Uzi wa vyakula tu

60580678.jpg
1605806751.jpg
 
Ukiendelea kuniita mpishi hodari utashangaa siku na mie naanza kujiita hivyo

we unga ulikuwa mgumu kiasi gani mpaka yawe magumu hivyo?? Next time embu jaribu kukanda unga ambao ukibonyeza unabonyea kirahisi. Alafu weka hamira ya kutosha & acha uumuke vizuri.

Hizo mbwembwe za butter mie huwa sifanya maana sipendi vitu vingi vingi. So huwa naweka Unga, Hamira, Mafuta kidogo, Chumvi kidogo na Sukari. That's it!!!!
Tutakuja na zoezi la kitumbua
 
Hazard CFC poleni sana Embu siku nyingine jaribuni kwa kuweka simple ingredients tu (Unga/Hamira/Mafuta/Sukari/Chumvi/Maji) alafu muone itakuwaje.

Mkikanda unga usiwe mgumu sana na pia muache uumuke kabisa!! Yani kama ukikanda unakuwa nusu kwenye chombo....uache uumuke mpaka ujae kwenye chombo ndio zoezi la kukaanga lianze. Na ukitaka uumuke vizuri uweke sehemu yenye joto la wastani (mf. juani, pembeni ya jiko au hata kwenye oven ila hapa inabifi uwashe kidogo ipate joto alafu uzime ndo uweke unga wako).
Unga nusu kilo kipimo cha hamira unatakiwa iwe kiasi gani?? Nipe vipimo kwa kutumia kijiko cha chakula
 
Unga nusu kilo kipimo cha hamira unatakiwa iwe kiasi gani?? Nipe vipimo kwa kutumia kijiko cha chakula
Nahisi kile kipakti kimoja kinatosha maana mie unga wangu (makadirio lakini sio exact measurements) around 1kg huwa naweka pakti mbili kasoro/moja na nusu ya hamira.
 
Hazard CFC poleni sana Embu siku nyingine jaribuni kwa kuweka simple ingredients tu (Unga/Hamira/Mafuta/Sukari/Chumvi/Maji) alafu muone itakuwaje.

Mkikanda unga usiwe mgumu sana na pia muache uumuke kabisa!! Yani kama ukikanda unakuwa nusu kwenye chombo....uache uumuke mpaka ujae kwenye chombo ndio zoezi la kukaanga lianze. Na ukitaka uumuke vizuri uweke sehemu yenye joto la wastani (mf. juani, pembeni ya jiko au hata kwenye oven ila hapa inabifi uwashe kidogo ipate joto alafu uzime ndo uweke unga wako).
Bi mkubwa anakanda andazi anaandaa moto analichoma na linatoka zuri hatari,

Ukiumusha maandazi anakushangaa,

Nilijaribu kuiga kilichotokea sina hata mpango wa kupika mandazi karibuni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom