Wana CCM naomba mhalalishe picha hizi

Wana CCM naomba mhalalishe picha hizi

This is not fair. Sasa hawa akina mama wamekosa nini hata uwaporomoshee matusi kiasi hiki? Inabidi uombe radhi kwa ufedhuli huu. Honestly...

Kuna hawa wanatimua vumbi....

ccm.jpg


Source: Mjengwa.Blogspot.com
 
Hao wakina mama wanafiki wakubwa......
Tatizo lao ni elimu na kujitambua kuliko umasikini....
Mbona kwa waganga wa kienyeji wananunua mbuzi na kuku wanapeleka???
Au ni imani kuwa hospitali ni bure na ni kazi ya serikali.....

Bottom line ni kuwa sio wote wanaoenda hospitali za serikali
ni maskini kupita kiasi......
Ni mazoea tu.........

Halafu hao akina mama..
Hizo mimba walizipataje????
Hao wanaume waliowapa hizo mimba
hawana kazi kabisa??????
Walihongwa nini kabla ya kufungua miguu
yao kwa hiyari????
Mbona hizo khanga wanazovaa ni mpya mpya
na bei ya khanga moja sasa ni sh 5000/??????

Serikali ina mambo mengi ya kulaumiwa but sio
hao ya akina mama wa mjini......

Nitailaumu serikali kwa huduma za afya vijijini.
But hoa wa mwananyamala na amana na temeke.
Hell no.
Kwani lazima kuishi mjini na kuzaa kama uwezo huna???????

Umeelewa mada inayozungumziwa hapa au umeamua kuvumbua mada yako mwenyewe? Chunga unachoandika jamani, ni aibu kubwa kama mtu mzima kabisa unaweza kuandika mambo kama haya kwenye forum hii.
 
Umeelewa mada inayozungumziwa hapa au umeamua kuvumbua mada yako mwenyewe? Chunga unachoandika jamani, ni aibu kubwa kama mtu mzima kabisa unaweza kuandika mambo kama haya kwenye forum hii.

Naelewa kauli za "The Boss" hazijawafurahisha wengi,hata hivyo kuna la kujifunza....Napendekeza wazo la filamu kuwaonyesha wakina mama hao jinsi walivyo "Hamnazo"

Hopefully mtajiuliza baadhi ya maswali magumu kama vile "Utamaduni wa Kanga" achilia mbali kanda2 na t-shirst kutumika kama "Hongo" kwakina mama hao nyakati za chaguzi mbali mbali.

Halafu kuna watu wanauliza eti kwanini wengine wanaingia kwenye siasa?Hata kama siasa ingekuwa "Msitu" kwa mtaji huu wataingia wengi tu.
 
