Vita Kali ndani ya CHADEMA

Vita Kali ndani ya CHADEMA

ma kweli mnakosa kazi za kufanya.. mtanisamehe.
Nilipoona mada hii nimekuja kwa kihoro nikitaka kufahamu labda kuna fisadi mwingine kaibuliwa ndani ya Chadema. Kumbe udaku mtupu ambao hauna hata kichwa.
Tanzania kuna viongozi wengi wenye matatizo ya kimaisha kama ya Dr.Slaa ikiwa haya ni ya kweli. matatizo haya kamwe hayawezi kummaliza mtu kisiasa ni Upumbavu mtupu!..
Guys ebu tupandishe daraja kijiwe hiki, hizi habari za maisha ya Slaa kutokuwa na nyumba, sijui kapanga zinahusu nini humu!
 
kilitime, hiyo unayosema inaitwa hekima. Na anayetarajia viongozi wazuri wasio na makosa, atasubiri hadi kiama!

Tukiwa makini tunaweza kupata wazuri kulinganisha na tulionao, mifano tunayo kwenye majimbo na kila mahali!!! Kwa mfano... Kitila Mkumbo ni kiongozi, mwenye akili yeyote anajua hilo,,, lakini Iddi Azan sio kiongozi wa kupewa Jimbo kubwa kama la Kinondoni... Dada Betty Mkwasa ni Mkuu wa Wilaya, before that aliongoza idara yoyote? pale ITV yenye wafanyakazi wangapi sijui?! maana leader, not manager anaonekana mapema sana.


Ndio maana napendekeza tukwepe sana mambo ya binafsi ambayo hayaingiliani na kazi au majukumu ya mtu na si kinyume cha sheria au hakileti mgongano wa aina fulani wa kimaslahi. Na hasa masuala ya ngono! Kuanzia enzi za Adam hadi leo, viongozi wengi wamekuwa wakijaribiwa kwa hilo na hilo halina chama, dini, itikadi n.k
Kweli mzee umenena!!! na mimi niko na wewe ingawa sikuona umuhimu sana wakuongelea mambo haya hali ikijulikana DODOMA kipindi cha Bunge mambo yako vipi!!!

Hata wengi wetu tunaopiga kelele hapa inawezekana tunapata kachumbari nyingine pembeni au tunakodoa kodoa macho pembeni (tukiwa breki ya JF). Lakini hilo peke yake halitufanyi tuache kuikosoa serikali, vyama n.k
Kukosoa kuko kwa aina mbili, kuna ushabiki,,, una-wish fulani akosee ili nipata sababu ya mimi kuingia, na kuna wale ambao wanakosoa-objectively... mifano iko wazi kwa wabunge wa-CHADEMA kazi wanafanya na watanzania wanajua hilo..

Na hilo halihusiani na kufumbia macho maadili, bali kuyaweka maadili katika maudhui yake hasa. Kwamba, kiongozi ambaye amekula uroda wa Katibu Muhtasi wake kwa hiari yao wenyewe, lakini akakemea na kuzuia watu kula fedha za umma na kuwatimua.. nitamchagua nikilinganisha na kiongozi anayeacha watu wale mali ya umma na kuwafumbia macho huku akijifanya yeye mswalihina!! the less of two evil sir!!

sawa twende mbele
 
Wapendwa:

Nilitoa udhuru siku za nyuma kwamba nitakuwa msomaji tu tena wa mara chache hapa JF na kwa kweli kwa muda mrefu nimeacha kuchangia chochote katika ukumbi huu. Hata hivyo suala hili "Vita Kali ndani ya CHADEMA" nimeshindwa kulivumilia na limenifanya nirejee ukumbini japo kwa leo na kuchangia.

Kwa haraka ningeweza kusema kwamba habari hii ni UDAKU hivyo kuipuuza. Ila kwa mtiririko wa matukio yanayoendelea ya kumchafua Dr Slaa na CHADEMA nimekubaliana na wahenga kwamba- Mzaha Mzaha; hutumbuka usaha. Uwongo ukisemwa sana; na ukikaliwa kimya-unaweza kuaminika kuwa ni ukweli. Lakini bahati nzuri ni kuwa; kama hayati Bob Marley alivyowahi kuimba- ‘unaweza kuwadanganya watu wachache kwa muda mchache; lakini huwezi kuwadanganya watu wote wakati wote!

Naandika ujumbe huu ikiwa ni masaa machache toka nilipotoka kwenye mkutano na waandishi wa habari kujibu Hotuba ya Kikwete aliyoitoa kwa taifa wakati akihitimisha wiki ya vijana ya Taifa mkoani Arusha. Rais Kikwete pamoja na mambo mengine alitumia muda huo kuwaambia vijana kuwa wawapuuzie viongozi wa kisiasa wanaotaka kuwatumia vijana kwa kumwaga damu zao kwa ajili ya kuingia madarakani. Nilimjibu mambo kadhaa katika mkutano huo wa waandishi wa habari; Kama vyombo vya habari vya hapa nyumbani vitaandika yale niliyosema natumai mtayasoma kwa kina.

Lakini kwa ufupi; kauli ya Rais ililenga kuwachonganisha wanasiasa wa upinzani na vijana kwa kizingizio kuwa wanataka kuvunja amani hii ni kwa kuwa Rais ametoa kauli hii huku ushirikiano wa upinzani ukiwa umempa Rais mpaka Novemba kuunda Tume Huru ya kuchunguza ufisadi uliotajwa na Dr Slaa ama sivyo upinzani utaongoza maandamano nchi nzima. Leo nimemshangaa Rais Kikwete badala ya kuitumia wiki ya vijana ambayo ndicho kipindi mahususi cha kuzungumza na vijana kueleza ni vipi ametekeleza ahadi yake ya ajira milioni moja kwa vijana; ametumia siku hiyo kufanya propaganda za amani!

