Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Urais 2015: Mtei amshukia Zitto

Hakuna haja ya kumfukuza Zitto ndani ya Chama abaki tu dawa ni kumpuuza na kumpotezea CDM ni chama kikubwa zitto ni sisimizi tu ndani ya cdm msikilizeni then mmuache akichoka atakaa kimya dogo ni mpenda sifa sana.
 
Mkuu Molemo, alichofanya ZZK sio kutangaza kugombea urais kupitia Chadema, bali kutangaza nia ya kuiomba Chadema kumpitisha kama mgombea wa Chadema 2015!. Naomba sana utofautishe kati ya "kutangaza nia" na "kutangaza kugombea"!.

ZZK alipotangaza nia, mimi nilimuunga mkono na kutangaza nia ni jambo jema na jambo la kheri na nikatoa wito kabisa kuwa kila mwenye nia na aitangaze!, hivi kuna ubaya gani?. Hebu kanisome hapa Urais 2015 tusimlaumu Zitto; Nani anaujua Msimamo wa Dr. Slaa ...

Lakini ZZK alipojitangaza rasmi kuwa hagombei tena ubunge na badala yake "atagombea urais kupitia Chadema" nilimpinga!. Nilimwambia wazi, that was wrong!, hakupaswa kujitangazwa, bali alipaswa tuu kuonyesha vitendo vya ki presidential candidate ndani ya chama, ili wenzake ndio wamuone na kumuomba agombee na sio kujipigia debe na hapa nilimtahadharisha Urais wa ZZK 2015: Ngoma Ikivuma Sana...!. Wenye uwezo wa kumtangaza mgombea ni Chama na sio mwan achama individual!.

Ila lazima mkubali, mkatae, ndani ya Chadema kuna double standards za hali ya juu!, kuna baadhi ya mambo yakifanywa na kina fulani ni halali, ila wakifanya kina fulani inageuka ningwa!.

Tatizo ni kuwa ndani ya mioyo ya wana Chadema wengi, wanaye mgombea wao mioyoni mwao, sio tuu kuwa mgombea huyo anakubalika sana kwao, bali anaabudiwa!. Kitendo cha ZZK kujitokeza anaonekana kama kumkufuru huyo mungu mtu anaye abudiwa!. Na kwa wasio jua, mimi naujua msimamo wa huyo mgombea wenu kipenzi kuhusu kugombea au kutogombea urais na usome hapa Msimamo wa Dr. Slaa Kwenye Urais 2015 ...

Unashauri kamati kuu itoe miongozo, hivi kumbe Chadema haina demokrasia ya kila mwanachama yoyote kugombea nafasi yoyote ni mpaka kamati kuu itoe miongozo!.

Tena kwa vile ZZK ni rafiki yangu, na kabla hata ya huo urais kuna uchaguzi wa viongozi wa Chadema, nitamshauri agombee tena Uenyekiti na this time hakuna kujitoa mpaka kieleweke!.

Hivi nyinyi wapenzi wa Chadema, bado hamjajua ZZK ndio mtaji wenu pekee wa ushindi 2015?. Jee mnajua CCM itamsimamisha Membe?, sasa kwa vile huyo mgombea kipenzi wetu na Membe hawana tofauti katiuka zile kampeni za "kivile", na hamjajua kwa mujibu wa katiba mpya, ili chama kishinde urais wa JMT, lazima kipate angalau theluthi moja ya kura za Visiwani!, hivi huyo mgombea wenu kipenzi, kwa siasa zetu "zile", hizo theluthi ya kura kutoka visiwani zinatokea wapi?!.

ZZK anakubalika sana kutokana na kuendesha "strategic politics" kwa urafiki wake na January Makamba, atazivuna kura zote za vijana wa CCM!, kwa urafiki wake na Jussa, atazivuna kura zote za CUF kule visiwani. Kwa usomi wake, atazivuna kura zote za vijana/wasomi na wataka badiliko ya kweli with clear goals na right strategies!.

