Wanafunzi wa vyuo vikuu vya Sudan wahamishiwa vyuo vikuu vya Tanzania. Hongera kwa Serikali ya Tanzania

Avantar 2

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
524
526
Hongera kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Hasa Rais wetu mpendwa kwa kupokea Wanafunzi wa Udaktari toka nchini Sudan.

Ikumbukwe nchi ya Sudan ipo katika vita vya wenyewe kwa wenyenye. Mungu akawape utulivu, wepesi na waendelee vema na masomo yao katika Chuo cha Kikuu cha tiba Muhimbili.

---
Wanafunzi 150 wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na Teknolojia (UMST) cha Khartoum nchini Sudan wamehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kukamilisha mwaka wao wa mwisho wa masomo.

Akiongea wakati wa kuwakaribisha wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa hali ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini Sudani imesababisha kufungwa kwa Vyuo na baadhi ya shughuli kusimama hivyo Wataalamu hao kushindwa kuendelea na ratiba yao ya masomo ya kawaida.

“Wanafunzi hawa wapo mwaka wa tano wa shahada ya kwanza ya utabibu, ambapo katika mwaka huo, mafunzo hufanyika kwa vitendo zaidi, hivyo Madaktari hawa Wanafujzi watafanya mzunguko (Rotation) katika idara mbalimbali ikiwemo idara ya upasuaji chini ya usimamizi wa Madaktari bingwa ili kuhakikisha wanapata maarifa yanayotakiwa”

Amesema kuwa MNH itatoa fursa kwa Wataalamu hao kujifunza kama ambavyo inatoa kwa Wataalamu wengine wa ndani na nje ya Nchi na hata baada ya kumaliza masomo kama watapenda kufanya mafunzo tarajali (Intenship) MNH itawapa nafasi hiyo.

Kwa upande wake Ruba Anwar Salih ambaye ni Kiongozi wa kundi la Wanafunzi hao amesema kuwa wamefurahi kupata fursa ya kuendelea na masomo katika Hospitali kubwa na yenye wataalamu wa kutosha, ni imani yao kwamba watapata fursa nzuri ya kujifunza.

s1.jpg
s2.png
s3.jpg


Pia soma: Rwanda yapokea wanafunzi wa udaktari kutoka Sudan
 
IMG_7660.jpeg


Wanafunzi 150 wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na Teknolojia (UMST) cha Khartoum nchini Sudan wamehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kukamilisha mwaka wao wa mwisho wa masomo.

Akiongea wakati wa kuwakaribisha wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa hali ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini Sudani imesababisha kufungwa kwa Vyuo na baadhi ya shughuli kusimama hivyo Wataalamu hao kushindwa kuendelea na ratiba yao ya masomo ya kawaida.

“Wanafunzi hawa wapo mwaka wa tano wa shahada ya kwanza ya utabibu, ambapo katika mwaka huo, mafunzo hufanyika kwa vitendo zaidi, hivyo Madaktari hawa Wanafujzi watafanya mzunguko (Rotation) katika idara mbalimbali ikiwemo idara ya upasuaji chini ya usimamizi wa Madaktari bingwa ili kuhakikisha wanapata maarifa yanayotakiwa”

Amesema kuwa MNH itatoa fursa kwa Wataalamu hao kujifunza kama ambavyo inatoa kwa Wataalamu wengine wa ndani na nje ya Nchi na hata baada ya kumaliza masomo kama watapenda kufanya mafunzo tarajali (Intenship) MNH itawapa nafasi hiyo.

Kwa upande wake Ruba Anwar Salih ambaye ni Kiongozi wa kundi la Wanafunzi hao amesema kuwa wamefurahi kupata fursa ya kuendelea na masomo katika Hospitali kubwa na yenye wataalamu wa kutosha, ni imani yao kwamba watapata fursa nzuri ya kujifunza.
 
Kundi la wengine 500 litarajia kuingia nchini muda sio mrefu, kati Yao wasichana ni 300 na wavulana 200, msije kusema nimewabania taarifa muhimu
===
Wanafunzi 150 wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na Teknolojia (UMST) cha Khartoum nchini Sudan wamehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kukamilisha mwaka wao wa mwisho wa masomo.

Akiongea wakati wa kuwakaribisha wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa hali ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini Sudani imesababisha kufungwa kwa Vyuo na baadhi ya shughuli kusimama hivyo Wataalamu hao kushindwa kuendelea na ratiba yao ya masomo ya kawaida.

“Wanafunzi hawa wapo mwaka wa tano wa shahada ya kwanza ya utabibu, ambapo katika mwaka huo, mafunzo hufanyika kwa vitendo zaidi, hivyo Madaktari hawa Wanafujzi watafanya mzunguko (Rotation) katika idara mbalimbali ikiwemo idara ya upasuaji chini ya usimamizi wa Madaktari bingwa ili kuhakikisha wanapata maarifa yanayotakiwa”

Amesema kuwa MNH itatoa fursa kwa Wataalamu hao kujifunza kama ambavyo inatoa kwa Wataalamu wengine wa ndani na nje ya Nchi na hata baada ya kumaliza masomo kama watapenda kufanya mafunzo tarajali (Intenship) MNH itawapa nafasi hiyo.

Kwa upande wake Ruba Anwar Salih ambaye ni Kiongozi wa kundi la Wanafunzi hao amesema kuwa wamefurahi kupata fursa ya kuendelea na masomo katika Hospitali kubwa na yenye wataalamu wa kutosha, ni imani yao kwamba watapata fursa nzuri ya kujifunza.

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Waswahili mna shida sana, kwa hiyo akiamia UD akaacha Oxford, UD inakuwa bora?

Kwa nini sababu isiwe elimu ni mbaya, bei ipo chini ndo maana wameamia Tanzania?
 
Waswahili mna shida sana, kwa hiyo akiamia UD akaacha Oxford, UD inakuwa bora?

Kwa nini sababu isiwe elimu ni mbaya, bei ipo chini ndo maana wameamia Tanzania?
Wacha ubishi wa kitoto, msikilize huyo makamu mkuu wa chuo Cha Sudan vigezo alivyotumia kuichagua Tanzania katika nchi zote za Afrika.

Mkuu, katika ukanda huu, hakuna nchi yenye elimu Bora ya Afya(Medical education), kuizidi Tanzania, South Afrika tu ndio wanazidi Medical schools za Tanzania.

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom