Unatumia njia gani kuwasaidia ndugu na jamaa zako pale kipato chako kinapokuwa chini ya mahitaji yako ya muhimu?

Jamii zetu ni watu wa kupenda kusaidiwa sana wanapoona ndugu au jamaa anapokuwa na kipato cha uhakika lakini cha ajabu mbongo hana moyo wa kutoa msaada wala mazoea ya kutoa msaada hata chembe nilivyokuwa chuo nilishuhudia ndugu zangu wa karibu kabisa,jambo la msingi ni kuishi kama wazungu mzazi,wanao na mkeo akina dada,dogo kama amemaliza chuo,mjomba sijui nani huko wapambane na hali zao kama mimi sikupata msaada kwa mtu yoyote kwanini isiwe kwao.
 
Jamii zetu ni watu wa kupenda kusaidiwa sana wanapoona ndugu au jamaa anapokuwa na kipato cha uhakika lakini cha ajabu mbongo hana moyo wa kutoa msaada wala mazoea ya kutoa msaada hata chembe nilivyokuwa chuo nilishuhudia ndugu zangu wa karibu kabisa,jambo la msingi ni kuishi kama wazungu mzazi,wanao na mkeo akina dada,dogo kama amemaliza chuo,mjomba sijui nani huko wapambane na hali zao kama mimi sikupata msaada kwa mtu yoyote kwanini isiwe kwao.
Ha ha haa. Unyama unyama tu, au siyo? Kwa maoni yangu nadhani kama una nafsi ya kusaidia inakubidi usaidie tu bila kujali kama ulisaidiwa ama la. Lazima ujue ndani ya dhamiri yako kuwa kwanini inakubidi kusaidia na unalenga ku-achieve jambo gani katika maisha yako ili uishi kwa furaha. Kama moyo wako unafurahia kufanya jambo hilo ni vema ukafanya, kama haufurahii unaweza kuacha pia.
 
Kwa upande wangu naona ni vema kusaidia kwa uwezo wako ila si kila saa ili usigeuke tegemezi kwa asilimia 100.

Hili ni jambo ambalo nafanya kwa ndugu wote wanaoniomba pesa. Kuna mida nakupa yote. Kuna mida nakupa nusu. Kuna mida sikupi kabisa.

Nachanganya hivi ili nisije kujulikana kama mtu toatoa hela asiyejua kusema hapana katika ukoo/familia jambo ambalo nasikitika linaleta mzigo sana kwa wengi kwenye familia za kiafrika. Hivyo unakuta nikiingia katika mode ya NO inapita miezi sijatoa hela kwa ndugu labda tu pesa ambayo naitoaga automatically kwa mama kila mwezi kusaidia expenses zake.
 
Watu tupunguze kuomba omba pia waweza mwona mtu yuko safi kumbe naye ana budget zake Kali na mengineyo Mimi wakati nasoma nilikuwa Hadi najilipia ada kwa bumu langu na sikuwahi kusumbua mtu tena saa nyingine nilikuwa Nampa mwenye uhitaji, kuliko kuomba omba hela ni heri ubuni wazo uombe kamtaji uanze kujishughulisha hyo itaondoa umaskini
Manka kama Manka
 
Saidia wanaokusaidia mkuu,Chuma huliwa na chuma,dawa ya moto ni moto. Mimi ndugu hawajawahi kunisaidia,so kamwe sitowasaidia ila wahuni tu wa mitaani wamenisave sana kipindi nahangaika.

Ndio maana niko tayari nimsaidie mtu baki ila sio ndugu
 
Ningejua kama wewe ni mfuasi wa BIblia ningeweza kukuuliza hapo kwenye kutoa usizedi uwezo, vipi kuhusu kuhusu sadaka ya yule mama Mjane aliyetoa senti yake ya mwisho kabisa?
Mimi ni mfuasi wa upande mwingine.
 
Mtu anayekuwa DISAPPOINTED na NDUGU ZAKE NI HAJIELEWI. Hao ndio watakuuguza pamoja na UTAJIRI WAKO ndugu ndio msaada wako, hakuna mtu aliuguzwa na MARAFIKI ZAKE. Jitambue kama kijana, we've a lot to do in this world lkn kubwa WAPENDE NDUGU ZAKO. WAO NDIO WATAZOA MAVI YAKO WAKATI UKO HOI KITANDANI.
Ukisaidia ndugu umejisaidia wewe mwenyewe.
Umeongea kweli ila mkuu si kila ndugu wako ivyo.