Nashauri, baada ya Mzee Mtei kukikabidhi chama kwenye "safe hands" za mkwewe, his advisory role yake ibaki limited kwa insiders tuu wa chama na sio ku express his public opinion publically as if chama bado ni chake!. Heshima yake kama muasisi ipo pale pale, lakini kwa sasa chama sio chake tena, sasa chama ni cha wanachama!, tena Mwenyekiti Mbowe anatakiwa kujipambanua kabisa kwa hili kuwa "amekata kabisa zile mothers apron strings" ili isje onekana kina Mzee Edwin Mtei ndio bado wanaendesha chama by proxy kupitia kwa wakwe zao!.

Ili chadema kuonysha ina "practice what it preach" lazima iache democracy i prevail!.
Go ZZK Go!.

Pasco.

Kwenye RED, Naona ni namna tu ya kuremba lugha ili uonekane una maana mbili tofauti lakini kitu ni kilekile tu kuvuruga hali ya hewa ya chama chake. Suala linaloleta ukakasi kwa ZZK si hayo maneno unayoyaandika hapo, bali ukweli ulio wazi kuwa kwa mujibu wa Katiba ya sasa na umri alionao Zitto hana sifa ya hicho anachokililia sasa. Sasa watu wanajiuliza inakuaje mtu anajua kabisa Katiba ya sasa haimruhusu kugombea Urais leo atangaze kutogombea ubunge na badala yeke atagombea urais? Kinachoshangaza zaidi kila baada ya miezi mitatu lazima aibuke na ndoto yake hii isiyo na uhalisia kwa mujibu wa katiba ya sasa.

Zitto anaweza kuwa analenga katiba mpya inayotarajiwa kwamba itashusha umri wa kugombea, swali ni je amejuaje kuwa umri utashushwa? Itakuaje kama umri uliopo sasa wa miaka 40 wananchi wakataka uwe miaka 45? Hizi kelele anazoibuka nazo ZZK kila wakati zitakuwa na maana au impact gani kwake na zaidi kwa chama chake?
 
Hivi kwa nini TOP BRASS ya CDM inaogopaga KIVULI cha ZZK, yaani Megacalories wanazo zitumia kumu-contain Zuberi si bure; ukiangalia kwa makini modus operand ya TOP BRASS hiyo mtu unahanza kuhoji kama wako sincere na transparent katika Uongozi wao.

Siwasemi vibaya lakini ukifanya analysis za events/incidents zilizo wahi kutokea huko nyuma mtu unakuwa na wasi wasi kwamba chama hiki inner circle imekaa kifamilia/kiukoo zaidi kuliko kuwa a public DOMAIN, hii ndio maana wakiona member fulani anakuwa popular kuliko wao - basi wanatafuta kila njia kujifanya eti wanampa ushauri asubiri kwanza, sijuhi umri bado - wanatumia kisingizio hicho kuwakingia kifua jamaa zao, yaani inapokuja katika suala hilo member yeyote anayejaribu ku-challenge cocoon hiyo anaonrekana expendable kwao regardless ya umaharufu wake. I stand to be corrected.
 
Jamani mtu kutangaza nia kupitia chama chake na yuko tayari kupokea matokeo yoyote wakati utakapofika tatizo liko wapi.Huyu mzee ana matatizo ya akili akapimwe mwendekeza udini sana
 
Kwenye RED, Naona ni namna tu ya kuremba lugha ili uonekane una maana mbili tofauti lakini kitu ni kilekile tu kuvuruga hali ya hewa ya chama chake. Suala linaloleta ukakasi kwa ZZK si hayo maneno unayoyaandika hapo, bali ukweli ulio wazi kuwa kwa mujibu wa Katiba ya sasa na umri alionao Zitto hana sifa ya hicho anachokililia sasa. Sasa watu wanajiuliza inakuaje mtu anajua kabisa Katiba ya sasa haimruhusu kugombea Urais leo atangaze kutogombea ubunge na badala yeke atagombea urais? Kinachoshangaza zaidi kila baada ya miezi mitatu lazima aibuke na ndoto yake hii isiyo na uhalisia kwa mujibu wa katiba ya sasa.

