DEMBA wazazi wetu wamefanya makosa mengi sana
Na wengi tu ambao hadi leo hatuna mahali pa kupaita nyumbani
Kuna wengine nyumbani ni kwa babu yao
Sasa unaweza kujiuliza iweje babu awe na kwake halafu baba ashindwe?
Kuna mabo mengi sana
Lakini baba na mama ni msingi mkubwa sana wa kuimarisha familia
Wakiparaganyika mazazi aliebaki na watoto ni kazi kubwa kuiimarisha hiyo familia
Wakati mwingine watoto wanakuja kuwa na maisha mabovu na ukiangalia kwa makini chanzo ni wazazi
Kuna rafiki yangu mmoja aliniambia mwaka 2001 kuwa wakati huo alinunua tv na alikuwa na umri wa miaka 24
Katika familia yao ya watoto 7,kwenye familia yao hawakuwahi kuwa na godoro la sponji,yeye ndio alikuwa wa kwanza kulinunua
Unaweza tu kuifikiria hiyo familia ilikuwa inaishi maisha gani wakati baba yao alikuwa ni mfanyakazi serikalini kwa muda mrefu sana!
Inauma sana!