Kumbe ndivyo unavyofanya eh? Next time nikija halafu ukadanganya hivyo nitakujibu poa hamna noma niachie tuu funguo, ukirudi utanikuta. Kwishaney.
Duh kuna hawa wanaokuja kuangalia mpira.......kila jumamosi wapo...maskini sofa zangu
Hii miezi miwili huwa wanakusaidia kwenye bajeti au ndio wanategemea kila kitu toka kwako?
vp wakija na bia zao na za kwenu? Halafu wawe wamebeba grill na nyama tamu kuliko zote duniani na masala zake pamoja na mapochopocho mengine kwa ajili ya BBQ?
Duh kuna hawa wanaokuja kuangalia mpira.......kila jumamosi wapo...maskini sofa zangu
yaani bosi ni kama umeniona apa ndo yamenikuta saa ivi jamani sina hamu.lakini lazima nitoke nimepanga ngoma kumi ma nusu nawaaga mi nasepa zangu
Dah, yalinikuta hayo last sunday nilikuwa njiani natoka kanisani ghafla nikapigiwa cm eti tuko njiani tunakuja kutembea. Kwa vile walinifanyia sapraiz na mm nikawatoa kimasomaso nikawaambia mm na wife tuko kwenye mfungo. Waliondoka wamenununa usipime.
Hiyo ni baraka, maana sehemu za outing ziko nyingi sana, ukiona watu wamekuja kwako kufanya outing ya sikukuu yao umshukuru Mungu.
Pia kwenye sikukuu kuna mabalaa mengi sana, kama kuibiwa, ajali na kadhalika, huenda Mungu amekuepusha.
halafu wawe wamekuja na One way ticket, wakitegemea ya kurudia utawapa wewe. Mimi huwa nawafukuza mkuu huwezi kuja nyumbani kwangu bila ya kunitaarifu hata chooni ukiingia unapiga hodi sasa inakuwaje wanakuja moja kwa moja kama wanakwenda Muhimbili au kituo cha polisi.
Ndugu zangu na marafiki zangu wananijua huwa simuonei haya mtu hata akiwa Maza lazima ukweli umfikie na mimi huwa siendagi kwa mtu bila ya kumtaarifu
Mgeni akija nyumbani kwangu bila ya nitaarifu hata kama nipo ndani sifungui mlango na akipiga simu akiniambia nipo nje ndio namwambia sina appointment ya kukutana na wewe na wala sipo nyumbani nimetoka nitarudi kesho. Kama hana Nauli atajua pakuipatia
I am taking my life serious not as a Joke. Waswahili wanasema samaki mkunje angali mbichi, sasa lazima wakubaliane na matakwa yangu sio unakuja kama unakuja kwako, heshimu nyumba ya mtu kama mimi ninavyoheshimu nyumba zao.
Sitaki Ujinga mimi sio Fisadi Kikwete kuchecheka na Mafisadi, Huwa natoa maamuzi mazito wengi wenu hapa JF hamuwezi