Nimemweleza Rais kuwa kwa kauli yake ni ya kichochezi pengine ni ishara ya dola kujiandaa kumwaga damu kama vijana wa kiandamana Novemba ili baadaye isingizie ni sababu ya wapinzani(walifanya hivyo Zanzibar Januari 26 na 27, 2001). Nimekumbusha Kikwete kwamba amani ni tunda la haki. Kwa kuwa alizungumza Oktoba 14 nimemkumbusha Kikwete kuwa baba wa Taifa alisema kama kuna vitu vinavyoweza kusababisha kumwaga damu nchini ni Ufisadi, Kutokupatikana kwa haki na kuongezeka kwa matabaka katika Jamii. Nimewaambia vijana wampuuze Rais Kikwete. Nimewaambia vijana waendelee na harakati za kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za nchi hii. Nimewaambia vijana ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za taifa vikiendelea ajira zitaendelea kuwa ndoto na maisha bora kwa kila mtanzania yataendelea kuwa kauli mbiu tu ya Kikwete na wenzake. Nimemwambia Rais Kikwete kwamba kauli yake ya kuwa ameicha TAKUKURU ichunguze madai hayo na kwamba haitaingiliwa na mtu yoyote ikiwemo yeye ni ya kinafiki kwa kuwa tayari imeshaingiliwa na yeye na viongozi wengine wakuu wa serikali. Nimemkumbusha Rais kwamba ni yeye aliyezungumza na waandishi wa habari na kusema Mkapa aachwe apumzike na kwamba serikali yake haiwezi kumchunguza. Matokeo yake ni TAKUKURU kutangaza kwamba haitamchunguza Mkapa. Mkapa ambaye ametajwa na Dr Slaa katika orodha ya mafisadi. Hapa ni wazi Rais ameingilia uchunguzi wa TAKUKURU na kuuzuia! Spika Sitta alifunga mjadala wa Mengi na Malima bungeni; siku chache baadaye TAKUKURU ikatangaza kwamba haitachunguza madai ya Ndesamburo kuwa Lowasa amemwambia kuwa baadhi wabunge wamepewa rushwa na Manji kwa kuwa Spika amefunga mjadala bungeni. Huku si kuingiliwa kwa TAKUKURU? Si ajabu hata ripoti ya TAKUKURU kusema hakuna rushwa kwenye mchakato wa zabuni ya Richmond baada ya Lowasa kusema mvua zimeshanyesha sasa watanzania wasijadili tena kuhusu Richmond. Ripoti ya PPA bahati nzuri imeonyesha wazi kuwa kuna mkono wa Kigogo nyuma ya mkataba wa Richmond. Ni wazi, maneno niliyoyazungumza, ya kusema Rais apuuzwe na kauli yake ni ya kinafiki, ni makali na pengine ni ya kumvunjia heshima Amiri Jeshi Mkuu. Lakini hapo ndipo Rais Kikwete alipotufikisha kwa kushinda kuwachukulia hatua watu wake wa karibu mpaka sasa. Miezi imepita tunaendelea kumbembeleza Rais, sasa imefika hatua ya kuita panga ‘panga' na si kisu kikubwa! Pengine hapa Rais atajua sasa kwamba ‘usanii umetosha'; ni wakati wa kuchukua hatua. Dr Slaa ameonyesha mfano kwa kusimamia ukweli na kutaja majina hadharani. Hivyo niliposoma ujumbe huu wa ‘vita kali ndani ya CHADEMA' umegusa hisia zangu na kunikumbusha mambo mengi.

Nichangie mawazo yangu kuhusu waraka huu wa ‘vita kali ndani ya CHADEMA', naomba radhi kama nitarudia baadhi ya mambo ambayo pengine yameshasemwa na wachangiaji wengine. Sijapata wasaa wa kusoma michango ya watu wengine; nimeona niujibu ujumbe huu moja kwa moja.

Naomba nieleweke kwamba nitakayoandika hapa kwa kiasi kikubwa ni msimamo wangu binafsi kama John Mnyika na pengine kama Mkurugenzi wa Vijana lakini hayawasilishi msimamo wa CHADEMA kama taasisi.

Niombe radhi pia kwa kiongozi mwingine yoyote wa CHADEMA nitayemtaja humu hususani Dr Slaa kwa kuwa sijapata wasaa wa kujadiliana nae wala kumwuliza maswali kwa yale yaliyomo katika ujumbe huu. Niandikayo humu ni kadiri ya ukweli ninavyoulewa mimi.

Pia nikuombe radhi ndugu yangu unayenisoma kwa kuwa mara nyingine naweza kuacha kuwasiliana nawe na kujikuta nikiwasiliana na aliyeandika huu ujumbe ama walioko nyuma ya huu ujumbe. Hii ni kwa sababu; ninazo taarifa kwamba yupo mmoja wao wa waliotajwa katika orodha ya mafisadi ambaye ndiye anayeendesha mikakati ya kuchafuana kwa kutumia kikosi chake cha uchafuzi; alianza kwa kujaribu kunichafua Mimi na Zitto; naona sasa amehamia kwa Dr Slaa. Sitamtaja jina katika hatua ya sasa; lakoni hali hii ikizidi- nitaanika ukweli hadharani. Sitavumilia katika Tanzania ya leo kuona tukichafuliwa; alivumilia Dr Salim Ahmed Salim- kwa sasa sidhani kama uvumilivu pekee utatusadia kama taifa: Baadhi ya majipu lazima yapasuliwe, usaha utoke, tuuguze kidonda, tubaki na jeraha ambalo na lenyewe huweza kutoweka!

Dr Slaa yuko ziarani Marekani(taarifa ya ziara yake na mafanikio yanayoendelea kupatikana ikiwemo katika kuwasaidia walemavu; Mwenyekiti Freeman Mbowe yuko nchini Uingereza; Zitto mahali Fulani hapa Tanzania.

Na hapa naanza kuona mapungufu ya ujumbe huu unaosambazwa: Mwandishi anasema ujumbe huu unasambazwa na Mbowe na Zitto baada ya kipindi cha Ze Comedy na kwamba unatokana na Vita ndani ya CHADEMA- Mbowe yuko Uingereza wiki kadhaa sasa; Zitto alikuwa Kenya na sasa Tanzania. Mbowe hajakiona kipindi cha Ze Comedy, na hayuko Tanzania- sijui wamekutana wapi na Zitto na kuanza kuusambaza huo ujumbe? Na kama wao ndio wanaousambaza ni kwa njia gani? Iweje ujumbe huo uwe ni taarifa ya aliyeandika kuwa Mbowe na Zitto wanasambaza ujumbe ambao hakuna anayejua uko wapi? Mbowe na Zitto wamevipigana hivyo vita dhidi ya Slaa ndani ya CHADEMA lini wakati wako nchi tofauti? Hii ni ishara ya wazi kwamba mwandishi wa ujumbe huu amelenga kuwachonganisha Dr. Slaa, Mbowe na Zitto! Huu ni mkakati katika mapambano unaoitwa ‘divide and rule'; wagawanye uwatawale. Naamini Dr Slaa, Mbowe na Zitto hawawezi kuingia katika mtego mdogo kama huu!