Kuna watu wanasaidiwa na marafiki zao kuzidi hata hao ndugu.

Labda tuseme hivi, pale tunapoweza tusaidie bila kujali ni ndugu ama rafiki. Kila mtu katika maisha yetu ana mchango wake. Tuwape nafasi kwa kiasi . Tusije kuamini sana ndugu tukasahau marafiki. Imagine mtu unaishi Dar es Salaam na ndugu wako Kigoma itakuwaje siku umekwama , mgonjwa taabani utasaidiwa na nani????

Binafsi nawajali wote kadri ya uwezo wangu.!!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hili suala la " kusaidiana" lipo overrated Sana katika jamii za kiAfrika.Tatizo Ni pale unapojitoa kuwasaidia watu/ mtu fulani ukitegemea itafika siku fulani waanze kujisimamia na kujikimu wenyewe,kumbe wao Wala hawajistukii ila wanaendelea kukutegemea siku nenda siku Rudi.


Heshima kwenu Wakuu.

Nimebahatika kuishi Nchi za wenzetu kwa Mabeberu, kiasi fulani nimejifunza mambo kadhaa.

Sisi Wabongo tunaishi maisha ya ujamaa, yaani kugawana kidogo tunachokuwa nacho ili kila mtu apate japo mkate. Hali hii inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya sisi wabongo bado maisha yetu yapo chini sana hivyo idadi ya wategemezi kwenye familia zetu bado ni kubwa sana hivyo tunaishi kwa kutegemeana.

Hata hivyo, hali ni tofauti kwa wenzetu mabeberu. Nadhani hii inatokana na kuwa, wao kiwango cha ukosefu wa ajira ni kiasi kidogo sana, hivyo kila familia ina uwezo wa kujiingizia kipato chake na kumudu gharama za maisha. Jambo lingine ni kuwa, wenzetu hawana maisha ya kijamaa kiviile. Yaani ni yeye na familia yake full stop. Mnaweza kuwa mnaishi nyumba moja ila mkawa mnasalimiana tu hakuna stories zaidi ya hapo. Msamiati wa kukopana pesa sijauona, ukiwa na shida unaweza kuomba msaada kwenye serikali ya jimbo lako. Kwa nchi kama Sweden, serikali ya mahali unapoishi inaweza kugharamia gharama za kuishi kwa vijana wasiokuwa na ajira ama kupoteza ajira. Unaweza kupata pesa ya kujikimu na ukalipiwa rent. Hi ni kwa raia pekee. Siyo kama sie wakuja.

Nirudi kwenye mada sasa.

Vibwagizo kidogo


1. Nilipokuwa nasoma wakati flani, kutokana na maisha yetu ya uduni, nilikuwa nikiomba masaada kwa ndugu yangu (binamu) hapa na pale ili kukidhi mahitaji muhimu. Huyu binamu yangu, kwa maoni yangu, alikuwa na unafuu kidogo wa maisha kwa maana ya kuwa na ajira, nyumba yake na kiusafiri. Hivyo kwa kuwaza kwangu kipindi hicho nikajua atakuwa na maisha bora na ana mpunga wa kutosha. Chakushangaza, wakati mmoja nikamuomba msaada nilikuwa chuoni wakati boom limekata akawa amenitumia kiasi cha pesa kidogo sana kuliko nilivyotarajia. Niwe muwazi kuwa nilifadhaika, nikasema, yaani kweli binamu ananitumia elfu 10 tu kweli? na nimemweleza kuwa nina shida na sina kitu kabisa?

2. Huyohuyo binamu yangu, wakati nipo mdogo kwa shangazi yangu, nilikuwa nashangaa, iweje tunaishi maisha magumu pale home pengine pesa ya kula inakata na wakati yeye ana kazi huko Dar na anakula maisha? (mawazo yangu). Na pesa ilipokuwa inakata, binamu alikuwa hatumi pesa mpaka Shangazi apige simu na akipiga alikuwa anatuma kiasi kidogo sana. Kwakweli niliwaza sana nikajisemea kuwa kwanini watu waliofanikiwa kupata vijisenti hawatumi pesa kwa wazazi wao mpaka waambiwe? Ina maana hawajui wajibu wao?

