WanaJF na MMU.....Karibuni tufunge mwaka 2013!

WanaJF na MMU.....Karibuni tufunge mwaka 2013!

wakati unafikiria nikuandalie nini kwanza hebu kamata hii:busu@jounegwalu
 
enh kwani keeeesi!
kah!
umeshadadiiiiiia!
EEENH BASI NDIO WEWE NI DUME LA HAJA!
kha!
umefurahi sasa!
manake maneno mengi kama unatoa muswada wa kamusi!
ah samahani Eiyer nimesema kwa hasira za kusoma maandishi ya ukweli!lol!

Tatizo lenu mmezoea zile story za kwenye tamthilia na vibishoo tu
Kanaoga mara 6 kwa siku

Sijui huwa wanafanya kazi saa ngapi
Shughuli "takatifu" haviwezi kazi kuja hapa JF na kulalama ohhh hawezi kimoja tu jogoo hawiki

Mkikutana na dume la haja lisiloona haya kujitangazia uanaume wake maneno meengi
Hebu acha kumbwela sana
Ebo!!!!!!!
 
Mbona gia ni nyingi sana na nakuhakikishia huzijui zote na lazima nitafanikiwa tu
We ngoja tu!

Kwahiyo lini sasa?
Acha kuniweka roho juu mtoto wa mwanamke mwenzio!

Hahahaaaa-gear?!? Labda utumie za chopper!

Subiri mpaka mtoto wa Maria na Yosef atakaporudi!
 
Very special for mkuu EMT... Much respect kwako kaka


Yuko wapi lakini?

Nipo Babu. Mihangaiko tuu ya hapa na pale. Sijui nianzie wapi maana niko kote kote. Pia sijui nimtaje nani na nimwache maana huwa nawasoma na ku-interact na watu wengi. Katika mwaka 2013 nimeendelea kujifunza mengi kutoka kwa WanaJF hasa kwenye threads/posts zao za kujifunza, kuhabarisha, kufurahisha na pia za kuhusunisha sana. Hivyo kujaribu kuwataja wote will be like fighting a loosing battle.

Hata hivyo, niwapongeze waendeshaji wa JF kwa kuendelea kuboresha jukwaa hili hasa katika kipindi hiki ambacho JF imepanuka kwa kuwa na members ambao siyo wapya tuu bali pia walio na mawazo tofauti. Niwapongeze moderators kwa kazi yao ngumu ya ku-moderate JF. Japokuwa baadhi yetu huwa tunawanaga kwenye posts zetu, we still value your your work. Ni vigumu sana ku-moderate social media ambayo information ina-flow horizontally.

Lakini pia nichukue nafasi hii kuwashukuru baadhi ya WanaJF ambao wameni-trust kiasi cha kuniomba ushauri katika masuala yao binafsi bila kuwashirikisha Members wengine au kwa kuwashirikisha Members wachache sana. I know we go through through life by putting our trust on others, lakini inapofikia mpaka mtu ambaye hakujui na humjui nje ya JF kuku-trust na kukuomba ushauri kwenye masuala yake binafsi huna budi ku-appeaciate na kushukuru. So, I thank all those JF Members who have put trust on me. For confidentiality reasons, sitawataja hapa.

Pamoja na faida binafsi ambazo tunazipata hapa MMU, nadhani kama wapenzi wa jukwaa hili bado tuna changamato kubwa. Tuna changamoto ya kuwakubali members wapya ambao wana mawazo tofauti na tuliyoyazoea huko nyuma. Tusiwanage sana bali tukubali kuwa JF inaelekea kwenye hatua nyingine. JF is no longer a club for certain type of people. JF inaanza ku-reflect maisha ya Watanzania kupitia kwenye michango ya members wake.

Lakini changamoto kubwa ambayo naiona mbele yetu ni jinsi ya kulifanya jukwaa hili kuwa na impact siyo tuu kwetu sisi individually kama JF Members, bali pia kwa jamii yetu nzima kwa ujumla. Mahusiano, mapenzi na urafiki ni mambo muhimu siyo tuu kwa mtu mmoja mmoja bali pia kwa jamii nzima. Kama kuna mahusiano, mapenzi na urafiki ndani ya jamii, basi jamii hiyo itachanua na kusaidia nyanja nyingine kuchanua pia.