Ujumbe wangu kwa uliyeandika-usitarajie kabisa kwamba Dr Slaa; Zitto na Mbowe wataacha kuendelea kujadili ufisadi na hatma ya rasilimali za Taifa na kuanza kugombana wao kwa wao. Wataendelea kupambana na mafisadi mpaka kieleweke. Kumbuka kwamba CHADEMA inafanya kazi kama timu; Orodha aliyoitoa Dr Slaa imepita mikononi mwa viongozi wote hawa kabla ya kutoka. Kumbuka pale Jangwani Dr Slaa alikabidhi makabrasha yote ikiwemo ushahidi kwa Mwenyekiti Mbowe. Hii sasa imeshakuwa hoja ya umma; kumchafua mtu mmoja Dr Slaa haitawasadia mafisadi kujisafisha. Orodha hii ya ufisadi sasa iko mikononi kwa viongozi wa vyama, wa dini, mabalozi, wanaharakati na hata baadhi ya wananchi.

Mimi ni Mkurugenzi wa Vijana Taifa; hivyo ni mmoja watendaji wakuu wa kila siku katika chama makao makuu; na naingia vikao vya chama kwa nafasi yangu, hakuna kitu kama "hali ya kisiasa isiyotarajiwa kufahamika ndani ya chama cha CHADEMA" ama "Vita Vikali ndani ya CHADEMA" kama mwandishi anavyotoka kupotosha. Mwandishi atueleze vita hivyo vimepiganwa wapi na lini?

Mwandishi asijaribu kupotosha; ni lini na wapi Dr Slaa alizungumza na marafiki zake na kuwaambia kwamba tuhuma zake hazina uthibisho na kwamba ameshangaa kupata umaarufu na watu wamezipokea? Yoyote mwenye akili timamu akisoma orodha ya ufisadi atakuwa ameona jinsi hoja hizi zilivyo na ushahidi tena mwingine kutoka kwenye serikali yenyewe. Hivyo nyie MAFISADI, msidhani watanzania ni wajinga kiasi cha kughilibiwa na ‘michezo yenu ya maneno'; jibuni hoja zilizoibuliwa na serikali ijieleze kiunagaubaga kwa wananchi. Mlisema ni uzushi na mtakwenda mahakamani; mnasubiri nini? Subira yenu bado si salama yenu; kwa kuwa sasa suala hili liko mikononi mwa mahakama ya umma!

Kwa nini Mbowe na Zitto wawe na chuki na Dr Slaa? Kwani nani alisema umaarufu ni keki kwamba mmoja akipata kipande kikubwa zaidi anawanyima wengine? Umaarufu ni hali isiyo na mipaka na isiyogawanyika; yoyote anaweza kuipata wakati wowote kiasi chochote!. Zitto atagombeaje Urais 2010? Inaelekea mmeshajipanga kubadili katiba ili imruhusu agombee nini? Kwa kadiri ilivyo sasa umri wa kugombea urais ni miaka 40 ambayo Zitto hatakuwa nayo 2010. Kumtaja kwenu Zitto hapa ni aidha ishara ya kutokujua au makusudi ya kuchonganisha. Haitawasaidia; Dr Slaa, Mbowe na Zitto si wanajuana! Niko karibu sana na Slaa; sijawahi kusikia akitamka kwamba ana ndoto ya Urais. Nawajua wenye ndoto ya Urais kadhaa katika CHADEMA, Slaa si mmoja wao. Lakini hata kama angekuwa na ndoto hiyo si kitu kibaya; ni suala zuri tu- kama una maono ya kupinga ufisadi na kusimamia rasilimali za taifa na una nia, sababu na uwezo kwa nini usiote?

Kwamba anatoa orodha ya ufisadi kwa sababu za maslahi yake binafsi? Hilo silijui! Nijuavyo mimi, siku moja tulikuwa na Dr Slaa ofisini, tulikuwa tunajadili hili suala la ufisadi; siku chache baada ya Slaa kumkabidhi hoja Jangwani Mwenyekiti Mbowe na kuipa muda serikali kuzifanyia kazi ama sivyo angetaja majina hadharani. Nilijifunza mengi kutoka kwa Mzee huyu; kubwa kuliko yote ni uvumilivu wa Mzee huu na kupenda kwake kufuata utaratibu. Niliona wazi jinsi ambavyo alijitahidi sana suala hili liiishie bungeni kwa bunge kuchukua hatua; Spika Sitta pengine kwa shinikizo la Lowasa. Hoja yenyewe aliyokuwa aitoe bungeni kutoka kamati teule iundwe.

Lakini bado Mzee huyu akawa mvumilivu akaipa muda serikali- lakini pamoja na hayo Kikwete hakuchukua hatua zozote. Nikamuuliza kama Kikwete hata chukua hatua itakuwaje? Akasema ni wazi atataja majina hadharani. Na kweli akafanya hivyo; nilichojifunza ni kwamba alikuwa na vitu viwili mbele yake: kunyamaza kimya, kukubali kuitwa mwongo na kuwaacha mafisadi wapete ama kusimama, kusema ukweli, kulinda heshima na kutetea rasilimali za taifa. Dr Slaa akachagua kilicho bora; kwa kuchagua ukweli amekuwa adui wa waongo na mafisadi. Nilimuuliza wakati huo kama yuko tayari kufa ama kuchafuliwa; alisema yuko tayari kwa lolote. Nilimwambia; tuko pamoja nawe-pamoja tutashinda!

Mwandishi anasema-‘Mbowe na Zitto wameepa kummaliza Dr Slaa'!- huu ni uzushi wa mwaka. ‘Mbowe na Zitto wameamua kuanika madhambi ya Dr Slaa!'-madhambi yapi hayo na wapi? Kwamba Dr Slaa na Zitto wametumia mamilioni kuyazika madhambi ya Dr Slaa ili yasifahamike?- hiki nacho ni kioja kingine cha karne! Ni njia zipi hizo za mamilioni kwa madhambi yapi?

Kuhusu Dr Slaa alifukuzwa upadri!- mimi ni Mseminari wa zamani wa kikotoliki, hivyo naelewa kwa kiasi cha kuridhisha taratibu za ufukuzwaji wa mapadri na mchakato wa kuacha upadri(ingawa upadri ni sakramenti isiyopaswa kufutika). Na niliwahi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wanafunzi Wakatoliki Mkoa wa Dar es salaam. Nafahamu kuwa Dr Slaa ni kati ya mapadri wachache sana(na kuna uwezekano kuwa ni padri pekee hapa nchini) aliyeacha upadri kwa kufuata taratibu zote za kisheria na kupata kibali, ndio maana mpaka sasa anaendelea kuheshimika katika medani za TEC. Mbona hanaouzua haya hawaendi Baraza la Maaskofu kuthibitisha madai yao?

Kwamba "Dr Slaa amekula fedha za Walemavu"; huu nao ni uzushi mwingine? Walemavu wa wapi hao wasiosema kwamba wameliwa hela zao mpaka habari zianze kusambaa baada ya Dr Slaa kutaja orodha ya mafisadi? Dr Slaa ametumikia Tanzania Legue for Blind(TLB) kwa muda mrefu kama mtendaji, na wakati anaondoka walemavu walimlilia na wakamfanya kuwa mjumbe wa baraza lao wadhamini mpaka sasa. Kama angekuwa amewaibia; wangemuacha vipi kuwa mjumbe hadi leo? Kadhalika Dr Slaa mpaka sasa ni Mwenyekiti wa Shirika la CCBRT ambalo linashughulika pia na walemavu pamoja na magonjwa ya macho nk.

Mwandishi amenesema kwamba Dr Slaa ‘ugonjwa mkubwa'! Hili nalo ni jipya kabisa kwangu. Labda mwandishi atuambie ni ugonjwa gani huo? Maomba ya kuandika ugonjwa mkubwa na kuyaacha hivyo yanalenga kumfanya anayesoma aweke majibu yake anayoyataka. Si kweli kwamba Dr Slaa anakwenda Afrika Kusini mara kwa mara. Kwa miaka kadhaa niliyofahamiana naye amekuwa akienda Afrika Kusini hususani kwa masuala ya SADC. Ni kweli mwaka 2006 alilazwa Agha Khan baada ya kuugua akiwa kwenye vikao cha SADC; aliondoka na jeraha na baadae likampa infection; aliporudi Tanzania akaenda hospitali mwenyewe-madaktari wakashauri alizwe afanyiwe operesheni ndogo. Nilikwenda hospitali mara kadhaa kumwangalia; haikuchukua muda akatoka na kuendelea na kazi kama kawaida.

Kwamba Slaa alimuua Mume wa Mtu Mjerumani ili arithi mkewe; hilo nalo linachekesha. Wewe mwandishi wa waraka huu ujue kuwa Dr Slaa ameua mume wa mtu kwa kushirikiana na Mkewe ujerumani vyombo vya upelelezi vya Ujerumani visijue na kuchukua hatua! Kama ingekuwa ni ukweli si mkepata sababu nzuri ya kumsakizia kwa serikali ya Ujerumani imkamate na hatimaye asiendelee kuwataja nyinyi mafisadi kwa kuwa atakuwa kifungoni? Kwa nini mnaishia tu kuandika waraka na kuusambaza kwa mtandao?

Mwandishi anasema Dr Slaa amesambaza taarifa za kughushi toka idara ya usalama wa taifa ili kuwachufua! Hii ni njia nyingine ya kupoteza malengo. Binafsi, nimeshtukia mafisadi. Baada ya Dr Slaa kusoma ripoti toka Usalama wa Taifa kwenda Serikalini inayotaka Waziri Mkuu azuie hoja ya Dr Slaa isijadiliwe Bungeni kwa kuwa serikali haina majibu. Huu ni mkakati wa kutaka wananchi wasiamini ripoti hiyo ambayo baadhi ya maofisa wa usalama wa taifa wanoitakia mema nchi wamempa Dr Slaa; binafsi nimeiona ripoti hiyo.

Mwandishi anasema Mbowe na Zitto wanaungwa mkono na CUF katika mkakati wao huo wa kumchafua Dr Slaa! uzushi mwingine na mkakati wa uchonganishi. Hamtafanikiwa katika mkakati wenu wa kutochonganisha CHADEMA na CUF.

Mwandishi ameibua hoja kadhaa akilenga haiba na faragha ya Dr Slaa katika mkakati wake huo. Bahati njema; binafsi namfahamu Dr Slaa kama si tu Katibu Mkuu wangu bali jirani yangu pale Sinza; niwewahi pia kwenda Karatu kwa ajili ya kuendesha Semina ya Madiwani kule. Mara kadhaa nimekuwa karibu na Mwenyekiti wetu wa Halmashauri Lazaro Masey ambaye pia ni mjumbe wa Kamati kuu akiwa na Dr Slaa hapa DSM na hata nilipokwenda Karatu- ukaribu wa viongozi hawa ni wa kuigwa mfano. Hawa ni watu waoongoza mapambano pamoja yanayoifanya CHADEMA iendelee kuwa chama tawala Karatu.

Kwa hali hii; inaonyesha jinsi ambavyo mwandishi alivyolenga kumchafua Dr Slaa na kuchochea vita ndani ya CHADEMA. Mwandishi analenga kupoteza lengo la kujadili hoja ya mafisadi na utetezi wa rasilimali za taifa.

Mikakati yenu michafu haishindi matakwa ya umma; nakumbuka wakati wa kampeni 2005 nikiwa nagombea Ubunge Jimbo la Ubungo baada ya kuzidiwa hoja mlianza kupanda jukwaani: Mkaanza kusema ‘huyu mtoto hata kufungua nguo ya ndani hawezi', ‘huyu mtoto mwizi', ‘msiomuone mwembamba ana virusi vya ukimwi-atakufa ndani ya mwaka mmoja' nk nk nk. Kumbukeni majibu yangu kwenu: Dhahabu haichafuliwi kwa vumbi!". Ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Period!

Pamoja na maelezo yote haya; kwa kuwa sehemu kubwa ya madai yamemgusa Dr Slaa kama mtu binafsi- namtumia pia ujumbe wa mwandishi huyu ili aweze kuuona. Nawatumia pia Mbowe, Zitto na CUF ili waweze kuusoma.

Najua uongo una utamu wa kusambaa haraka kuliko ukweli ambao baadhi huuona mchungu; lakini mwisho wa siku ukweli una uwezo wa kudumu milele na uwongo hujitenga ukweli unapowasili. Ombi langu kwa yoyote anayeguswa na ufisadi na utetezi wa rasilimali ya taifa asambaze ujumbe huu kwa wengine kadiri inavyowezekana; hii ni kwa sababu mafisadi wanaendelea kusambaza ujumbe wao wa kupotosha. Badala ya kutuacha watanzania tujadili hoja ya Dr Slaa; sasa wanataka tumjadili Dr Slaa. Badala ya hoja wafanya vioja!. Kumbuka, uovu hushamiri wema unapokaa kimya. Albert Eistein aliwahi kusema, kila mtu ana haki ya kupata ukweli-akishaupata ana wajibu wa kuusambaza. Ni wakati wako wa kusimama na kuhesabika. Ni wakati wako wa kusambaza ukweli. Ufisadi na kushindwa kulinda rasilimali za taifa kumelisababishia taifa kupoteza zaidi ya Trilioni 1.3( Zaidi ya bilioni 1300) ambazo zingekwenda kwenye barabara, afya, umeme, elimu na kuongeza mishahara ya watumishi wa umma. Hizi ndio fedha ambazo zimeshindwa kuingia kwenye uzalishaji ikiwemo katika kilimo hatimaye kuna mfumuko wa bei na uchumi uko mikononi mwa wachache.