Natundika haya kwa haraka; nachelewa, mwaka umeanza!
Mimi si mwana-uchumi wala sina haja ya kuleta hapa mahubiri ya dini ya dini za kigeni (kama u-Kristu au u-Islamu).
Lakini hiki kitabu cha Biblia huwa napenda sana kukisoma soma; hususani, Agano Jipya lenye methali nyingi za Yesu (the Christ).
Yesu (the Christ) alitumia methali hizi kuwafundisha watu kuelewa kwa urahisi mambo ya uhusiano baina ya ufalme wa dhambi hapa duniani (transient or temporal mundane sinful space) na ufalme wa milele mbinguni (anticipatory and permanent divine space).
Nasema mimi si mwana-uchumi kwa sababu moja kubwa. Sielewi kabisa uchumi wenye kujali bidhaa (goods) na huduma (services) zipitazo sokoni (market place) “to be aped and relevantly applied to satiate or answer” hali ya Tanzania!
Naelewa sana kwamba sisi wa-Afrika wengi bado ni wale ambao bidhaa (goods) na huduma (services) zetu hazipiti sokoni; “zinaliwa” au zinatumia moja kwa moja.
Kwa mfano, wa Tanzania wengi ni wazalishaji na walaji hapo hapo (producers and consumers) au kwa masamiati mpya ni “prosumers”, ambao nitawaita “wazalishalaji” (wakulima, wavuvi, wafugaji, waokotaji mwituni , na kadhalika).
Sioni kabisa uhai (functional utility) wa uchumi ambao haulingani na mazingira ya binadamu wake uhubiriwe!
Lakini kuna wasomi, kama Profesa Benno Ndulu, ambao wameyasomea mambo hayo ya uchumi. Sasa Prof. Ndulu amekuja na Kozi Mpya ya Uchumi: 101 - Faida (Profit) Itokanayo na Mtaji (Capital) Sio ya Mwenye Mtaji.
Anatufundisha kutaka tuelewe, na wengine akina sisi tumesema kamwe hatutafundishika (never to be educatable) kuamini kwamba faida (profit) hiyo ni mali ya watumishi; sio ya mwekeaji au mlimbikizaji!
Turudi nyuma kidogo. Mwaka jana (mwanzoni mwa kudorora kwa hali ya uchumi kulikoletelezwa na kuanguka kwa benki za mikopo ya majumba na Bima hapa Amerika, na kuambukiza Ulaya Magharibi na ulimwengu wote) alituhakikishia kuwauchumi wa Tanzania hauwezi kuyumba kwa sababu Tanzania ilikuwa imewekeza pesa zake, sijui, “bonds” katika ma-benki ya nchi ambazo uchumi wake haungeweza kudorora!
Hii ikawa ni danganya toto!
Mwishoni mwa mwaka jana (juzi tu) Prof. Ndulu alikuja na hilo la kozi yake mpya.
Turudi kwa methali ya Yesu (the Christ) ya tajiri (Tanzania) na watumishi (BoT) na talanta. Tajiri aliwagawia watumishi wake watatu; wa kwanza talanta tano, wa pili talanta tatu, na wa mwisho talanta moja. Sio kuwa alikuwa akibagua au akipendelea. Lakini sababu tosheleza (significance and rationale) ya kugawa hizvyo ilikuwa ni kutokana na uwezo wa kila mmoja.
Labda, Yesu (the Christ) angekuwepo ki-mwili hapa Tanzania ya leo, na angefundisha juu ya kuwajibikia pesa za umma kwa kutoa mfano huu:
"Ni sawa na mtu mmoja tajiri aliyetaka kusafiri ng`ambo. Aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake. Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja; kisha akasafiri.

"BoT ikapewa talanta tatu. Ikafanya kazi nazo ikapata faida kubwa. Sasa Tanzania inataka kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.

" BoT inakuja amechukua zile talanta tatu na faida yake juu. Inaiambia Tanzania, ulinikabidhi talanta tatu. Hapa pana talanta zako tatu na talanta nyingine mbili zaidi kibindoni faida niliyopata. Hizi talata tatu ni ulizonikabidhi. Chukua hizi zako. Za zaidi talanta mbili kibindoni ni mali yetu sisi watumishi wa BoT.”
Gavana Benno Ndulu alinukuliwa na gazeti moja akitamka kuwa pesa hizo "si za serikalini bali zinatokana na operesheni mbalimbali za benki hiyo ikiwa ni pamoja na riba inayotokana na mikopo mbalimbali wanayoitoa kwa serikali na kwa mabenki mengine nchini.”
Ndio! Hiki ndicho kitovu cha sababu ya Gavana Benno Ndulu kutamka wazi kuhusu chanzo cha pesa hizo za mikopo wafanyakazi wa BoT kujijengea majumba.
Na sio hiyo tu; ni kitovu cha sababu ya viongozi hao wa BoT kujijengea majumba ya fahari yasiyolingana na hali ya mazingira hapoJijini Dar es Salaam!
Gharama ya sakafu ya mawe nje ya majumba hayo inatosha kabisa kujenga zahanati mbili!
Sakafu ya mawe nje hailingani na hali ya mazingira hapoJijini Dar es Salaam yenye joto! Inaongeza joto wakati wa jua kali badala ya nyasi! Walanyumba hiyo haitumii umeme wa jua au upepo!
Badala ya Gavana Ndulu kuiambia Tanzania kuwa faida ni yako na Tanzania kusema, "Vema, mtumishi mwema na mwaminifu,” Gavana Ndulu anadai kuwa kuwa pesa za kuwakopesha watumishi wa BoT SIO PESA ZA SERIKALI!

