Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu

Duh!! Mungu anamuona lakini!

Amejitetea kiume sana

Makamu wa Rais Dr Mpango na DC mstaafu Dr Kihongosi watakuwa mashahidi wake muhimu kama katiba inaruhusu.

Rais mstaafu Mkapa aliwahi kupanda kizimbani kumtetea Prof Mahalu pale Kisutu!
KUNA KIFUNGU HUA KINATENGULIWA

mpango lazima afike mahakamani
 
Mkuu wa wilaya ya Ya Hai anatumwa na Raisi akafanye operation wilaya isio yake ya Arusha? Raisi Hana operative wakuu wa wilaya ya Arusha au mkuu wa mkoa wa Arusha hidden operative wa kufanya hiyo Operation?

Sabaya zigo lako Hilo uliwezaje kwenda kufanya military operation nje ya your judistriction? Hiyo Operation alitakiwa afanye Mama Mgwira au mkuu wa wilaya ya Arusha au polisi wilaya ya Arusha au mkoa etc etc but from Arusha.Raisi hawezi ishiwa operatives wa any mission Hana haja ya kutafuta mtu wa Hai kwenda Arusha!!!

Sabaya jambazi wewe kesi Hilo lako usisingizie Marehemu wewe hukujua kuwa Arusha sio eneo lako la judistriction? Kuwa wewe ni
mkuu wa wilaya ya hai? Ungekuwa huna area ya uteuzi utetezi wako unge matter. Lakini mmmmmm .una kesi ya kujibu
sasa mkuu kama umepewa amri na boss wako unaanzaje kukataa?
 
Baada ya maelezo Yake ndo amejua hajui
IMG_20210814_042643.jpg
 
Natabiri sabaya kuachiwa huru na atapangiwa kazi nyingine na mamlaka za uteuzi.
 
Wala sio ngumu, ni ngumu kwa wasio jua sheria na siasa.
Sabaya anaelekezwa kazi na wajibu wake ni kutii hiyo unaielewa?

Pili kwenye siasa laziwa wachache waumie ili kuokoa wengi( hii hainaga ushaidi) hata magufuli kama alimtuma ilikuwa ni kukamilisha matakwa fulani kwa manuafaa ya maendeleo.( means jpm angekuwa hai usingesikia kesi ya kijinga kama hii)

Wenye akili mbovu watasema jpm ni mbaya sio mbaya hata kidogo, hiyo ndo siasa lazima wachache waumie wengi tuokoke.ukipata nafasi ya kuwa rais nilichokwambia leo utakikumbuka.

Watu wengi hawatumii akili kuwaza sana sana wanatumia mihemuko na tumbo kuwaza.

Ni nchi gani iliyopata maendeleo bila watu wachache wanaokwamishwa maendeleo kuumia? Hiyo ni siri ya ndani wajinga hawawezi ilelewa

Kila utawala mnaouita mziri jua kuna watu wameumia ili mambo yaende. Tumia akili.

Tuachane na kesi ya sabaya coz huyo ni mtumishi kazi yake ni kufata amri.

Mfano mwingine
Mfano mimi leo ni kiongozi wa nchi kuna kundi la majambazi la vigogo ni ngumu kuwashugulikia je nafanya nini na mimi ndo mama/baba wa taifa?
Hapa ni kutumia akili za kuzalia na sio za darasani+ madaraka yangu.

Ninachoweza kufanya namchukua kiongozi wa hayo majambazi nampa cheo nampa amri staki kusikia chembechembe yeyote ya ujambazi je kazi unaitaka au hutaki? Nitafanya hivyo coz huyo niliempa kazi si anajua wenzie staki kujua kafanya nini mimi nataka kusikia hakuna jambazi yeyote.

=Lazima watu wachache waumie tupate maendeleo.

=Ilimbidi yesu aumie ili tuokoke.

Kuwa raisi wa nchi ni kubeba misaraba yote kazima utumie akili mambo yaende.

Kwa mtu yeyote mwenye akili kuhusu sabaya hapo hakuna kesi ni kitu kama employer's liability.
Hata rais anajua sabaya hana kesi ila ni siasa tu hapa, dogo atazungushwa weeee watu waone serikali inafanya kazi kumbe hakuna kitu

Lakini kwa upande wa employer vipi? Je ni kosa? Kwa kutumia akili ni nusu kosa coz anakuwa hana chaguo..
Sijajua naongea na mtu mwenye uelewa kiasi gani, usipoelewa wewe wataelewa wengine.
Nimekuelewa vyema mkuu
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
 
Hii kesi haina tofauti na ya Prof. Mahalu naye wakati alipo shitakiwa alidai alitumwa na aliye kuwa Rais wa awamu ya 3 Mkapa, kweli Mkapa walikuja na kumtetea Mahalau na Mahalu aliachiwa huru.