Nasikitika mwandishi ameacha kuandika jina lake wala anuani yake! Hii ni ishara ya kuhofia anachoandika yeye mwenyewe. Kama Dr Slaa ameweza kuwataja mafisadi hadharani kwa majina; vipi nyinyi mnaogopa kusimama hadharani kusema tuhuma zake?

Hakuna Vita ndani ya CHADEMA; ila kuna vita ya nje inayoongozwa na CHADEMA-ya kupambana na ufisadi na kutetea rasilimali za Taifa. Na haya ndio ambayo tunataka serikali iyatolee ufafanuzi. Ndio maana tunawakumbusha watanzania kauli yetu ya mwaka 2005 kwamba "Mabadiliko ya kweli, hayawezi kuletwa na mafisadi walewale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule, wakiendeleza yale yale eti kwa ari, nguvu na kasi mpya…kwa falsafa ya Chukua Chako Mapema(CCM). ya Chama Cha Mafisadi(CCM)-NIMEONGEZEA…..Tanzania yenye neema haiwezekani.Lazima tudai Mabadiliko ya Kweli na Uhuru wa Kweli kwa falsafa ya Nguvu ya Umma- Hakuna Kulala, Mpaka Kieleweke!

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa

Samahanini: Nimeandika ujumbe kwa haraka bila kuuhariri; kama kuna makosa ya uchapaji mniwie radhi
 
1.
Vita Kali Ndani Ya Chadema

Great, lakini no thank you vita vya ndani ya chama cha Chadema, sisi wananchi kama taifa ni none of our bussines, hili kama lipo kweli ni tatizo la wanachama wa Chadema, matatizo ya ndani ya Yanga na Simba, sisi taifa hayatuhusu!

2.
Jamani hii nimeipata kwenye e mail na naona inazunguka hapa sijaadd chochote nawasiliasha hoja
Quote:

Sawa sawa mjumbe hauwawi, ingawa ni vyema ukasema source yako au kama ni dataz, itaeleweka!

3.
Tarehe 11/10/2007 katika kituo kimoja maarufu cha runinga kulionyeshwa kipindi kimoja cha vichekesho ambacho sasa kimezua jambo ndani ya chama maarufu cha CHADEMA. Katika kipindi hicho, baadhi ya vitendo vichafu vya Dr. WILBROD SLAA vilianikwa hadharani. Awali watazamaji wengi hawakutilia maanani yaliyosemwa kwenye kipindi hicho kwani walidhani ni vichekesho vya kawaida. Lakini sio hivyo tena baada ya hali ya kisiasa isiyotarajiwa kufahamika ndani ya chama cha CHADEMA.

Again, matatizo ya ndani ya Chadema au CCM, hayatuhusu taifa, But, lakini wananchi at large tunaweza kuwa na best interest kama kuna ugomvi wa ndani ya chama tawala, maana kama kusingekuwepo huo ugomvi tusingejionea mkataba wa Buzwagi, jinsi tunavyoibiwa mchana kweupe, halafu pia ni hatari sana kwa mtu yoyote kufikiri kuwa nchi yetu inaweza kuongozwa kwa kutumia maigizo, kwa maneo hayo juu ina maana kuna mtu ndai ya CCM aliyeamua ku-penetrate kwenye usanii ili kupitisha hiyo agenda, kama ni kweli basi ni hatari sana kwa taifa kuongozwa kwa kutumia maigizo, I do not buy that maigizo thing!

4.
Katika siku za karibuni Dr. SLAA amejichotea sifa nyingi baada ya kutoa hadharani tuhuma alizoziita za kifisadi na kutaja majina ya watu aliowaita mafisadi. Ingawaje Dr. SLAA mwenyewe amekiri miongoni mwa marafiki zake kwamba tuhuma zake hazina hata chembe ya uthibitisho lakini amepata furaha ya mshangao kuona jinsi ambavyo tuhuma zake zimempa sifa lukuki ndani na nje ya nchi
.

Hii hoja ni a lie, tena a big lie Slaa amedanganya kwenye evidence za BOT? Kwa hiyo Coondoliza-Rice, alipomuuliza Muungwana kule DC kuwa wao State Department, wanafuatilia kwa makini the outcome ya uchunguzi wa wizi wa BOT, alikuwa akinukuuu uongo wa Slaaa? Hivi kweli unaweza kumueleza hata mtoto mdogo akaamini hii spinning? Hivi unajua Rice ana sources gani na ngapi mpaka kufikia kusema hiyo mbele ya the sitting president wetu? Huuu ni uongo wa mchana, kwenye tuhuma against Mbunge/Mwanasheria Mkono, slaa amenukuu the outcome ya uchunguzi wa kamati ya bunge, ambayo iliwakilishwa bungeni na kutofanyiwa kitu, sasa inakuwaje kuwa eti Slaa amesema uongo? Hii hoja nayo pia ni NONESENSE, waliotuhumiwa kwa nini wasiende mahakamani kama wanaamini kuwa Dr. Slaa ni muongo?

5.
Habari toka ndani ya chama cha CHADEMA zinasema kuwa ingawaje kwa juu juu MBOWE na ZITTO KABWE wanaonekana kufurahia umaarufu wa Dr. SLAA lakini wote hao wawili kwa sababu zao tofauti wameelezwa kuumia sana kwani wanaona Dr. SLAA anawapiku umaarufu wa kisiasa na kwamba huenda akaamua kugombea urais mwaka 2010 kwa tiketi ya CHADEMA. Mhe. MBOWE na ZITTO KABWE wameapa kummaliza kabla hajafika mbali. Ati MBOWE anaona Ikulu inamwita na njia ni nyeupe lakini sasa anaibuka mtu anaitwa SLAA anataka kumnyang'nya kilicho chake!

