Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Listening to the elders does'nt mean that they are perfect but we have to listen tothem simply because they have an experience for so many mistake what they did during their teenagers life.so anapaswa kuwa somo kwetu!
 
Gombaneni nae sasa hivi
atawasumbua mno huyo baadae...
atawatolea laana msipompa pesa...hapo baadae
mngeanza kugombana nae sasa
mmh nimeshagombana nae hadi kufikia
kutozungumza sometimes. but haonekani kujali kabisa na anadai kuwa yeye
haitaji nyumba bali akistaafu atarudi tu kijijini kwao na kujenga
kakibanda ka kumtosha. yaani yeye ni pombe na wanawake utasema ndo
anabalehe. ki ukweli nimeanza kumchukia lakini sina jinsi ndo baba
angu.
 
Umenikumbusha!

Leo tulikuwa na mjadala hapa maeneo ya kazi

Kuna jamaa walikuwa wanadai kuna watu "wamepangiwa" kukosa na wengine kupata,nikawauliza kuhusu walipotoa huo mtazamo wao hawakuwa na majibu ya kuridhisha kabisa wakabaki wananiambia tu eti Mungu ndie anaepanga nani apate nini na kwa kiasi gani

Nilichowaambia mimi ni kuwa watu kama hawa ndio wanafanya watu waendelee kuwa maskini hasa watoto wao wanaowalea,wanawafanya wabweteke bila kujibidiisha kikazi na kifikra

Pia wanataka kumfanya Mungu aonekane ni mwenye upendeleo wa kuwapa wengine nyingi na wengine kidogo jambo ambalo sio kweli

Nijuavyo mimi Mungu hapangi nani apate na nani asipate ila ameweka kanuni ambazo kila atakaezifuata na kuzitii na pia kufanya kazi kwa bidii kwa uangalifu na kutumia akili kwa kiwango chake atapata kwa kiwango hicho,haya mambo ya kukaa na kudanganyana eti Mungu hajanipangia kuwa tajiri ni maneno ya kivivu na ni maneno ya kukemewa kwa nguvu zote

Wazee kama hao uliosema hapo wamevuna kwa kiwango chao kama walichezea watakula kuchezea hoko,Mungu sio boi wako wa kufix mistake zako tena nyingi za kijinga unazozifanya kila uchao

Ukiwa mhongaji utavuna uhongaji!!!!!!!

Yaani Eiyer umeeleza vzr haswa! Ni dini Fulani ivi ndiyo inawadumaza watu kutokufanya kazi kwa bidii, wala kutopanga future eti Mungu akipenda ndio utakuwa tajiri!
Dini zingine ni za hovyoo na ni za Shetani mwenyewe manake Mungu si dhalimu wala hana upendeleo.
Kama ulivyosema Mungu ameweka kanuni, na ukizifuata huwezi kubaki maskini!
 
well said. tujifunze kuwekeza ktk maisha y baadae tho ha2jui cku ye2 ya kufa

Hata kama unaijua siku yako ya kufa bado ni muhimu kutochezea opportunities za maisha! Usipotumia wewe, watoto na wajukuu watatumia.
 
Hahaha...
Kuna fursa nyingi mno za kutukomboa kiuchumi huwa tunazipuuzia pengine kwa kutokuwa na uelewa au udumavu wa akili au kutothubutu.
Mathalani Tanzania imejaaliwa ardhi yenye rutuba na yenye kustawisha mazao chungu tele...huu ni mfano mdogo mno wa fursa ambayo sisi Wabongo tunaipuuzia...ni Watanzania wachache mno wenye uelewa au ufahamu wa kilimo chenye tija.

That's right Mkuu! Mfano mdogo nenda Bagamoyo uone ardhi nzuuuri mno! Nashindwa kuelewa umaskini utoke wapi jamani... Umaskini wetu uko kwenye brain mi nakwambieni! Kama akili imedumaa hata upindukeje hata serikali ingekuletea fedha ikakushikisha bado tatizo latabaki pale pale!
 
Wanasema eti Mungu hakuwapangia!!
Hata aibu hawaoni

Ifike mahali tuwajibike kwa makosa yetu!