BoT wanaiba FAIDA! Kwani faida hiyo ilitokana na pesa za nani!

Kama hizo pesa za faida SIO PESA ZA SERIKALI, sa si za serikali, je, tuna uhakika gani wa kujua ni mapesa mangapi ya faida yalliyokwishaKUIBIWA, na, pengine, kuhamishiwa nchi za nje?

Badala ya Tanzania kusema kwa niaba ya walalahoi, “Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha; nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.”

  • Wananchi wangu walikuwa na njaa, mkanisaidia kuleta matrekta ili kuondoa jembe la mkono wanachi wangu wa vijijini waongeze uzalishaji wa mazao ya chakula na kupambana na njaa.
  • Wananchi wangu vijijini hawakuwa na maji safi na y a kutosha, mkanisaidia kuwajengea visima vya maji.
3. Wananchi wangu hawakuwa na nyumba nzuri, mkanisaidia kuwajengea nyumba bora.
4. Wananchi wangu walikuwa uchi, mkanisaidia kuwavika.
5. Wananchi wangu walikuwa wagonjwa bila aspirini kwenye zahanati zao mkanisaidia kuwanunulia dawa ili wapambane na maradhi.
  1. Wakina mama walikuwa katika gereza la kutokujua kusoma na kuandika, mkanisaidia kuwaelemisha ili wapambane naujinga.
  2. Wakina mama walikuwa wakijifungua, kama nyumbumwitu wangu wa Serengeti, mkanisaidia kuwapatia huduma za kusadia kujifungua.
  3. Watoto wangu hawakuwa na shule na madawati, mkanisaidia kuwajengea shule.
  4. Na zaidi na zaidi yenye kuwakomboa walalahoi wangu!

Tanzania itamke, kupitia kwa JK, “Nawaambieni kweli, ninyi watumishi wa BoT, kila mnapokataa kumtendea mambo haya mmojawapo ya hawa walalahoi, mnalisaliti taifa letu!

Halafu JK achukue madaraka mikononi; tulimkupa uwezo huo, na awafukuze watumishi wote wa BoT!



“ Inncidentally”, hayo ya Benno na mgao wa faida ya umma hayakuanza wakati wa Benno Ndulu, yaliwahi kutokea miaka ya kuanzia (kama sikukosea) muongo wa 1970s wakati wa Edwin Mtei.

Wakati huo, BoT walitaka kugawana sehemu ya faida kwa kujipa marupurupu (gratuities) kila mfanyakazi shilingi 1000! Shilingi 1000/- za wakati huo zilikuwa ni kiasi kikubwa (masai kumi)!

BoT ilikunja mkia baada ya Mwalimu Nyerere kuingilia kati, na kung’aka:

“Yaani wanataka kugawana faida ya umma! Pesa za faida kwa BoT ni pesa za umma! Na kujigawia hizo pesa ni kuliibia taifa.”

 
Ndiyo. Ilani yetu ya uchaguzi imezingatiwa. Tuliiuza kwa wananchi wakaikubali. Tuna tekeleza tulichowaahidi wananchi
 
kijibanda cha governor

16badyu.jpg

xqhop2.jpg


wodi ya Kisasa ya kina mama waliojifungua wakiwa wanapumzika pale Hospitali ya Temeke. Ni hali ndiyo ilimfanya mwanamapambo Naomi Campbell..
Temeke+Hostital


Temeke+Hospital+2




article-0-0733CA59000005DC-875_468x686.jpg



Madarasa ya shule za msingi yaliyoboreshwa
shulembuyuuuuu.jpg




Madarasa ya Sekondari yaliyoboreshwa



WANAFUNZI12.jpg
 
Matatizo yoote tunayoyapata ni ya kujitakia; tunakumbatia wala rushwa na selfish pipo wasio na hata chembe ya interest na Tanzania wala watanzania wenyewe!!!