Hii kwenye taifa haituhusu, lakini logically haiwezi ku-stand, Zitto, hatakuwa na umri wa kutosha ku-full fill katiba yetu kuwa mgombea urais by 2010, Freeman, kama hii hadithi ni kweli basi alipaswa kuwa na tatizo na Ndesamburo kwanza kwenye ile ishu ya Sitta na Malima, Dr. Slaa hakuitoa hii ishu ya mafisadi peke yake, hawa watatu wamekuwa wakifanya kazi kwa pamoja na kuzunguka pamoja, kama Freeman alitaka kummaliza Slaa, njia ilikuwa ni rahisi sana yaani yeye kubana kule Hull, UK akisingizia shule, lakini that has not beeen the case, Dr. Slaa asingeweza kusimama peke yake, na ndio maana hakuitoa bungeni hii ishu, akashauriwa kuitoa kwenye public kwa kukitumia chama kizima cha Chadema, kama kweli creators wa hii article wanaaamini, hii hoja ni kweli then wanashindwa nini kwenda mahakamani?

Hapa ukweli ni kinyume, CCM chama changu ndiyo chenye matatizo ya ndani baina ya makundi yake, ambayo ndio chanzo cha Dr. slaa, kama alivyokuwa Mzindakaya zamani, kupata evidence za ufisadi, this time Mzindakaya amejiunga pia na wafisadi baada ya kukatiwa mgawo wake kule BOT, kwa hiyo kundi moja la CCM wakaamua kumpatia Dr. Slaa hizo evidence, sasa evidence ni za moto kiasi kwamba CCM hatuwezi kutafutana uchawi kwa kuogopa kutolewa data zaidi na hilo kundi, kwa hiyo dawa ni ku-divide and rule upande wa pili, it won't happen maana mimi binafsi nilifahamishwa toka last week kuwa hii article inakuja, inatengenezwa mahali flani, watuhumiwa wajibu tuhuma za Slaa, Butiku amesema, Mwinyi amesema, mabalozi wa nje hapa bongo wamesema, hawa wote hawakuuona huo uongo wa Slaaa?

6.
Ni kwa msingi huo, sasa MBOWE na ZITTO wameamua kuanika madhambi ya Dr. SLAA ili wananchi wajionee kwani wanaamini madhambi yao wao hayajulikani maana wameshatumia mamilioni ya pesa kuyazika madhambi hayo. Ili kutimiza lengo lao wameamua kusambaza baadhi ya vioja vya Dr. SLAA. Hivi wanadai ni baadhi tu kwa vile orodha ni ndefu na wataitoa kwa awamu. Wameanza na nyepesinyepesi. Haya ndiyo wameyaanika kwa sasa:

MJUE DR SLAA

Mpaka sasa SLAA hana nyumba huko Karatu, badala yake hulala kwa rafiki yake ambaye inadaiwa ni shoga.

Absolutely, none ishu kwa taifa hata kama anlala na mbuzi leave alone shoga, unless huyo shoga ni mbunge naye pia au kiongozi wa taifa then yes, otherwise hakuna ishu hapo wala hoja! Kama ni nyuma mbona kina Sozigwa, marehemu Mnauye hawakuwa na nyumba, je iliwafanya wawe viongozi wabovu kwa kutokuwa na nyumba?

7.
Tangu mwaka 1977 hadi 1991, SLAA alikuwa Padre wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbulu. Aliachishwa Upadre baada ya kukosa uaminifu na kuendekeza tabia ya ufuska na wake za waumini. Hali hiyo ilimpelekea kupata watoto wawili wakati akiendelea kutoa huduma za kiroho. Watoto hao ni EMILIANA aliyezaliwa 18/06/1987 na LINUS aliyezaliwa 23/09/1988. Dr. SLAA alimuoa ROSE, mmoja wa waumini wake mwaka 1991 ndipo kanisa likamfukuza Upadri. Wakati huo ROSE alikuwa mchumba wa mweka hazina wa Kanisa ambaye miaka michache baadaye alikufa kutokana na mfadhaiko. Uchunguzi umeonesha kwamba, Dr. SLAA ni fuska aliyebobea, na anayo tabia ya kufanya mapenzi na wake wa marafiki zake hata baada ya kuoa. Kwa mfano Diwani wa Kata ya Baray wilayani Karatu LAZARO TITUS MASSAY (CHADEMA) aliwahi kupeleka malalamiko katika uongozi wa juu wa CHADEMA kuhusu tabia ya SLAA ya kufanya mapenzi na wake za watu wakiwemo hata wake za Madiwani Jimboni Karatu. Aidha, tarehe 01/11/2004, SLAA alifumaniwa na mkewe katika chumba kimojawapo cha Hotel 56 mjini Dodoma akiwa anafanya mapenzi na msichana aitwaye NJARI. SLAA aliruka dirishani bila nguo na wahudumu wa hoteli wakamsetiri kwa shuka na kumficha hadi mke wake alipoondoka kwa hasira kali baada ya kupambana na wizi・wake sawasawa - tukio hilo lilinaswa kwenye mkanda wa simu ya mkononi ya mhudumu na umehifadhiwa kwa matumizi katika wakati muafaka.

Haya yote hayajahusika na kumfanya aasifanye kazi yake ya ubunge wa upinzani, na kama ni ya kweli basi aendelee nayo maana yanaweza kuwa motivation kwake kuwataja viongozi mafisadi hadharani bila woga, hata Mungu kuna wakati alimtumia a prostitute kuwaficha watu wake wasihsikwe na maadui, huenda in our case Tanzania, tunahitaji kiongozi "Fuska" wa level ya Slaa kama madai haya ni ya kweli, kutuletea ukombozi, hiii nayo pia ni hoja hafifu sana, yangekuwa ya kweli wananchi wa jimbo lake wangeshamtoa siku nyingi sana!

8.
Dr. SLAA anasumbuliwa na ugonjwa mkubwa・ Amekuwa akienda kutibiwa mara kwa mara nchini Afrika Kusini. Mwezi Oktoba hadi Desemba, 2006, SLAA alilazwa katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam akitibwa gonjwa moja hatari sana
・

Viongozi wangapi wa CCM, wanaumwa ngoma jamani mbona nyani anajaribu kulicheka behind yake? Mpaka tuwatake majina? Mbona wanaongoza bila tatizo sasa tatizo liko wapi Slaa kuwa nao? Magic Johnson, mbna anazidi kuwa tajiri tu ndio kwanza amenunua Starbucks Coffee, kama kuwa na ngoma ni dhambi kiasi hiki kwa nini wanamuuzia? Hoja hafifu!


9.
Dr. SLAA amewahi kula mamilioni ya fedha za vilema ambazo zililetwa na wafadhili toka Ujerumani. Ushahidi upo kama atafanya ubishi.

