Madhara ya Vyuo Vikuu Kufundisha CERTIFICATE na DIPLOMA kwa Wanafunzi

Mwinyimadi

New Member
Aug 13, 2022
3
0
Habari ndugu wana JF,

Leo nimependa kuzungumza nanyi mada kuhusu vyuo vikuu kufundisha ASTASHADA na STASHAHADA. ni ukweli usiopingika sera ya elimu inabidi kufanyiwa marekebisho kwasababu vyuo vikuu siku hizi zinachukua watoto wanaomaliza kidato cha nne (4) wengi wao chini ya miaka ya 18 ambapo tunachukulia kama watu wazima kinyume na sheria ya nchi kwani vyuo vikuu vyote vinasema ni elimu ya watu wazima kwahiyo wanafunzi hawa wa Astashahada (Certificate) na Stashahada (Diploma) wanakuwa wahanga kubwa wa unyanyasi wa kingono na ukatili wa kijinsia kwasababu anakuja pahala ambapo hakuna mchunga yaani ana kuwa huru kufanya lolote lile atakalo kwa uhuru.

Kwa kipindi nilichofanya kazi moja ya chuo kikuu nchini nimeweza kugundua wanafunzi hawa ndio wamekuwa swala wa vyuo na ndio waathirika wakubwa wa ukatili wa kingono, unyanyasi wa kijinsia na mimba za utotoni.

Ninatoa wito kwa wadau wa elimu kuangalia upya sheria zetu vizuri kwasababu watoto hawa wamekuwa wakibadilika kimaadili kwa muda mfupi mwishoe wanaingia katika uraibu.

Hivyo rai yangu vyuo vikuu vibadilishe mtazamo wake au viache kufundisha non- degree kwa mustakabali mpana wa vizazi.
 
Hilo ni swala la kimaadili, halihusiani na taaluma.
Hakuna taaluma pasi na maadili ndio maana utasikia umekiuka maadli ya taaluma yako. Imagine binti yako anarudi nyumbani kwa kupewa ujauzito na mwalimu wake je kama mzazi utajisikiaje? Kwanza kusema maadili na taaluma haviendani kusingekuwa na dressing Code kwa wanafunzina na watumishi wa umma, leo serikali imeleta social workers vyuoni kwaajili ya kusaidia wanafunzi kutotumbukia katika mmomonyoko wa maadil
 
Hoja ni nzuri lakini unachozungumzia kina ukakasi kidogo.
Tafiti zipi umefanya zinaonyesha Unyanyasaji wa kijinsia unasababishwa na watu wa degree kuliko non-degree huko vyuoni kwasababu wapo watu wanachukua certificate na diploma ( Non-degree) wamekuzidi umri hata wewe .

Kwahio tutegemee wapo watu wa certificate na diploma wanawanyanyasa watu wa degree vizuri tu alafu tukiachana na umri Unyanyasaji wa kijinsia unasababishwa na vitu vingi kama vile pesa,elimu,tamaduni au malezi, imani na nk kitu ambacho hatuwezi sema sababu zote hizo zinawaangukia tu watu wa Degree pekee

Basi phd au masters nao tuwatenganishe na degree kwasababu sababu zitakua ni hizo hizo

Ingawaje wengi wanaochukua diploma na certificate wanakua na umri mdogo ila elewa si wote amini nakuambia wapo waliokuzidi umri tena wengi tu

Hoja yako iwe tu na misingi ya kutoa elimu kwa watu wote hasa wanafunzi wa mashuleni na vyuoni tu wala kusiwe na matabaka

Lengo la vyuo vikuu kuwa na certificate, diploma, degree, masters na Phd ni kubwa kitaaluma kwa wanafunzi lakini ni kweli
mfumo wa elimu kwenye vyuo vyote kutozingatia umri wa wanafunzi unaweza kuchangia Unyanyasaji wa kijinsia

Ila wazo lako lipo kuleta matabaka na hii inaweza kuleta athari kwenye taaluma na elewa tu wanafunzi wa level zote chuo wakisoma pamoja kuna faida na hasara zake ingawaje hasara Zinaonekana ni chache kuliko faida labda uje na tafiti zako.
 
Hoja ni nzuri lakini unachozungumzia kina ukakasi kidogo.
Tafiti zipi umefanya zinaonyesha Unyanyasaji wa kijinsia unasababishwa na watu wa degree kuliko non-degree huko vyuoni kwasababu wapo watu wanachukua certificate na diploma ( Non-degree) wamekuzidi umri hata wewe .

Kwahio tutegemee wapo watu wa certificate na diploma wanawanyanyasa watu wa degree vizuri tu alafu tukiachana na umri Unyanyasaji wa kijinsia unasababishwa na vitu vingi kama vile pesa,elimu,tamaduni au malezi, imani na nk kitu ambacho hatuwezi sema sababu zote hizo zinawaangukia tu watu wa Degree pekee

Basi phd au masters nao tuwatenganishe na degree kwasababu sababu zitakua ni hizo hizo

Ingawaje wengi wanaochukua diploma na certificate wanakua na umri mdogo ila elewa si wote amini nakuambia wapo waliokuzidi umri tena wengi tu

Hoja yako iwe tu na misingi ya kutoa elimu kwa watu wote hasa wanafunzi wa mashuleni na vyuoni tu wala kusiwe na matabaka

Lengo la vyuo vikuu kuwa na certificate, diploma, degree, masters na Phd ni kubwa kitaaluma kwa wanafunzi lakini ni kweli
mfumo wa elimu kwenye vyuo vyote kutozingatia umri wa wanafunzi unaweza kuchangia Unyanyasaji wa kijinsia

Ila wazo lako lipo kuleta matabaka na hii inaweza kuleta athari kwenye taaluma na elewa tu wanafunzi wa level zote chuo wakisoma pamoja kuna faida na hasara zake ingawaje hasara Zinaonekana ni chache kuliko faida labda uje na tafiti zako.
Nimekuelewa vizuri sana,,, sijaona kosa langu coz ukisoma uzi wangu nimesemema wengi wao na sijasema kwamba wote ni watoto.
 
Back
Top Bottom