Nimekuwa nikimheshimu sana
Molemo humu Jf na nikiamini ni mpiganaji mahiri wa CDM. Hata hivyo, the way alivyojenga chuki binafsi dhidi ya
Zitto na mbaya zaidi anaziexpress hadharani, kwa sasa namuona kama pandikizi hatari sana kwa chama.
Molemo kwa makusudi kabisa amepotosha hii habari, kwa mfano anamlisha Mtei maneno kama vile kusema Zitto amekuwa mkaidi na hasikii. Ukiisoma stori, maneno hayo hayajatamkwa na Mtei. Kwenye kipengele cha Zitto kutaka katiba isimzuie mtu kugombea kwa umri, mzee Mtei ametumia neno "itaonekana" mbinafsi. Molemo akabadilisha na kusema "atakuwa" mbinafsi na mwenye uroho wa madaraka!!!
Naombeni nyie vijana wa CDM hapo makao makuu mtuambie kama chama chetu kina makundi, na nyie mnafuata kundi gani. Sisi tunatambua CDM hakuna makundi, tunawakubali viongozi wetu sawa, na binafsi naamini kati za Slaa, Mbowe na Zitto, yeyote akiwa raisi, nchi itakuwa imepata kiongozi bora. Acheni kutufarakanisha na Zitto...