Okay, Now this is a serious charge, Dr. Slaa anatakiwa kuijibu hoja hii kwa ushahidi lakini iwapo tu wale wanamtuhumu watatoa ushahidi kama yeye alivyoutoa wa mafisadi, ila so far haupo hakuna ushahidi zaidi ya hadithi tu! Kwa hiyo na yeye aijibu hii kihadithi hadithi tu kama ilivyotolewa, unless kuna more serious evidence!

10.
Alihongwa nyumba Ujerumani na hawara yake wa Kijerumani ambaye sasa ni marehemu na Dr. SLAA anategemea kuhamia huko. Inasemekana Dr. SLAA na hawara yake ambaye ni marehemu walishirikiana kumuua mume halali wa mama huyo aliyejulikana kwa jina la 全imbosh・

Kama kweli, basi ni ishu ya serikali ya ujerumani, na sio Tanzania au Chadema, again NONE-ISHU!

11.
Dr. SLAA alikuwa kachero wa Idara ya Usalama wa Taifa kama alivyo LYATONGA MREMA na alikuwa anaendelea kulipwa kiasi kikubwa cha fedha. Baadaye Idara hiyo nyeti iligundua fedha hizo anapeleka kwa hawara zake hivyo ikasitisha malipo hayo hali ambayo imemuudhi na akaanza kuipaka matope kwa kuituhumu na taarifa za kughushi anazodai amezipata. Vyanzo vya kuaminika vimebaini SLAA alipewa taarifa ya kughushi na akainunua kwa bei mbaya. Baada ya kubaini hivyo sasa anamsaka mbaya wake aliyemwingiza mjini.

Sijui kama aliwahi kuwa kweli agent au hapana, lakini kama alikuwa tatizo ni nini? Mbona Membe alikuwa agent na sasa ni waziri so what? Again NONE-ISHU! Wakati wa kugombea ubunge wa Karatu, kama CCM walijua hili kwa nini wasiseme kuwa Slaa ni mmuongo kwa kutosema kazi yake ya zamani? WHY now?

13.
Ujumbe huu ambao inaaminika MBOWE na ZITTO KABWE wanausambaza kwa kasi umemtia hofu Dr. SLAA kwani anajua yapo mengi yanayomhusu ambayo asingependa yajulikane. MBOWE na ZITTO wanaungwa mkono na chama cha CUF ambacho nacho kinadhani CHADEMA imekipiku katika umaarufu wa upinzani. Sera ni jino kwa jino.

JAMANI ATI HAWA NDIO WANATAKA KUCHUKUA
NCHI ・WATANZANIA TUTAFAKARI KWA MAKINI


Again kwenye hii where is an-ishu? in the whole thing kama kweli kuna ishu ya Slaa kuijibu, ni ile tu ya hela za vilema, lakini only kama kutakuwa na ushaidi zaidi ya hayo maneno tu ya mtaaani ambayo one time yalidai kuwa na Mengi naye pia alikula hela za vilema. Otherwise ningewashauri kina Slaa, waendelee na shughuli zao za kutuamsha wananchi na uozo unaoendelea ndani ya taifa letu, hii article isihusihwe kabisa na ushahidi ulitolewa na Dr. Slaaa, against mafisadi hazifanani kabisa,

Hapa ninapenda kuwaomba wale wananchi tulipo hapa forum, na ambao we are serious kuhusu mustakabali wa taifa letu, kuwa tukate hii ishu bila ya kulinganisha na orodha ya mafisadi, kwa sababu kama una akili timamu, hizi ni ishu mbili tofauti, hatuwezi kuangukia mtego wao walioiandika hii article, kutaka kulinganisha hii article na orodha ya mafisadi, not even close!

Hii nyepesi nyepesi imeandikwa na wepesi wepesi, ni nani hao? Ndugu zangu huuu uwanja sasa ni mkubwa mno kukoseshwa usingizi na this kind of article, haina facts muhimu kwa taifa letu, Pure Nonesense, kama kuna hoja ni ya hela za vilema, lakini where are the evidence?

Wakuu tufikie mahali in the future inapoletwa article kama hii tuigomee kabisa kuijibu! Tunataka ishu muhimu kwa taifa sio good kwa maigizo huko vichochoroni! Hili taifa haliwezi kuongozwa kwa maigizo, eti wananchi waone maigizo waelewe kuwa serikali yao inasema nini, THAT IS NONESENSE, maana it was os horrible hata wananchi walalhoi walishindwa kuelewa the message kwenye maigizo, lakini thank God kwamba wananchi hawa walalahoi hawakuhitaji maigizo kulelewa mkatba wa Buzwagi kuwa ni wizi wa mchana, na kwamba orodha ya mafisadi ina serious evidence, ndio maana wakawazomea viongozi wetu wa taifa, maana hawkuhitaji maigizo kuelewa kuwa kwenye mkataba wa Buzwagi, wameibiwa!

Mungu Ibariki Bongo!
 
mnyika acha zako, unadhani nani atasoma maneno yote hayo bana, ungesamalaizi tu ! unaona sasa mie naskia kizunguzungu !
 
Mnyika ume-interfere flow yetu ya mjadala, Mara kuna Hotuba za Kikwete I wish ujumbe wako ungeugawanya na kuweka kwenye thread tofauti!!! well, tushapata majibu kutoka kwa Zitto tunakushukuru...
 
Mnyika,
Mara nyingi lundo la maneno si kuwin political battles.....watu wengi hawawezi kusoma na kuelewa maneno mengi namna hiyo. Wenzetu huwa wanakitu wanakiita "sound bites." Maneno machache lakini moja kwa moja kwenye point, yaani hata wakina 'Joe Somebody' wanakuwa hawapati tabu kuingia kundini.Hata hivyo asante sana kwa majibu yako.
 
Pengine mimi ndio nilikosea niliwaomba watuhumiwa ambao ni member wa kijiwe chetu waje wajibu tuhuma. Sorry guys naona wengi hatupendi kusoma insha. Natumaini Mnyika atalichukulia hilo positively.
 
This thread is likely wasting our time. Nashukuru Mnyika Umejibu mambo mengi na ya msingi. Admin tumia busara yako, hii thread ina hujumu muda wa kujadiliana masuala muhimu na hili si moja wapo.
Waziri wa Ujenzi wakati wa Awamu ya pili Mzee Kiula si Alifumaniwa? lakini si tuliona ni masuala yake binafsi. Yesu aliwaambia wayahudi wale waliomleta mwanamke mzinzi kwake kwamba asiye na dhambi (pengine ya ngono) awe wa kwanza kurusha jiwe dhidi ya mwanamke yule. sote tunajua yaliyotokea.

mimi hapa ninao vimada, pengine na wewe pia unao, but this is real personal, let us focus on sensitive issues. tusiingie mtegoni nasi tukategeka.