Wengi wetu tukipata kazi, cha kwanza kufikiri ni mali, badala ya service kwa wanaotutegemea, hii ni culture tumei-embrace na sasa inatutafuna vilivyo!!! Sishangai kuona Ndulu anakuwa very happy na kutetea upuuzi wa kuishi kwenye jumba hilo na kuendesha SUV la nguvu wakati watu wake wanasombwa na mafuriko!!! at least basi lingekuwa private house, maana tayari ana majumba yake na sijui atayafanyia nini??

Picha hizi zitakuwa endorsed na mzee makamba na kutetea zile rach walizogawana na viunga vya madini walivyowekeza kwa wazungu na kudai wazungu ndio wawekezaji

Kule simanjiro kuna watoto zaidi ya 200 wana walimu wawili na darasa moja, huku Dar kuna nyumba kubwa ya serikali ingeweza kutengeza madarasa 50 lakini anakaa babu, bibi, na vijukuu vichache plus mbwa, paka na swimming pool
 
mwanakijiji,

gavana anastahili alale kwenye kitanda cha sufi, na mashuka ya silk, paa lake na nyumba yake inapaswa inukie kama keki na kalamati, huku maji yanatiririka kama maporomoko ya pangani na nuru ndani ya nyumba yake ni kama vile jua limehamia ndani ya nyumba yake na kuipatia nishati!

Gavana ana umuhimu sana kwa maana asipopata malezi haya bora, je unafikiri ni nani atakaa na kutafakari mbinu mpya za kiuchumi kwa taifa letu? Unafikiri hawa kina mama na watoto wao wana uwezo hata wa kuelewa jinsi kalamu ya risasi inavyofanya kazi au utamu wa kulalia mashuka ya hariri?

You are damn right kuwa ccm ina kipaumbele naye ni ni gavana!

bora mwehu-kichaa kuwa rais wa nchi. Maana asingekubali ujinga na upumbavu huu
 
Ccm oyeeeeee.
Maisha bora kwa kila mtanzania,
naomi campbell anauza tu sura na kupiga picha za kutengeneza kwenye photoshop akijidai ni tanzania
 
akiamungu mwanakijiji laana'kaka ufai unatisha
hii serikali inabidi ikupe hata cheti maalum
mmmhh
 
Wacha hilo tu m'kijiji
nimesikia juzi mawaziri wake mapumbavu wanasema
wanatafuta billion 7 kuileta brazil hiyo kwao aisumbui
hii serikali imelaaniwa siku alipokufa nyerere ,
 
Tanzania , ni nchi ya ajabu sana ulimwenguni, na ndio maana inaongoza kichawi na kinajimu.

Baada ya Kawawa kufa Sheikh Yahaya anajitapa mitaani kuwa utabiri wake kuwa mwaka 2009 usingeisha bila kiongozi mkubwa kufa umetimia.

Sasa kama nchi iko hivyo mnataka Gavana aweje?
Naye huyu kutumia bilioni 3 kujenga nyumba wakati nchi inaenda kuomba msaada wa vyandarua na kupewa vyenye dhamani ya milioni 78 wanakuja na kuutangazia umma kuwa ni mafanikio ya JK .

Inatia uchungu sana, nilikuwa Tanga Jimbo la Handeni wakina mama wanachota maji kwenye mto , na tangu Augusti mwaka jana kata ya Kiva pekee imeshapoteza watu 248 kutokana na ugonjwa wa kipindupindu, halafu gavana anajenga jumba ambalo , sijui la kazi gani.
 
Tanzania , ni nchi ya ajabu sana ulimwenguni, na ndio maana inaongoza kichawi na kinajimu.

Baada ya Kawawa kufa Sheikh Yahaya anajitapa mitaani kuwa utabiri wake kuwa mwaka 2009 usingeisha bila kiongozi mkubwa kufa umetimia.

