Wageni wa 'ghafla' majumbani mwetu.....

Wageni wa 'ghafla' majumbani mwetu.....

BAK, mimi naona ni ustaarabu pale ambapo mtu anakutaarifu beforehand kuwa atakuja kukutembelea. Na katika hizi zama za simu za mkononi hakuna sababu yoyote ile kwa nini mtu asikutaarifu mapema kuwa atakuwa mgeni wako.

Kutaarifu mapema kunampa mtu/ mwenyeji fursa ya kujipanga. Mimi sipendi kabisa kuvurugiwa bajeti zangu.
Sasa hata akikutaarifu, unampikia nini? Si inaafect budget pia? au nikupigie on the 25th ili uweke chakula changu cha 5th na cha 18th katika budget ya november? acheni uchoyo bwana. Chakula cha kupika nyumbani hakina bei. Bei ya vocha na chupa mbili in your favorite club unapika chakula for extra 5 people!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Kusema tu kweli mimi kama mwanamke ninae miliki budget, chakula sio the key thing kinacho maliza budget. kuongeza 2 or three portions haiharibu wiki. Budget iko affected na makadi ya sim bila mpango, fuel, outing etc. an extra plate on the talbe here and there haina effec. Na host mzuni ni yule amesha piga budget yake kwa kucatter hao watu!

Well, kila mtu na uwezo wake.
 
Bajeti yangu ndo inanifanya niishi kwa kujitegemea. Mijitu inayoibuka tu bila taarifa haina umalaika wowote. Ni mivurugaji ya bajeti.
yaani hadi sasa hivi bado ninacheka sana na umenivunja mbavu LOL!! Mkuu NN unaonekana wewe ni mzee wa budget/fiscal conservative na hutaki mchezo kabisa na hela zako.
Lakini rudisha moyo mkuu, dini zinasema wageni ni malaika na ni baraka banaaaa. Waache waje anytime
 
BAK, mimi naona ni ustaarabu pale ambapo mtu anakutaarifu beforehand kuwa atakuja kukutembelea. Na katika hizi zama za simu za mkononi hakuna sababu yoyote ile kwa nini mtu asikutaarifu mapema kuwa atakuwa mgeni wako.

Kutaarifu mapema kunampa mtu/ mwenyeji fursa ya kujipanga. Mimi sipendi kabisa kuvurugiwa bajeti zangu.

Nakubaliana nawe NN, tena mgeni kama huyu anayekutaarifu mapema mimi huwa namheshimu sana kwa kuonyesha kuthamini muda wangu. Kama siku hiyo nina nafasi na sioni tatizo lolote la kumkaribisha basi nitamkaribisha tena kwa mikono miwili atakula na kusaza na kama sitaki mgeni siku hiyo basi nitamwambia atafute siku nyingine ya kuja nyumbani, na siyo tabia ya kuzuka tu bila taarifa.
 
Sasa hata akikutaarifu, unampikia nini? Si inaafect budget pia? au nikupigie on the 25th ili uweke chakula changu cha 5th na cha 18th katika budget ya november? acheni uchoyo bwana. Chakula cha kupika nyumbani hakina bei. Bei ya vocha na chupa mbili in your favorite club unapika chakula for extra 5 people!

Siyo uchoyo. Ni hali halisi tu ya maisha.

Piga picha kila weekend una wageni ambao wanakuja unannounced. Hapo lazima bajeti ivurugike unless you have an unlimited supply of money. But some of us budget everything including money for leisure. I don't like spending my hard earned money on things I haven't budgeted for...
 
yaani hadi sasa hivi bado ninacheka sana na umenivunja mbavu LOL!! Mkuu NN unaonekana wewe ni mzee wa budget/fiscal conservative na hutaki mchezo kabisa na hela zako.
Lakini rudisha moyo mkuu, dini zinasema wageni ni malaika na ni baraka banaaaa. Waache waje anytime

Hahaha...Sheriff, mimi sipingi wageni. Napenda wageni waje ila waje kwa mpangilio. Kama ilivyo illegal immigration kwa US....watu wengi hawapingi immigration. Wanachopinga ni illegal immigration.
 
Upo nyumbani kwako umepumzika,ni wikiendi au sikukuu
kama leo.una mipango yako binafsi
labda unataka kulala tu siku nzima
au kutoka na mkeo/mumeo bf/gf so mnavuta vuta mda hivi....

ghafla bin vuu wanaibuka 'wageni ' pengine ndugu zako au wa mwenzio
au tu marafiki na jamaa, wamekuja 'kukutembelea' au
'kusheherekea sikukuu' labda wamekuja na 'watoto wao'
na muelekeo wao ni kushinda hadi jioni ndo warudi makwao.....

dah jamani mimi hili huwa linanikera mno....
siku hizi si kuna simu????inakuwaje jamani??????

nyinyi ikiwatokea mnafanya nini?????????

Nilipokuwa mdogo nakumbuka tulipata ugeni wa uncle wangu na mkewe na mtoto wao waliibuka one night tulikaa nao for 10 days. Wakati bado wapo, shangazi nao akaja na binti yake alikuwa mgonjwa akafikia kwetu for 2 weeks. Wakati huo huo shemeji yangu nae alifikia kwetu kwaajili ya shughuli zake za kikazi. Lakini baba na mama hawakulalama wala kuchukia. chakula kilipikwa na kila mtu alikuwa ni mwenye furaha.
 
Hiyo ni baraka, maana sehemu za outing ziko nyingi sana, ukiona watu wamekuja kwako kufanya outing ya sikukuu yao umshukuru Mungu.
Pia kwenye sikukuu kuna mabalaa mengi sana, kama kuibiwa, ajali na kadhalika, huenda Mungu amekuepusha.

Sawaa hilo linaeleweka.....swali ni kwamba wameshindwa kupiga simu kutoa taarifa ya ujio wao wajameniii???!!!!! Mambo mengine ni uswahiliiii too much,nini maana ya kuwa na simu bwana???!!!! Hata kama nimeamua kukaa ndani ili kuepuka vurugu za barabarani pia nahitaji mapumziko yangu na familia. INAKERAAAA
 
wakiwa ni wazazi nauwa safari ila marafiki majirani ratiba haibadiliki mkuu
 
Haya mambo ya kuarifiana yameanza miaka hii ya teknolojia mpya (simu na mitandao), huko nyuma hata mtu akitoa taarifa kabla ilikuwa ya salamu za mdomo au barua. Lakini ukweli wapo ambao hawatoi taarifa hata wangekuwa na simu ngapi. Kuhusu chakula, "wanachokula watatu wanaweza kula sita, lakini kuna mengine yanaudhi na hayavumiliki.

Mfano ni hilo la wageni kutoka mikoani au vijijini, wanakuja kikundi na watoto wao. Wamekuja na tiketi za kuja, za kurudi utoe wewe. Ukisema uwakomoe usiwape nauli, watabakia hapo miezi; ukitoa nauli, wakirejea walikotoka wataenda kusifia kuwa pesa unazo. Nyumba uliyojenga vyumba vitatu (chako, cha watoto na cha wageni) unashitukia imejaa kama nyumba ya ndege mpaka wengine wanalala sitting. Chooni foleni, wasojua matumizi ya choo wanapakaza vinyesi kila kona; nguo zimezagaa kila pembe...Bujibuji, baraka ya aina hii ninaitilia mashaka.
 
Nilipokuwa mdogo nakumbuka tulipata ugeni wa uncle wangu na mkewe na mtoto wao waliibuka one night tulikaa nao for 10 days. Wakati bado wapo, shangazi nao akaja na binti yake alikuwa mgonjwa akafikia kwetu for 2 weeks. Wakati huo huo shemeji yangu nae alifikia kwetu kwaajili ya shughuli zake za kikazi. Lakini baba na mama hawakulalama wala kuchukia. chakula kilipikwa na kila mtu alikuwa ni mwenye furaha.

hata kama baba na mama hawakulalama
lazima kuna kitu kilibadilika
si ajabu matunda na soda yaligeuka 'anasa' kipindi hiko
 
Dawa yao unawazuga tunataka kwenda muhimbili kunamgonjwa apo lazma waage wakisepa tu namwambia wife niletee castle lite afu niwekee movie ya ong-back nijiachie

"Pole sana ndugu, wacha tuongozane tukamjulie hali mgonjwa"
Sijui utafanyaje?!
 
"Pole sana ndugu, wacha tuongozane tukamjulie hali mgonjwa"
Sijui utafanyaje?!

Hahahaaaaaa nimecheka sanaaa.....ilinikuta hiyo(ila mm nilisema naenda town) mtu alinipa nitakusindikiza unapoenda haina shida maana hata sina haraka ya kurudi nyumbani! We achaaaa kuna watu ving'ang'aaaa
 
yote tisa! Mie kila mwezi wa sita na wa 12 napata suprise ya ndugu toka amerika! Hawafikii hotelini na hawasemi wanakuja lini. Hata ukinuna au kujifanya unasafiri wanauchuna na wanakaa miezi 2! Yaani wee acha tu. Kuna wakati niliwapigia na kuwaambia wasifikie kwangu lakini ndio kwanza wakaongezeka idadi!
 
yote tisa! Mie kila mwezi wa sita na wa 12 napata suprise ya ndugu toka amerika! Hawafikii hotelini na hawasemi wanakuja lini. Hata ukinuna au kujifanya unasafiri wanauchuna na wanakaa miezi 2! Yaani wee acha tu. Kuna wakati niliwapigia na kuwaambia wasifikie kwangu lakini ndio kwanza wakaongezeka idadi!

duh...na wewe unaenda kwao pia au wao tu?
 
Wengine tunaishi kwa bajeti bana. Sasa haya mambo ya kuibukiana bila taarifa ndo mwanzo wa kuharibiana bajeti.

NN inategemeana aisee. Kuna wageni walitembelea home bila taarifa na wakaja na mikungu miwili ya ndizi, matunda, mboga za majani na nyama mwitu toka shamba.
 
yote tisa! Mie kila mwezi wa sita na wa 12 napata suprise ya ndugu toka amerika! Hawafikii hotelini na hawasemi wanakuja lini. Hata ukinuna au kujifanya unasafiri wanauchuna na wanakaa miezi 2! Yaani wee acha tu. Kuna wakati niliwapigia na kuwaambia wasifikie kwangu lakini ndio kwanza wakaongezeka idadi!

Hii miezi miwili huwa wanakusaidia kwenye bajeti au ndio wanategemea kila kitu toka kwako?
 
NN inategemeana aisee. Kuna wageni walitembelea home bila taarifa na wakaja na mikungu miwili ya ndizi, matunda, mboga za majani na nyama mwitu toka shamba.
Hapo sasa, kama unatabia ya kukataa wageni sababu ya msosi kinakushuka shu!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
NN inategemeana aisee. Kuna wageni walitembelea home bila taarifa na wakaja na mikungu miwili ya ndizi, matunda, mboga za majani na nyama mwitu toka shamba.

Hao ni wastaarabu maana at least walikuwa considerate. Wouldn't you say so?
 
Hapo sasa, kama unatabia ya kukataa wageni sababu ya msosi kinakushuka shu!

RR, more than 90% of them huwa wanakuja mikono mitupu....na vijizawadi ambavyo kwa kweli havimalizi hata wiki halafu wanategemea kuwepo kwa mwezi au hata zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom