kazi, basi ujue mnatimuliwa within no time kwenye hio kota. Tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa Gurumo na Marehemu mzee Kipara
 
Back
Top Bottom