If a person cannot live without love, then the society cannot also live without love. Tunajitaji mahusiano, mapenzi na urafiki kwenye jamii yetu. Lakini jamii yetu kwa sasa inaelekea kuendekeza ubinafsi kwa kutothamini maisha ya watu wengine. Ubinadamu unapungua kwa kasi kubwa sana kwenye jamii yetu.

Tumesoma na wengine tumeona yaliyotokea Mwanza. Kama alivyosema Chakaza kwenye uzi wake, "Marehemu ameuwawa katika eneo lake la uongozi ambalo mwaka 2010 alitajwa kuwa alishinda kwa kishindo na amekuwa mwakilishi wao katika baraza la madiwani la wilaya ya Magu toka wakati huo. Hii ni kuonyesha kuwa Raia hao alikuwa nao siku zote, wanamfahamu kama kiongozi wao, shida zao za kila siku wanampelekea yeye kama Diwani na mahusiano yapo ya kila mara kati yake na viongozi wa vitongoji vya kata hiyo ya Kisesa" lakini bado wakaamua kumwua. Wengi wamelichukulia hili suala kama ni la kisiasa, lakini linaweza pia kuwa suala la kijamii aka kukosekana kwa mahusiano, mapenzi na urafiki baina ya wahusika.

Jamii imefanya baadhi ya watu waamini kuwa wanaweza kuishi bila mahusiano, mapenzi na urafiki na ku-thrive. Watoto ambao hawatunzwi na kupendwa huwa wanafariki kutokana na kitu kinachoitwa "failure to thrive". Wale ambao wanafanikiwa kuishi kwenye jamii isiyokuwa na mahusiano, mapenzi na urafiki wanashia kuwa anti-social (kutokuwa na mahusiano, mapenzi na utafiki), wanakata tamaa na wanashindwa kuzalisha. Matokeo yake ni kuwa na jamii iliyo na wazalishaji wachache sana.

Hakuna jamii au mtu binafsi anaweza kushamiri bila kuwa na mahusiano, mapenzi na urafiki. Hivyo basi, wakati MMU ikitusaidia kuboresha mahusiano, mapenzi na urafiki baina yetu kama WanaJF, pia tutathmini jinsi MMU itakavyoweza kuimarisha na kuboresha masuala hayo nyeti kwenye jamii yetu kwa ujumla.
 
Santee bby

Mwaah ya shavu la kushoto na kulia:smile-big:


Huyu lazima keshapita chalinze aisee.... Ila hayo majina mengine Bwana, ....ni sumu kama kumwanga chumvi kwenye barafu.

Babu DC!!
 
Jf' ni jukwaa la kipekee sana binafsi najivunia kuwepo hapa. Jamiiforum imenipa marafiki na imenikutanisha na ndugu na jamaa zangu kutoka pande mbalimbali za dunia hii. Jamiiforum ni mahala ambapo watu huwa tunapishana na kukubaliana kimawazo(agree to disagree) lakini ni matumaini yangu haitupelekei kuwa maadui. Nichukue nafasi hii kuwashukuru brothers ambao nimekutana nao humu ndani lakini ukweli tumekuwa zaidi ya ndugu hata nje ya jukwaa hili(jf). Kwanza nikushukuru brother Ritz wewe niwa kipekee sana na ninajivunia kujuana na wewe, Boko haram, THE BIG SHOW, mzee wangu Mohamed Said nakushukuru sana kwa ushauri na mawazo yako unayonipatia kiukweli ninafarijika sana, brother dr kahtaan, ndugu yangu gombesugu, Mohamedi Mtoi, Elli, Zumbe Mkuu, MANI, ZeMarcopolo, Madame B, Mamndenyi, mkuu wangu chama, dada AshaDii, Nguruvi3, Wickama, best yangu Shardcole et al. Nimejifunza kutoka kwenu na nawatakia kila heri.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom