A
Anonymous
Guest
Mimi ni miongoni mwa Wafanyakazi 1,299 waliokuwa Watumishi katika Mradi wa AFYA ENDELEVU chini ya BENJAMIN MKAPA FOUNDATION uliokuwa unafadhiliwa na USAID.
Baada ya USAID kufuta Mradi wa AFYA ENDELEVU kuanzia tarehe 24/3/2025, Taasisi yetu (Mkapa Foundation) ilitutumia notice ya kutupa taarifa kuwa tufanye kazi hadi tarehe 31/5/2025 ambapo tungelipwa stahiki zetu tunazo wadai ikiwa ni pamoja na mishahara ya mwezi Aprili na Mei, 2025.
Kilichotokea ni kuwa tulilipwa mshahara wa mwezi Aprili 2025 pekee ila ule wa Mei hatujalipwa hadi sasa, ilipofika tarehe 28/5/2025 tulifanya kikao na Viongozi wa Taasisi hiyo, ambapo walituahidi kutulipa stahiki zetu zote ifikapo tarehe 31/5/2025 na hata ikizidi sana itakuwa 3/6/2025.
Mpaka kufikia sasa tunaelekea kuitafuta Julai 2025 hatujalipwa stahiki zetu za kuachishwa kazi pamoja na mshahara wa Mei 2025, kwani kila tunapouliza tunapigwa danadana, hatujui pakuelekea, tunaomba msaada wa kutusemea.
Baada ya USAID kufuta Mradi wa AFYA ENDELEVU kuanzia tarehe 24/3/2025, Taasisi yetu (Mkapa Foundation) ilitutumia notice ya kutupa taarifa kuwa tufanye kazi hadi tarehe 31/5/2025 ambapo tungelipwa stahiki zetu tunazo wadai ikiwa ni pamoja na mishahara ya mwezi Aprili na Mei, 2025.
Kilichotokea ni kuwa tulilipwa mshahara wa mwezi Aprili 2025 pekee ila ule wa Mei hatujalipwa hadi sasa, ilipofika tarehe 28/5/2025 tulifanya kikao na Viongozi wa Taasisi hiyo, ambapo walituahidi kutulipa stahiki zetu zote ifikapo tarehe 31/5/2025 na hata ikizidi sana itakuwa 3/6/2025.
Mpaka kufikia sasa tunaelekea kuitafuta Julai 2025 hatujalipwa stahiki zetu za kuachishwa kazi pamoja na mshahara wa Mei 2025, kwani kila tunapouliza tunapigwa danadana, hatujui pakuelekea, tunaomba msaada wa kutusemea.