That's right! Unalala vibarazani, kutwa kwenye vijiwe vya majungu, hata kufuga kuku wawili wa kienyeji wasio nagarama kubwa ya madawa na vyakula unashindwa, hata kuweka bustani ya mchicha uani, kupunguza garama ya fedha ya chakula huwezi!
Unapokuwa na nidhamu na bidii kwa vitu vidogo ndivyo Mungu naye anakupa maarifa ya mambo makubwa!
 
Kwangu mimi hii itakuwa the best thread i have ever read,na si kwasababu inaongelea maisha ya wazee wetu bali kwa jinsi ilivyojaa umakini.
Back to the topic:
Ukiangalia kuna wazee wengi ambao mpaka leo nashindwa kuelewa kwamba nini kilitokea katka maisha yao mpaka mwisho wa siku wanaishia kuadhilika kwa kiasi kibaya,
Kuna wazee wengi ambao nisingependa kutaja majina yao wamekuwa wakiongelewa mara kwa mara kwamba wanahitaji misaada wakati ukiangalia ni watu ambao wamewahi kuwa na majina makubwa hapa nchini na kutambulika hata nje ya mipaka,lakini kwa kukosa umakini wanaishia kudhalilika

Me too Mkuu! Nyingine ni ya jana inayozungumzia wajane na yatima wanavyozulumiwa mali.
Ile ilinibadili bad attitudes towards men, niliona walivokuwa wakitetea haki za wake zao na watoto wao!
 
Hivi siku moja tukipata rais ambae ataroa tamko kuwa baada ya mwaka mmoja kijana yoyote asie na kazi anatakiwa either amepata cha kufanya au kama hana aondoke mjini na kwenda kwenye mashamba na kujikusanya vijana angalau wa 5 na serikali iatawapa eneo na penbejeo kwaajili ya kilimo na itawapa mahitaji yote muhimu kwaajili ya chakula na kilimo kwa muda wote watakaokuwa mashambani

Halafu ikaweka sheria kali ya kwenda mijini hovyo na ni marufuku kuonekana kijana anazurula hovyo bila kazi na baadhi wakakkamatwa na sheria ikachgukua mkondo wake unadhani kutakuwa na asie na kazi?

Unadhani kutakuwa na njaa?

Thubutuuuuuuuuuuuu!!!!!!!!!!!!

Hahahahahaaaa...... I wish uwe president wewe, alaf mimi waziri wa kilimo na mifugo!
 
hiyo ni kweli mkuu sijui wazee hawa wa zamani hawakuwa na ufahamu? mimi naona walikuwa wanapata vitu vingi bure na nafuu so wakajisahau. Nina mfano hai jana tu hapa ofisini kuna mzee mmoja mfanyakazi mwenzangu wao ndo watu wa kwanza kuajiriwa hapa ofisini hiyo ni miaka ya sabini tunakaa njia moja hivi sasa jana kaniona napita zangu kuja job yeye yupo kituoni mm sikumuona sasa akaja ofisini akasema mtani kama nilikuona wewe ukiwa kwenye gari Fulani hivi ila nikajiuliza mbona gari yako ninayoijua sio hiyo? nikamwambia nilikuwa mimi basi akaanza kulalama yani sisi tulichezea maisha mtu ulikuwa unapewa kila kitu bure mwisho wa siku unachukua mwanamke jioni unaenda pumzika nae!! yani kuanzia chakula, bia, usafiri wa kurudishwa home vyote ni bure! sasa anajuta na kusema tazama vijana wa siku hizi mambo yenu yalivyo mazuri sisi tumebaki kuwakodolea macho tu! sasa nashindwa kusema mfumo uliokuwepo ni tatizo au ni akili ya mtu binafsi!
Wazee wa aina hii wapo wengi sana tena wengine walikua bahili hata kusomesha mtoto. Kumbuka kipindi hicho ada ya shule ilikua ndogo sana lkn mtoto ikitokea kafeli walikua hawajisumbui kutafuta njia mbadala ya kumuendeleza mtoto. Inashangaza sana mzee wa miaka 70 kutokua na nyumba , halafu wanalalamikia uongozi wa nyerere wanaudhi sana. Hawakufikiri kuhusu maisha yao ya baadae.
 