Zitto anaweza kuwa analenga katiba mpya inayotarajiwa kwamba itashusha umri wa kugombea, swali ni je amejuaje kuwa umri utashushwa? Itakuaje kama umri uliopo sasa wa miaka 40 wananchi wakataka uwe miaka 45? Hizi kelele anazoibuka nazo ZZK kila wakati zitakuwa na maana au impact gani kwake na zaidi kwa chama chake?

Mkuu umenena.Mimi ni kijana wa miaka chini ya 35 lakini tayari nimepeleka maoni kwenye tume ya Warioba kwamba umri wa kugombea Urais uanzie miaka 45 na hii ni kwa sababu ninaogopa kuja kuongozwa siku moja na mwendawazimu lakini akashinda tu kwa kigezo cha ujana.
 
Tunahitaji Katiba Mpya ambayo itaruhusu mgombea binafsi. Haingii akilini kwa chama chenye wanachama milioni tano au sita kikaongoza watanzania zaidi ya milioni arobaini ambao hawana vyama! Kipengele hiki kikiwepo,malumbano yote hayatakuwepo na hizo kambi zao.
 
Zitto akiona picha za mr dhaifu akiwa Canada akivutwa na vitoroli kupitia farasi naona ndio anachanganyikiwa kabisa kwa tamaa anataka hata kubadilisha birth certificate yake ili isome miaka 42 afikapo 2015

Kwa mtazamo wangu wa sasa (maana hapo mwanzoni Zito nilimwona tofauti (mtu makini)) namwona Zito ni dhaifu. Anafuata hisia zilezile za kupendwa kwa sura na kwa haraka haraka anaonyesha nia ya kuwa rais. Ajue kwamba watanzania wanateseka sasa hivi kwa dhambi yao ya kupenda ghafla na pasipo mashiko. Namshauri atulie aendelee kuonyesha vipawa vyake na jamii itamhukumu (itaamua) kama anafaa. Ikulu sio mahali pa kukimbilia unahitaji kuwa na mzigo juu ya watanzania.
 
sasa nimeamini ni kweli kabisa tumbo linaponza tigo! pole sana kaka zz!
 
Hivi kwa nini TOP BRASS ya CDM inaogopaga KIVULI cha ZZK, yaani Megacalories wanazo zitumia kumu-contain Zuberi si bure; ukiangalia kwa makini modus operand ya TOP BRASS hiyo mtu unahanza kuhoji kama wako sincere na transparent katika Uongozi wao.

Siwasemi vibaya lakini ukifanya analysis za events/incidents zilizo wahi kutokea hapo nyuma mtu unakuwa na wasi wasi kwamba chama hiki inner circle imekaa kifamilia/kiukoo zaidi kuliko kuwa a public DOMAIN, hii ndio maana wakiona member fulani anakuwa popular kuliko wao - basi wanatafuta kila njia kujifanya eti wanampa ushauri asubiri kwanza, sijuhi umri bado - wanatumia kisingizio hicho kuwakingia kifua jamaa zao, yaani inapokuja katika suala hilo member yeyote anayejaribu ku-challenge cocoon hiyo anaonrekana expendable kwao regardless ya umaharufu wake. I stand to be corrected.

Wewe Magamba utaandika kipi tofauti na ulichoandika?
 
mtei ni wa kupuuzwa,
huyu si ndo aliehoji mbona waislam wengi kwenye tume ya katiba?
Si ndio aliesema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemjua wakati zkk alipotaka kugombea uenyekiti wa chama?
Hana busara hata kidogo huyo mzee, anamtetea mkwe wake.
 
ungejibu hoja zao mkuu, sio kuwaita ccm.
Huko ni kukimbia hoja.

Zkk alisema atakiomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea, na akasema kisipompitisha atampigia kampeni mgombea yeyote atakae pitishwa na chama.
Sasa tatizo liko wapi?

Na kama mtei anakipenda kweli chama na hataki malumbano, kwanini anaongea hayo kwenye media na asimuite zito au ashauri chama kiitishe kikao kujadili hilo swala?

Kama tatizo umri, sio zito pekee anaepinga huu umri, vijana wengi hatuutaki na tunataka katiba mpya iupunguze.
Ikumbukwe Wastan wa maisha ya mtanzania ni miaka 45.

