ni swala la kujua tu malengo yako. pamoja na kila kitu unachotaka kujifanyia/kufanyia watu, unatakiwa kujua mwisho wa siku wewe unataka nini.
huwa nawatimuaga ndugu zangu ambao wao na mimi wote wafanyakazi, wao inapofika muda wa kulipa ada ya shule ya mwanaye anakuja kwako kukuambia anaomba msaada hana hela ya ada, hali kadhalika inapofika kulipa kodi ya nyumba.
Huwa najiuliza hiki kitu hakijatokea ghafla, mtu unajua kabisa mwezi fulani nalipa ada/kodi kiasi fulani. Mshahara wako kwa miezi 2 hautoshi kulipa (usiniambie ulikuwa unategemea dili). kwa nini usianze ku-accumulate kidogo kidogo mpaka itakapokamilika? hilo deal likitokea utafanyia kitu kingine.....
Salutu! kuna watu uwaona wenzau kama wajinga vile,wewe msgahara wako wote umeukopea school fee ya watoto unaenda kupiga mizinga, mkopowote jmeenda kununulia viwanja.sikusaidii ng'oo!