But all in all......
maisha ya watu wengi sana yakiharibika huwa tunaonewa sana wamama......
kuna kipindi pia huwa naingiaga huu mkenge, kuwa sisi ndo tunapaswa kushika control ya maisha ya familia zetu.
familia nyingi ambazo mama ana vision ya maendeleo huwa inafika mbali sana..... hata kama huyo mama hana kipato kikubwa.
Kuna watu wengi sana wa karibu nami ambao walikuwa na kipato kikubwa sana lakini wameishia kuwa na maisha mabaya sana sababu wake zao walikuwa hawaangalii sana future ya familia, wao ni kuvaa, kula, kunywa........ ananunua vitu vingine havina hata maana, sababu tu mume ana hela......
lakini pia kuna familia ambazo unaona kabisa hawana uwezo kiviiileeee, lakini mama kila siku anafanya juu chini angalau tu future ya familia iwe nzuri.
Naelewa kabisa kuna wababa ambao hawashauriki, hasa na wake zao. lakini mke ana uwezo wa kujua kabisa kuwa mume anapenda sana kusikiliza ushauri wa nani, anaweza kumtumia huyo mtu.
Kuna familia ambayo tunaichukulia kama wazazi wetu. ni watu wazima saana, wastaafu. lakini huyo mume anatusikiliza sana, kila tunachomshauri. Mke wake akitaka kufanya kitu chochote ambacho anajua mumewe ana uwezo nacho huwa anatuomba sisi tumshauri, ni kweli tukiongea naye tu anatoa hela faster, hata kama mkewe alishambishia saaana.
Huwa najifunza mambo mengi sana kwa kuwa karibu sana na watu wazima, haya maisha siyo kama tunavyoyaona kwa nje, kuna mengi yaliyojificha ndani ya nyumba.
usikute mzee wa watu (huyu tunayemjadili) hakuwa na starehe kihiiivyooooo, je alikuwa na mke mshauri?
Kweli my twin mke aweza kuwa tatizo pia. Umenikumbusha mengi mno nakumbuka mara kadhaa wanawake wamelaumiwa ktk familia nyingi. Hata sasa ukijaribu kuangalia baadhi ya familia kama mama ni weak basi familia hiyo huwa ina shida sina maana wababa wakati wote wanategemea wake zao la hasha kwani kuna wababa strong pia aweza kuwa na mwanamke mwenye matumizi makubwa lkn akambana na kuandaa future vema.
 
Mtu kulipwa elfu tatu mwaka 1978 ni 'milionea sana tu'
leo analia 'hakupata chochote'
Kweli haingii akilini lkn ndio kawaida ya binadamu kupenda kuhamishia lawama kwa mtu mwingine bila kujitazama yeye amechangia kiasi gani hali kuwa hivi. Wazee wengi walikua walevi sana na wapenda starehe , yaani umenigusa sana mkuu na hii post huwa najiuliza hivi kizazi cha wazee wetu walikuaje mbona wengi wanafanana akili. Halafu wazee hawa walikua bahili sana hata kutoa support ktk familia . hebu fikiria Enzi hizo karibu huduma nyingi walikua hawalipii kama huduma za afya zilikua nzuri. Kupeleka mtoto shule pia ilikua free na elimu ilikua bomba, wengine walishindwa hata kununua uniform za watoto kisa ubinafsi. Si umeona mzazi wa mbunge flani anadai mwanae kamtelekeza eti anasema alikua sijui japan kikazi for 10 yrs hivyo hakuweza kumhudumia mwanae . Nilikasirika sana kusikia hivyo nikajiuliza mshahara wake alikua anaufanyia nini.
 