Mkuu pole sana naona wewe ni new comer hapa JF 2011 inawezekana huwajui hawa jamaa
siku zote ni supporter was CCM leo ndo wamekuwa supporter wa Zitto?

Ukijibu hoja zao ni kama umeingia choo cha kike

Copy to Ritz, Pasco, chama, Ecoli, Kata nyodo, OTIS
 
Last edited by a moderator:
Mkuu chama,
Makundi kutoka Kaskazini kamwe hawawezi kuacha kupambana na Zitto, wakikaa kimya ni sawa kumuachia Nguruwe akuchomee mishikaki.

Zitto Kabwe, ana nguvu kubwa kutoka kwenye makundi ya vijana pamoja na wazee, sehemu kubwa ya Tanzania mikoa kama Dar es Saalam, Pwani, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Mwanza, Morogoro, Tanga, Bukoba, Mtwara, Lindi, Singida, Tabora, hawa wajumbe wote wa Chadema wapo upande wa Zitto Kabwe.

Sehemu za Kaskazini ni kweli Zitto hana nguvu zozote za kisiasa.

tabora gani hiyo ambayo Zitto ana wafuasi hao? Huku Tabora watu hatuna ushabiki bali tunachukia CCM na Ahadi hewa zake na tunaunga mkono CHADEMA na sio mtu.
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo Zitto kasema kabisa " Mzee Mtei kabla hajafa..." ?
 
mtei ni wa kupuuzwa,
huyu si ndo aliehoji mbona waislam wengi kwenye tume ya katiba?
Si ndio aliesema hawezi kuona cdm inaongozwa na mtu asiemjua wakati zkk alipotaka kugombea uenyekiti wa chama?
Hana busara hata kidogo huyo mzee, anamtetea mkwe wake.

Na wewe naona akili zako zile zile
Njaa inawasumbua mpaka sasa Nnauye Jr ajawapa mshiko wenu
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
Hivi kwa nini TOP BRASS ya CDM inaogopaga KIVULI cha ZZK, yaani Megacalories wanazo zitumia kumu-contain Zuberi si bure; ukiangalia kwa makini modus operand ya TOP BRASS hiyo mtu unahanza kuhoji kama wako sincere na transparent katika Uongozi wao.

Siwasemi vibaya lakini ukifanya analysis za events/incidents zilizo wahi kutokea hapo nyuma mtu unakuwa na wasi wasi kwamba chama hiki inner circle imekaa kifamilia/kiukoo zaidi kuliko kuwa a public DOMAIN, hii ndio maana wakiona member fulani anakuwa popular kuliko wao - basi wanatafuta kila njia kujifanya eti wanampa ushauri asubiri kwanza, sijuhi umri bado - wanatumia kisingizio hicho kuwakingia kifua jamaa zao, yaani inapokuja katika suala hilo member yeyote anayejaribu ku-challenge cocoon hiyo anaonrekana expendable kwao regardless ya umaharufu wake. I stand to be corrected.
Kumbe Dk Slaa na yeye ni ukoo wa kina MBOWE? mIMI NILIKUWA SIJUI!
 
Nasikitika sana Mzee Mtei kujitokeza kumjibu ZZK. Msimamo wa kumpuuza ulikuwa ni sahihi sana maana ni wazi kelele za kila baada ya miezi mitatu za Zitto juu ya kuutaka urais ni kama zinazopigwa kwenye vacuum maana umri wake kwa mujibu wa katiba haumruhusu kugombea hiyo nafasi mwaka 2015 na hata hiyo katiba anayotegemea kwamba itashusha chini huo umri hakuna uhakika wa hili unless otherwise kama ameshapiga ramli.
 
images
images
 
Mkuu chama,
Makundi kutoka Kaskazini kamwe hawawezi kuacha kupambana na Zitto, wakikaa kimya ni sawa kumuachia Nguruwe akuchomee mishikaki.

