Ukosoaji kwa serikali na majibu ya adhabu ya wakosoaji una tija katika misingi ya utawala bora!

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Tanzania inapitia kipindi kigumu cha mpito katika dhana ya uwajibikaji unao chagizwa na ukosoaji wa serikali na malipo ya wakosoaji toka serikalini.

Ibara ya 8 ya katiba ya JMT kwa ujumla wake imetoa uhalali wa madraka ya serikali yatatokana na mamlaka ya wananchi na serikali msingi wake mkuu ni ustawi kwa wananchi wake.

Ikiwa mamlaka na madaraka ya serikali yatatoka kwa wananchi kwanini sasa wenye mamalaka wamekuwa wakiwashughulikia walitoa madaraka na mamlaka hayo pindi utendaji mbovu wa serikali unapojadili kwa misingi ya ukosoaji.

Hakuna asiyejua kuwa janga la Taifa kwa sasa ni deni la taifa linakuwa kwa kasi sambamba na maendeleo finyu katika miradi ya maendeleo.

Taasisi ya kwanza kuliona jambo hili ni chombo cha uwakilishi wa wenye kutoa mamlaka na madaraka ya serikali(wananchi) kwa maana ya bunge kushugulikiwa na serikali kwa kauli ya aliyekuwa Spika wa Bunge Ndugai kuwa serikali inakopa sana kiasi nchi yetu itapigwa mnada, kila mmoja anajua saga alilokutana nalo Spika Ndugai.

Wengi walishangilia anguko la Ndugai,lakini hakuna aliyetazama kwa jicho la mwewe. Maanake anguko la Spika ni anguko la bunge kushindwa kuisimamia serikali na kuishauri bila kujali aina ya kauli iliyotolewa.

Bahati mbaya sana mihimili mmoja ukafanikiwa kuudhoofisha mhimili ambao ni chombo cha wananchi,maanake nini wananchi wanaotoa mamlaka na madaraka ya serikali wamewajibishwa kwa chombo chao kusindwa kusimama imara kuhahakisha bunge lina kuwa imara kusimamia matakwa ya wananchi kwa kuishauri na kuisimamia serikali.

Bunge,chombo cha uwakilishi wa wananchi kikageuzwa party caucus ya CCM kumsulubu kiti cha Spika. Hii kitaalamu wananchi wamedhoofishwa na kuwa wanyonge sana kuhoji utendaji wa serikali

Kwa mantiki hii separation of power iko wapi katika utekelezaji misingi ya utawala bora.

Je kuna haja ya kuendelea kuwa na bunge linaloweza kushugulikiwa na serikali na kuacha adhima ya bunge iliyo ainishwa kikatiba!! Tujadili kwa maslahi mapana ya Taifa letu
 
Ndungai hakutimuliwa Kwa sababu ya ukosoaji....
Ndungai katimuliwa Kwa kukosa nidham ...wapo wakosoaji..na hawaguswi....
Spika wa Bunge ambae ni mwanachama wa chama cha Mapinduzi ni mjumbe wa moja Kwa moja wa Cc ya chama...
Akafanye ukosoaji wake wote huko kwenye Cc....
Nje ya hapo ni utovu wa nidhamu...

Wewe unaweza kuita media kumkosoa mama yako au Baba yako?wakati mnaishi nyumba moja na ukiwa ndani huzungumzi chochote?

Mnaojaribu kumtetea Ndungai mnatia aibu
 
Ndungai hakutimuliwa Kwa sababu ya ukosoaji....
Ndungai katimuliwa Kwa kukosa nidham ...wapo wakosoaji..na hawaguswi....
Spika wa Bunge ambae ni mwanachama wa chama cha Mapinduzi ni mjumbe wa moja Kwa moja wa Cc ya chama...
Akafanye ukosoaji wake wote huko kwenye Cc....
Nje ya hapo ni utovu wa nidhamu...

Wewe unaweza kuita media kumkosoa mama yako au Baba yako?wakati mnaishi nyumba moja na ukiwa ndani huzungumzi chochote?

Mnaojaribu kumtetea Ndungai mnatia aibu


Ndungai hakutimuliwa Kwa sababu ya ukosoaji....
Ndungai katimuliwa Kwa kukosa nidham ...wapo wakosoaji..na hawaguswi....
Spika wa Bunge ambae ni mwanachama wa chama cha Mapinduzi ni mjumbe wa moja Kwa moja wa Cc ya chama...
Akafanye ukosoaji wake wote huko kwenye Cc....
Nje ya hapo ni utovu wa nidhamu...

Wewe unaweza kuita media kumkosoa mama yako au Baba yako?wakati mnaishi nyumba moja na ukiwa ndani huzungumzi chochote?

Mnaojaribu kumtetea Ndungai mnatia aibu
Utamaduni huu unaouzungumzia ndiyo unaipa serikali jeuri ya kuwaburuza wananchi,Bunge ni mhimili unaojitegema mbali na uccm,chombo hiki kinaendeshwa kwa kanuni na sheria za bunge na kwa mujibu wa Katiba ya JMT,Spika kuikosoa serikali ni sahihi bila kujali Uccm wake.
 
Utamaduni huu unaouzungumzia ndiyo unaipa serikali jeuri ya kuwaburuza wananchi,Bunge ni mhimili unaojitegema mbali na uccm,chombo hiki kinaendeshwa kwa kanuni na sheria za bunge na kwa mujibu wa Katiba ya JMT,Spika kuikosoa serikali ni sahihi bila kujali Uccm wake.


Spika kama angekuwa sio mwanachama wa CCM ingekuwa sahihi ...lakini vile vile kazi kubwa ya spika hata kama angekuwa sio mwanachama wa CCM ni kuwapa nafasi wabunge...sio yeye kuwa msemaji wa wabunge....
Kuwa spika hakukupi platform ya kupimana ubavu na serikali....

Alikuwa wapi wakati Magufuli anakopa Hadi benki binafsi?

Kukopa kaanza kuona wakati wa Samia?

Ndungai mnafiki atatatetewa na wasiokuwa na uelewa tu
 
Spika kama angekuwa sio mwanachama wa CCM ingekuwa sahihi ...lakini vile vile kazi kubwa ya spika hata kama angekuwa sio mwanachama wa CCM ni kuwapa nafasi wabunge...sio yeye kuwa msemaji wa wabunge....
Kuwa spika hakukupi platform ya kupimana ubavu na serikali....

Alikuwa wapi wakati Magufuli anakopa Hadi benki binafsi?

Kukopa kaanza kuona wakati wa Samia?

Ndungai mnafiki atatatetewa na wasiokuwa na uelewa tu
Kanuni ipi au sheria ipi inamkataza spika kuongea au kukosoa? Bunge si kwa maslahi ya ccm tu ni chombo cha uwakilishi wa wananchi,kwa mtazamo wa kiccm una haki ya kuhoji hilo unalo hoji lakini hakuna limit ya kumuuliza mtu alikuwa wapi wakati wa Magu.
 
Hapa ndipo umuhimu wa kuwa na spika asiyekuwa na chama unapokuja, ila simtetei Ndugai maana nae hajanyooka, ukiamua kunyooka nyooka siku zote.
 
Back
Top Bottom