Mkuu mi sio mchaga, ila kwa hili unatetereka. Wachaga wana kitu ambacho ni "unique" especially kuchangamkia fursa zinazokuja mbele yao!! Binafsi nipo Katavi mkoa mpya, ila speed ya hawa jamaa sio mchezo. Nilibahatika kwenda Kinshasa, nilikutana na wachaga wanamiliki daladala kule! Starehe kwake sio mpango wa maisha. Na kitu ambacho hukijui, wanajali kwao kuliko kabila lolote Tz!!
Amini usiamin, miji mingi imepwaya kutokana na hawa jamaa kwenda kwao kula xmas. Huu utamaduni ni mzuri mno, just imagine wanasaka noti mwaka mzima, na mwisho wa mwaka wanaenda kujumuika na kula na wale waliowaacha kule vijijini.
Kwa bahati mbaya, wengi wetu hatuelewi, tunadhani ndivyo sivyo! Big up wachaga, hata kama wapo nje ya nchi, watakuja mwisho wa mwaka, what a lovely culture!!!