Zitto Kabwe, ana nguvu kubwa kutoka kwenye makundi ya vijana pamoja na wazee, sehemu kubwa ya Tanzania mikoa kama Dar es Saalam, Pwani, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Mwanza, Morogoro, Tanga, Bukoba, Mtwara, Lindi, Singida, Tabora, hawa wajumbe wote wa Chadema wapo upande wa Zitto Kabwe.

Sehemu za Kaskazini ni kweli Zitto hana nguvu zozote za kisiasa.

Zitto Zuberi Kabwe hana nguvu hiyo anayodhani (na unayodhani) anayo! Fanya utafiti utabaini vijana wanaotaka mabadiliko walishaachana na Zitto kitambo tangu enzi za utetezi wa Dowans. Hana umaarufu huo unaojaribu kuutengeneza hapa. Kwanza alishinda ubunge kwa mbinde. Umaarufu wake kule kijijini Kigoma umeporomoka kwa kasi ya ajabu. Pili, mvuto wake wa kisiasa umepungua mno. Hayupo kwenye orodha ya watu wanaoaminiwa katika jamii hivi sasa (pamoja na vijitihada vyake vya kukataa posho na kadhalika). Hana tofauti na Jakaya. Amefulia kisiasa.

Uthibitisho wa kufulia, ni hizi kauli zake tatanishi wakati huu ambao wenzake wanahamasisha mabadiliko vijijini, yeye anahamasisha migogoro ya fikra (kuhusu vyeo) as if hilo ndilo jambo la msingi mwaka huu.

Kama kweli ana nia ya kugombea Urais, ni bora angefanya kazi ya ziada KUREJESHA IMANI ya wananchi kwake! Kwa sasa haaminiki! Na sijui kama hajui hilo. Watu wanamwona kama mtu MVURUGAJI, mtu ASIYEELEWEKA, kichwa ngumu, mpenda SIFA BINAFSI na Fisadi anayechipukia (rejea mkanganyiko wake kwa Dowans, Tanesco nk). Badala ya kupoteza muda wake na matangazo ya Urais, ni bora angeshughulika KUREJESHA IMANI.

Hakika hana nguvu hiyo. Na leo akiamua kuondoka Chadema, athari yake ni ndogo kuliko anavyojifikiria yeye.
 
Last edited by a moderator:
Zitto Zuberi Kabwe hana nguvu hiyo anayodhani (na unayodhani) anayo! Fanya utafiti utabaini vijana wanaotaka mabadiliko walishaachana na Zitto kitambo tangu enzi za utetezi wa Dowans. Hana umaarufu huo unaojaribu kuutengeneza hapa. Kwanza alishinda ubunge kwa mbinde. Umaarufu wake kule kijijini Kigoma umeporomoka kwa kasi ya ajabu. Pili, mvuto wake wa kisiasa umepungua mno. Hayupo kwenye orodha ya watu wanaoaminiwa katika jamii hivi sasa (pamoja na vijitihada vyake vya kukataa posho na kadhalika). Hana tofauti na Jakaya. Amefulia kisiasa.

Uthibitisho wa kufulia, ni hizi kauli zake tatanishi wakati huu ambao wenzake wanahamasisha mabadiliko vijijini, yeye anahamasisha migogoro ya fikra (kuhusu vyeo) as if hilo ndilo jambo la msingi mwaka huu.

Kama kweli ana nia ya kugombea Urais, ni bora angefanya kazi ya ziada KUREJESHA IMANI ya wananchi kwake! Kwa sasa haaminiki! Na sijui kama hajui hilo. Watu wanamwona kama mtu MVURUGAJI, mtu ASIYEELEWEKA, kichwa ngumu, mpenda SIFA BINAFSI na Fisadi anayechipukia (rejea mkanganyiko wake kwa Dowans, Tanesco nk). Badala ya kupoteza muda wake na matangazo ya Urais, ni bora angeshughulika KUREJESHA IMANI.

Hakika hana nguvu hiyo. Na leo akiamua kuondoka Chadema, athari yake ni ndogo kuliko anavyojifikiria yeye.

Kafulila mwanzoni alijidanganya hivyo hivyo lakini siku ile Mbatia alivyomfukuza aliangua kilio kama mtu aliyefiwa na mama yake.
 
Back
Top Bottom