3. Kumbe buana, yale yalikuwa nawazo ya utoto tu. Ukubwani sasa nimegundua kuwa Binamu yangu alikuwa ameajiriwa na pengine kipato chake kilikuwa cha kawaida sana na kutokana na majukumu ya familia yake na maisha ya mjini tena Dar, basi kipato chake si chochote kivile kumudu maisha na kutuma mapesa mengi kwao kama nilivyokuwa nawaza nikiwa mdogo.

4. Mawazo yangu hapo juu, yametokana na ukweli kuwa, pamoja na kipato changu kuongezeka karibia mara mbili ya kipato changu cha awali, nimegundua kuwa hata mie wazazi wangu sijawatosheleza kwa kuwasaidia mahitaji yao kwa kiwango cha kuridhisha sana. Yaani wanaishi maisha yenye unafuu kidogo ila bado wana ganga ganga tu. Pamoja na kujitahidi kutokuwa mbinafsi na kuishi maisha ya kawaida, bado naona kabisa hata msaada wangu wa kwa ndugu na jamaa bado ni kidogo sana pamoja na kipato changu kuongezeka kidogo. Najua huwezi kumfurahisha kila mtu na huwezi kuacha kulaumiwa, ila naamini wapo watu wanaoniona kama mtu niliyefanikiwa na nimeshindwa kuwasaidia. Kumbe bado naganga ganga tu.

Naomba nijielekeze kwenye hoja ya msingi baada ya vibwagizo hapo juu.
Naomba kulizungumzia kundi la wale ambao vipato vyao huweza kugharamia mahitaji ya msingi kama chakula, mavazi na kulipia kodi ya nyumba ama pengine anaishi kwenye nyumba yake. Kundi hili baadhi ya watu huliita kama middle class family. Kwa uchunguzi wangu, kundi hili lina mzigo mkubwa kwenye jamii maana jamii yetu hasa wale wanaotoka kwenye extended families na jamaa zao hawawezi kumudu mahitaji muhimu, hulitazama kundi hili kama kundi lenye unafuu kimaisha, hivyo hutegemea kupata msaada kutoka kwao. Hata hivyo, kutokana na kipato chao kulingana na matumizi, tena yale ya lazima tu, kiukweli kundi hili hujikuta kwenye changamoto kubwa kimaisha na kushindwa kukidhi matarajio ya jamaa zake na kuonekana kama mtu mbinafsi, hivyo hutupiwa lawama kwa kiasi kikubwa ilihali vipato vyao pengine vinatosheleza tu kula chakula na kulipia kodi ya nyumba.

Je, wewe kama kipato chako kina balance na matumizi yale ya lazima pekee, yaani chakula, mavazi na makazi. Huwa unatumia njia gani kusaidia ndugu na jamaa zako ambao wana maisha duni na wana matarajio makubwa kutoka kwako? Kumbuka nazungumzia mtu ambaye akipata kipato chake kinalingana na matumizi kwa mwezi husika na hawezi kufanya hata savings. Nyongeza, namzungumzia mtu ambaye si mbinafsi, ana moyo wa kuwasaidia wahitaji ila uwezo wake upo chini zaidi ya kile anachotakiwa kufanya katika jamii yake. Wahitaji wanaweza kuwa ndugu wa karibu wa tumbo moja, mabinamu, wajomba, mashangazi, baba mkubwa, mama mkubwa, rafiki wa karibu sana n.k.

1) Je, ni sahihi kukubali lawama kwa muda flani ili ubakie kwenye mapambano kwanza na usitoe msaada mpaka utoboe kwanza kufikia hatua ya kipato kuwa juu ya gharama za maisha? Natambua kuwa kadri kipato kinavyoongezeka mtu anaweza kuchagua maisha ya juu zaidi hivyo isifike siku ambapo atabakiza savings na kuwasaidia wahitaji, ila hapa nazungumzia wale ambao wana nia ya dhati ya kuwasaidia jamaa zao na pengine wangependa kuridhika na maisha waliyonayo hasa anapokuwa amefikia kwenye lifestyle inayomwezesha kula na kubakisha savings kila mwezi.

2) Au Je, kama maisha ya swali hapo juu ni ubinafsi, unadhani ni sahihi kupunguza gharama za maisha yako ili ukubali kurudi nyuma kidogo ili kubakiza savings, ziweze kuwasaidia jamaa zako wanaokutegemea? Kama kweli tunataka kutekeleza msemo wa kwamba kutoa ni moyo na si utajiri..?

3) Je, jambo hilo namba 2 hapo juu ni practical in real sense?

Nini maoni yako? Karibu ku-share mawazo ili tuelimishhane..
 
Back
Top Bottom