haya yanatokea kwa mtu ambayo yupo very close na mimi.....
babake alikuwa anajulikana mji mzima kwa hela, watoto wake walikuwa wanatembea kwenye magari tu, enzi hizo ambazo umiliki wa baiskeli ulikuwa shida. alibahatika kuwa na mtoto mmoja (nje ya ndoa), ambaye kwa sababu alikataliwa na baba na mama wa kambo basi alijisomesha ili angalau aweze kujikwamua kimaisha.
wale watoto wa ndani walikuwa na starehe tu kiasi kwamba hakuna aliyekumbuka shule.
huwezi amini kwa sasa huyo mtoto aliyekataliwa ndo anahudumia ukoo mzima, kuanzia baba/mama aliyemkataa, watoto wa watoto wao ambao walikataa kwenda shule, na watoto wa mzee ambao bado wanaenda shule......
na sasa mzee sababu anaona mwanaye alishasamehe na kuamua kuhudumia "familia" yake basi ameanza kudai haki yake kama mzazi, anatamka kabisa kuwa nahitaji kiasi hiki kwa mwezi..... bila aibu
Wanaudhi watu wa aina hii. Halafu usipowasaidia walalamishi hawakumbuki kabisaa walikotoka kweli watu husema mla kunde husahau lkn mzoa maganda huwa hasahau.Tena hujisifia kwamba bila mimi usingezaliwa , basi mwenzio nashangaaga sana na kusema kwani usingezaa wewe mtoto huyo si angezaliwa kwingine tena ulimpotezea opportunities nyingi tu. Ifike mahala wazee wa kesho wasiige hii tabia ya wazee wetu .
 
Mkuu The Boss pamoja na hayo inawezekana mzee ngurumo kuna makosa alifanya ambayo yamemfimisha hapo.

Lakini lazima thkubali serikali yetu haijaamua kuwasaidia wasaanii na kazi zao zinaibiwa kila leo.nimesikia wanaweka sticker kwenye kazi zao kupitia tra lakini hii ni njia inayo inufahisha serikali moja kwa moja si msanii.

Bado kuna tatizo kabisa ambalo lina changia umaskini wa wasanii wetu, watu wana burn kazi zao mitaani na hakuna sheria za kuwadhibiti maharamia wa kazi zao.

Na hawa wasanii wetu nao ni tatizo kabisa kwanza hawana umoja kabisa,pili kila leo wanakula futari na rais lakini wanashindwa kushinikiza sheria za kuwabana wezi wa kazi zao. Wana shindwa kumuomba rais kuunda kikosi kazi cha kupambana na wezi wa kazi zao nchi nzima,kinyume na hapo wanaishia kupiga nae picha alaf wanakuja kwenye media kusema tunakufa masikini wakati hawajui kutumia nafasi wazipatazo.
Umeona pia na mataanuzi wanayofanya. Kweli serikali ina sehemu yake lkn hebu tuanze na wao je wana mkakati wowote wa kuutokomeza umasikini. Ukiwaangalia huoni kutwa kushindana kwa starehe na mavazi.
 
yaani The Boss umetugusa wengi, babangu anaelekea kustaafu lakini hata nyumba hana. halafu sioni kama hili linamuumiza yaani sie tumekuwa wa kuishi kotta wakati mzee ana uwezo wa kujenga lakini anaendekeza starehe hadi uzeeni. sas sijui atamlaumu nani.
Hakikisheni mnambana awe na vitega uchumi atakuja kuwasumbua na kuwatia aibu. Wazee wa aina hii huwa wepesi sana kulaumu watoto wao. Jitahidini na mshirikiane ktk kumshauri juu ya future yake ili asiwaaibishe.
 
The Boss
umenikumbusha kitu,ila kwa upande mwingine kidogo!
kuna bibi mmoja hv wa kimanyema maeneo ya magomeni,alikuwa bibi yake na msusi wangu!
huyo bibi matusi yake kwa wasichana wa siku hiz ni kuwa wanafanya umalaya bila faida!
mmweneywe anakwambia ""enzi zetu sisi ukiwa ma.laya m.alaya kweli!
hizi nyumba za magomeni hizi zote ni kutokana na pesa za wanaume!siku hizi mlivyo wajinga mbnafanya u.malaya bila kuwa na akili!mna wanaume weeengi halafu hakuna faida!'"
pia waliosoma riwaya ya MIRADI BUBU YA WAZALENDO ,wanaweza kumkumbuka mhusika bi ntwara na binti yake
scenario hiz mbili zinaelezea kwa uhakika!wanaume wa miaka hiyo pesa zao zilikuwa zinaenda wapi!
 
Last edited by a moderator:
The Boss umenena

Tusisahau kuwa baadhi yao walijivunia darasa la IV la mkoloni...!
 
Wakati wa ujana wangu mimi baba yenu shati shilingi 6 unapata kwahv sasa shilingi 6 hata soda hupati.

=====================
Ukipata Ujumbe wa chuki matusi futa delete kabisa
=====================
 
  • Thanks
Reactions: awp
Back
Top Bottom