Sasa kama nchi iko hivyo mnataka Gavana aweje?
Naye huyu kutumia bilioni 3 kujenga nyumba wakati nchi inaenda kuomba msaada wa vyandarua na kupewa vyenye dhamani ya milioni 78 wanakuja na kuutangazia umma kuwa ni mafanikio ya JK .

Inatia uchungu sana, nilikuwa Tanga Jimbo la Handeni wakina mama wanachota maji kwenye mto , na tangu Augusti mwaka jana kata ya Kiva pekee imeshapoteza watu 248 kutokana na ugonjwa wa kipindupindu, halafu gavana anajenga jumba ambalo , sijui la kazi gani.
Check hio
 

Attachments

  • Picture 911.jpg
    Picture 911.jpg
    68.8 KB · Views: 44
  • Picture 912.jpg
    Picture 912.jpg
    79.8 KB · Views: 48
  • Picture 913.jpg
    Picture 913.jpg
    58.3 KB · Views: 43
  • Picture 914.jpg
    Picture 914.jpg
    56.5 KB · Views: 40
Wacha hilo tu m'kijiji
nimesikia juzi mawaziri wake mapumbavu wanasema
wanatafuta billion 7 kuileta brazil hiyo kwao aisumbui
hii serikali imelaaniwa siku alipokufa nyerere ,

Nadhani walikua wanatania...
Hivi hawa ni binadamu ama..???
Au ndo sikio la kufa...
Mabadiliko yatakuja kwa lazima iwe isiwe..
Uvumilivu waelekea ukingoni..
Endeleeni kutumbua makodi yetu mkiongozwa na Vasco sijui ataanzia wapi maanake mapumziko yameisha..
 
Nimenong'onezwa kwamba gharama ya kulitunza jumba hilo kwa mwezi ni shs za kitanzania milioni 43
 
Nduli ni mwajiriwa wa Serikali, asingeweza kukataa haki yake ya kupewa nyumba. Angekuwa mwanasiasa anayetafuta umaarufu ningekuelewa. Pia, aliyepitisha ujenzi wa hekalu hilo si Ndulu. Ni Balali, na ukapata baraka za Bodi ya Wakurugenzi.
 
Nimenong'onezwa kwamba gharama ya kulitunza jumba hilo kwa mwezi ni shs za kitanzania milioni 43
Kulitunza! Unamaanisha nini? Nina imani kuwwa huu sasa ni utani eeeh? Si eti eeeh? unamaanisha mavazi, chakula na upkeep ya walio humo ndani au ni maintance ya jengo - usafi, umeme, maji na yanayofanana na hayo.
 
Hao wakina mama wanafiki wakubwa......
Tatizo lao ni elimu na kujitambua kuliko umasikini....

Mbona kwa waganga wa kienyeji wananunua mbuzi na kuku wanapeleka???
Au ni imani kuwa hospitali ni bure na ni kazi ya serikali.....

Bottom line ni kuwa sio wote wanaoenda hospitali za serikali
ni maskini kupita kiasi......
Ni mazoea tu.........


Halafu hao akina mama..
Hizo mimba walizipataje????
Hao wanaume waliowapa hizo mimba
hawana kazi kabisa??????
Walihongwa nini kabla ya kufungua miguu
yao kwa hiyari????
Mbona hizo khanga wanazovaa ni mpya mpya
na bei ya khanga moja sasa ni sh 5000/??????


Kama nikutukana umetukana saaana mkuu we unaishi kwa balali nini???
We ninani usiojua hali ya TZ na mawazo yako ya kijinga kuwa kila mtu aliyepata ujauzito kahongwa ni nani kakuambia hivyo, hujui haki yako na kuwa serikali inapata pesa nying tuu toka kwa hao walalao chini na hujui kuwa ni majukumu ya selikali kuhudumia mambo hayo
SORRY KUKUAMBIA HAUNAZO ILA KWELI HUNA KICHWANI WEWE HUNA KABISAAA. HATA KAMA UNESEMA WALIPIE GHALAMA WALIPIE NINI NDO ZINGETOSHA KUWAPA VITANDA HAO WAKINA MAMA!
 
Back
Top Bottom