Watu wawili watatu wanaoshabikia hili jambo wasiteke akili na mawazo yetu ku concentrate kwenye hii thread na kuacha thread za maana. tunarudi nyuma badala ya kusonga mbele. haya ni maoni yangu.
 
Kada, Kili, YniM, DUA and all:

My apologies, the message had provoked me much to the extent that I over responded.

I have taken it very positively.

Tuendelee kumkoma nyani.

JJ
 
tumepoteza muda sana ingekuwa ijumaa siyo tatizo. Naona hii baada ya kushinda hapa kwa zaidi ya masaa kumi na mbili iende udaku au vibweka vya wakubwa ili anayetaka kuendelea kuichangia achangie.. JF is bigger than these non issues..
 
Kada, Kili, YniM, DUA and all:

My apologies, the message had provoked me much to the extent that I over responded.

I have taken it very positively.

Tuendelee kumkoma nyani.

JJ

Mnyika,

Wala hujakosea kutoa maelezo yote hayo uliyoyatoa. Hii inaonyesha ukomavu wa kisiasa na uwezo wa kuface baraza kama hili kwa hoja. Majibu yako na ya Zitto yatasaidia wale waliokuwa wakipiga kelele kuwa CHADEMA waje kujibu hapa.

Waliotoa udaku wametoa, na viongozi wa CHADEMA wameeleza kuwa hakuna ugomvi ndani ya CHADEMA. Ulichofanya kwa mtizamo wangu ni sahihi kabisaaaaa.

Baada ya haya majibu nadhani ni wakati mwafaka sasa tukarudi kwenye hatari inayonikaribia taifa letu. Mfumuko wa bei, hali ngumu ya maisha, uuzwaji wa nchi, mikataba mibovu, ziara za nchi zenye kutumbua mamilioni ya pesa, nk!

Wenye kupenda udaku kama kawaida yao wataendelea maana sio kuwa wameanza leo kufanya hili.

Asante sana Mnyika kwa kazi yako kwa taifa letu changa. Nchi inataka watu kama wewe.
 
tumepoteza muda sana ingekuwa ijumaa siyo tatizo. Naona hii baada ya kushinda hapa kwa zaidi ya masaa kumi na mbili iende udaku au vibweka vya wakubwa ili anayetaka kuendelea kuichangia achangie.. JF is bigger than these non issues..

Mwanakijiji hata mimi nilishauri hivyo zamani sana ila sikusikilizwa. Udaku ni udaku na utazidi kuwepo tu kila siku. Wanaoumia ni mama wajawazito vijijini wanaokosa vifaa bora vya kujifungulia wakati viongozi wetu wakitumbua mabilioni ya pesa.
 
Kada, Kili, YniM, DUA and all:

My apologies, the message had provoked me much to the extent that I over responded.

I have taken it very positively.

Tuendelee kumkoma nyani.

JJ

Asante sana muheshimiwa.
 
JF inaelekea pa ovyo kwa mtindo huu! Mtu anaingia na upupu bin pumba, wakuuu wanajikunja kuujadili!!Hii inawavuta wengi wenyewe kupenda kupiga Udaku tu...mmmh hatutapata cha maana. Niliposoma tu hiyo habari nilitamni niifute lakini ndo hivyo.
Waheshimiwa maneno ya ovyo tusiyape nafasi...Administrator saidia pia.
 
Mnyika
Usiniembie aliyeandika huu upumbavu ni EN yeye ndiye mjinga mjinga anayeongoza kundi la wapumbavu.
 
Oops.. na yeye huwa akiona jina lake tu hushtuka. so I stand corrected.. namzungumzia Nyani wa mtini siyo Ngabu.. !

...oo..hohohohoh..hohoho...
...kweli bwana nilipoona "nyani" nikastuka kidogo
...lakini sasa mapigo ya moyo yamerudia hali yake ya kawaida

Mwafrika...msalimie sisteri...
 
Mkuu Admin,

Tafadhali sana hii ifutwe kabisaaa, hapa sio mahali pake, maana haina faida yoyote kwa taifa letu, mengine uwe unayazima huko huko pembeni kabla hayajafikishwa hapa,

I mean how low can we go, yaani sasa tumewapa mafisadi karibu siku nzima ya kupumzika na mawe, hiii iondolewe tuendelee na kumkoma nyani hapa!

Hii haina faid yoyote kwa taifa, hebu turudi kwa kina Butiku na Mwinyi, na waliyoyasema majuzi!
 
Mkuu Admin,

Tafadhali sana hii ifutwe kabisaaa, hapa sio mahali pake, maana haina faida yoyote kwa taifa letu, mengine uwe unayazima huko huko pembeni kabla hayajafikishwa hapa,

I mean how low can we go, yaani sasa tumewapa mafisadi karibu siku nzima ya kupumzika na mawe, hiii iondolewe tuendelee na kumkoma nyani hapa!

Hii haina faid yoyote kwa taifa, hebu turudi kwa kina Butiku na Mwinyi, na waliyoyasema majuzi!

Naunga mkono ila isifutwe kabisa story ina utamu wake ipelekwe kwenye udaku.
 
Watanzania wenzangu,
Nadhani wengi wetu hapa tunakubaliana kwamba thread hii na content ya hiyo e-mail inayojadiliwa ina lengo moja tu nalo ni kumpaka matope Dr. Slaa na kumharibia jina. Sababu ya jitihada hizo za kumpaka matope zipo wazi na zinajulikana kwa wengi. Hivyo basi, kwa vile wengi wetu tunakubaliana kwamba yaliyosemwa kwenye e-mail hiyo si ya msingi na kwamba ni ya udaku, tunapoendelea kuyajadili tunakuwa tunayapa umuhimu usiostahili. Inavyoelekea mabwana tovuti nao wameyapuuza maombi ya kuhamishiwa kule kunakostahili (udaku na vibweka vya wakubwa). Hivyo basi ombi langu kwenu wana Jambo kama kweli mnakubaliana nami kuwa huu ni udaku, acheni hili bandiko langu ndio liwe la mwisho kuhusiana na hii topiki. Mkifanya hivyo tu mtakuwa mmeuua mjadala bila hata ya msaada wa mabwana tovuti. Nasubiri ushirikiano wenu na natanguliza shukurani zangu. Akhsanteni.
 
Back
Top Bottom