Wa mwisho ndiyo mshindi

Wa mwisho ndiyo mshindi

hahaa, ile gemu haiwezi pata mshindi kwa kua haina refa, labda tumwombe moderator mmoja awe refa, kuna jamaa alimalizia kwa kichina ila bado wakakichakachua!!
Wakakichakachua kirobota cha mitumba bila mwenyewe kutambua
 
hahaa, ile gemu haiwezi pata mshindi kwa kua haina refa, labda tumwombe moderator mmoja awe refa, kuna jamaa alimalizia kwa kichina ila bado wakakichakachua!!

Hatuwezi kumaliza game kwa kuchanganya lugha, kwa sababu ukiweka kichina wengine hatukielewi ndio maana hatukuendeleza. Ngoja nimtafute mwanzisha thread. Ataiona kwenye alert zake.
 
Habari wanaJF,

Nnaomba tucheze mchezo unaitwa "wa mwisho ndo mshindi"......... Ni mchezo rahisi sana, unaanzisha sentensi kwenye neno la mwisho la sentensi aloandika mwenzako.

Mfano:

Ualimu Tanzania ni kazi ngumu kiasi

Kiasi ambacho kama hukuzoea maisha ya tabu, utalalama kila siku

Siku uianze vizuri bwana, ukiianza vibaya lazima utukane mwenzio

Mwenzio ni mtu ambaye mnaweka hisia zenu pamoja bila kusalitiana kama dr. Ulimboka na madkatari

Madaktari wa Tanzania wanahitaji kulipwa zaidi........ (tuendelee kwa mtindo huo wanaJF, wa mwisho ndo winner.. Karibuni sana)


Mkuu Wambuzi njoo upulize kipenga cha kumaliza game hapa. Watu tumefikiria neno la kumaliza hii game uliyoanzisha tukalipata, lakini naona watu wameendelea kuchakachua. Sema kama hapa chini haionyeshi hii game sasa imekwisha;

Tutusa humu ndani ni mmoja tu!
 
Mkuu Wambuzi njoo upulize kipenga cha kumaliza game hapa. Watu tumefikiria neno la kumaliza hii game uliyoanzisha tukalipata, lakini naona watu wameendelea kuchakachua. Sema kama hapa chini haionyeshi hii game sasa imekwisha;
imekwisha tambulika kuwa baadhi wanaSiasa wa bongo ni washirikina
 
Back
Top Bottom