Sabaya hana makosa kama alikuwa anatekeleza maelekezo ya aliye mteua, naamini kama Magufuli angekuwa hai angemtetea Sabaya bila kigugumizi, lkn pia kama Mama Anna Mgwira ange kuwa hai ange mtetea Sabaya bila kigugumizi. sijaona unyang'anyi uliotendwa!

mnyang'anyi angechukua receipts machine ya nn?!!
mnyang'anyi angepiga simu kituo cha polisi?!
huo ni unyang'anyi wa wapi?!
Kwanza magufuli angekuwa hai hii isingekuwa kesi, hata gavana akiitwa kumtetea lazima atamluka ili ccm ijisafishe na kadhia hii
 
Tatizo sio kuagizwa ni je ulifanya makosa wakati wa utekelezaji wa maagizo!? Kumbuka kesi ya Zombe. Mwenye kosa hubeba kosa sio alieagiza.
Ume saiti vema, pia ameagizwa kwa ushaidi gani au uko wapi, documented?, Umeagizwa Kama nani, eneo lake la kazi lipi, halikuwa na mipaka Kama ndiyo atoe uthibitisho, maana yeye alikuwa wilaya ya hai akajitia mapembe kinyemela kuendesha ujambazi kwa uroho wa kutajirika
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
Hayo maagizo yako wapi, achaneni na muhuni kapatikana
 
Hujawahi kufanya kazi hata kwenye taasisi ndogo? Hakunaga watu wanatumwa kazi maalum kutoka DSM kwenda Mwanza, Mwanza kwenda Mbeya, Mbeya kwenda Moro, Moro Kwenda Arusha, Dodoma kwenda Babati? Huko kote kunawaga hakuna wanaojua hiyo kazi?
Hilo ni genge la mafia, wamepatikana
 
Na kama hayakuwa halali kisheria hao walioyatoa walikuwa na haki kuyatoa? Na kama hawakuwa na haki kuyatoa kwa nini hawapo selo na mahakaman hadi sasa?
Hawapo mahakamani hadi sasa kwa kesi ipi?! Kama mnadhani na wenyewe wanatakiwa kuunganishwa kwenye kesi, basi ni wajibu wa Sabaya kutoa uthibitisho wa hayo maagizo ambayo yalikuwa haramu, vinginevyo, ataonekana ni mfa maji tu!!!
Mzee ukipewa maagizo si unapewa na vitendea kazi vya kutekeleza hayo maagizo!!
Hizo nyaraka ni vitendea kazi au terms of reference kwa ajili ya kutekeleza maagizo.
Hivi unatarajia kabisa official documents zitatoa maagizo yasiyo halali?!

What I see, utakuta docs zimeandika maagizo kwa kufuata kanuni na sheria, lakini hapo hapo akapigiwa simu kupewa maagizo ya ziada yasiyofuata sheria!!! Na kwavile alitaka kumfurahisha mheshimiwa, ndipo si ajabu akafanya hadi in excess!!
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
Kama yalikuwa ni maagizo halali, basi alilazimika kutayetekeleza, lakini kama hayakuwa halali, kutotekeleza haiwezi kuwa insubordination!

HOWEVER, ili "kuheshimu" mamlaka, tena mamlaka yenyewe ya Kiafrika, ingekuwa ngumu kwake kusema HAPANA lakini alitakiwa kujihuduhulu ili kupisha wengine ambao wangekuwa tayari kufanya mambo yaliyo kinyume cha sheria!
 
Hawapo mahakamani hadi sasa kwa kesi ipi?! Kama mnadhani na wenyewe wanatakiwa kuunganishwa kwenye kesi, basi ni wajibu wa Sabaya kutoa uthibitisho wa hayo maagizo ambayo yalikuwa haramu, vinginevyo, ataonekana ni mfa maji tu!!!

Hivi unatarajia kabisa official documents zitatoa maagizo yasiyo halali?!

What I see, utakuta docs zimeandika maagizo kwa kufuata kanuni na sheria, lakini hapo hapo akapigiwa simu kupewa maagizo ya ziada yasiyofuata sheria!!! Na kwavile alitaka kumfurahisha mheshimiwa, ndipo si ajabu akafanya hadi in excess!!
Uthibitisho atatoa tu.
Kwa hiyo kama alipewa maagizo ya ziada yasiyo fuata sheria si ndo maana tunasema wote mtoaji na mpokeaji ni vululuvululu!!
Halafu Sasa cha kujiuliza kama saa mbaya mmoja anakiri alipewa maelekezo yasiyofuata sheria kuwa akaumize watanzania jiulize ni wangap wamepewa maelekezo ya hivyo na ni watanzania wangapi wameumizwa na dikteta? Mkiona watanzania tunalilia katiba mpya ndo mjue twalia kwa mengi.....TUNATAKA KATIBA MPYA
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
Achilia mbali insurbonation kwanza; Kijana mdogo Jiwe akupe ukuu wa wilaya halafu akuagize jambo eti umjibu vyokovyoko utakuwa unajipenda wewe!!! Majaajii wenyewe na supika waliufyata ije iwe DC?!!! Kwanza simu yake tu ukioona kabla hata hajazangumza si ushajikojolea na kujihar?!!
 
Unapotumwa kufanya uhalifu na boss wako.. na ukafanya Huku ukijua ni kosa utafungwa..hata kama aliyekutuma ni rais..Sheria ni msumeno na hakuna aliye juu ya Sheria nchi hii ...
 
Back
Top Bottom