BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
UPDATE: Miili zaidi imefukuliwa katika Makaburi yanayohusishwa na 'ibada ya njaa', na kufanya jumla ya vifo kufikia 83, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka
-
Polisi wamekuwa wakizunguka msitu wa #Shakahola kwa takriban Siku 4 baada ya kupokea taarifa kuhusu dhehebu linaloongozwa na #PaulMackenzie Nthenge, ambaye aliwataka wafuasi wake kufa njaa ili kumtafuta Mungu

.............................................

Idadi ya maiti zilizotolewa katika msitu wa Shakahola zimeongezeka na kufikia 59, kufuatia kufukuliwa kwa miili kumi na nane kutoka kwenye makaburi 7 siku ya Jumapili, huku wapelelezi wakiwa bado hawajachimba zaidi ya makaburi 50 na idadi ya walio hai bado haijajulikana.

Familia za wanaotafuta ndugu zao waliotoweka kwa zaidi ya miaka 3 zimeitaka serikali kuweka mkazo zaidi katika kuwasaka wale ambao bado wamejificha ndani ya msitu wa Shakahola na hawataki kuokolewa wakati maafisa wa upelelezi wakiendelea kufukua makaburi mengine.




1682240365841.png

Uchunguzi wa tukio hilo umeanza Nchini Kenya ikiwa ni pamoja na kumkamata Mchungaji aliyewataka Waumini wa Kanisa la Good News International wasile chakula ili wafe kwasababu ndio njia pekee ya kufika Mbinguni.

Mapema Wiki hii, Polisi walifanikiwa kuwanusuru Waumini 15 wakiwa hai, Wanne kati yao walifariki njiani wakati wakipelekwa Hospitali na baada ya Uchunguzi zaidi wamebaini Makaburi 32 yanayodaiwa kuzikwa baadhi ya Waumini.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kituo cha Runinga cha NTV, Polisi imeeleza huenda uchunguzi unaoendelea ukafanikisha kupatikana Miili mingine zaidi kutoka katika Makaburi yaliyopo Malindi jirani na Msitu wa Shakahola.

====

Police began investigations amid reports that cult followers believed they would go to heaven if they starved to death.

Kenyan police have exhumed human remains from more than a dozen suspected graves in the east of the country amid an investigation into followers of a Christian cult who believed they would go to heaven if they starved themselves to death.

Police began exhuming bodies on Friday, said Charles Kamau, a detective in the town of Malindi near the Shakahola forest in Kilifi county, where police rescued 15 members of the Good News International Church last week, according to footage broadcast by Citizen TV.

Unnamed police sources told the AFP news agency on Saturday that 21 bodies had been found so far and that more could yet be uncovered.

“In total since yesterday, we have 21 bodies,” a police source told AFP on condition of anonymity, referring to exhumations in the Shakahola forest outside the coastal town of Malindi.

“We have not even scratched the surface which gives a clear indication that we are likely to get more bodies by the end of this exercise,” the source added. A second police source confirmed the same toll, also on condition of anonymity, AFP reported.

Kenya’s NTV channel reported on Saturday that seven bodies had been removed from two of 32 suspected gravesites marked out by police.

AL JAZEERA
 
View attachment 2597010
Uchunguzi wa tukio hilo umeanza Nchini Kenya ikiwa ni pamoja na kumkamata Mchungaji aliyewataka Waumini wa Kanisa la Good News International wasile chakula ili wafe kwasababu ndio njia pekee ya kufika Mbinguni.


AL JAZEERA
Ila kenya wana occults nyingi kwa mwamvuli wa ukristo. Halafu baba mchungaji bila shaka yeye hajafunga
 
Ila kuna wakati unawaza huyu baba mchungaji alikusudia nini!? Yaani alikuwa ananufaikaje na vifo vya hawa waumini wake!?? Halafu yeye baba mchungaji alikuwa hataki kwenda mbinguni? Maana yeye mpaka amekamatwa na police alikuwa hajafunga!
 
Inasikitisha sana, utapeli wa kidini umegharimu maisha ya watu wasio na hatia
 
Back
Top Bottom