UDSM tupunguzeni masifa sasa

UDSM tupunguzeni masifa sasa

Mwaka wa kwanza ndio ulivyo,utakuta wengi bado wamesuka,wana vaa nguo zao za kushonesha,kuna watu utakuta wamejikoki na suti nzito za kushonesha chini panaa,wasichana wanavaa zile skuna za kijijini na wanasalimia kwa kupiga magoti.Wana mabegi na makaunta book makubwa na rula na mikebe wameshanunua.
Sasa baada ya kupata boom utakuta wanakimbilia Kariakoo kununua jeans na suruali na vikoba vya begani.Baada ya miezi sita unaanza kutafuta nguo za kushona.Kuziona labda uvizie siku ya Jumapili.
Hahahaha
Waache vijana waji praud, mbona hata wa ifm, cbe, na TIA wanavaaga
 
ukinisoma between lines utajua nimemaanisha nini!
Binafsi nimefundishwa na baadhi ya hao wateule ni ukweli usiopingika wapo vizuri kuliko hawa wengine wanao ajiriwa kipindi hiki
Binafsi naona jpm anaiharibu udsm
Nimekupata mkuu. Kuna idara chuo kimoja imefanikiwa kutoa viongozi wa vyuo kama 6 kwa muda mfupi-sasa kazi hapo ni tia maji tia maji. Lakini wakubwa hawaoni na ukisema utaonekana huwatakii waheshimiwa mafanikio.
 
Sahani kidogo kwani sheria inasema wavae mwisho wapi? Kama hamna kikomo basi waacheni, ww kama unasoma IMTU basi vaa cha IMTU
 
Mwaka wa kwanza ndio ulivyo,utakuta wengi bado wamesuka,wana vaa nguo zao za kushonesha,kuna watu utakuta wamejikoki na suti nzito za kushonesha chini panaa,wasichana wanavaa zile skuna za kijijini na wanasalimia kwa kupiga magoti.Wana mabegi na makaunta book makubwa na rula na mikebe wameshanunua.
Sasa baada ya kupata boom utakuta wanakimbilia Kariakoo kununua jeans na suruali na vikoba vya begani.Baada ya miezi sita unaanza kutafuta nguo za kushona.Kuziona labda uvizie siku ya Jumapili.
Heshima yako Mkuu kwa uchambuzi huu
 
the worst thing ni kwamba, they have no any credible impact after three good years in the collage.

kwa mfano, bachelor in Kiswahili 🙄 🙄

its impact is actually likely to deem up to -0.0%.

utamkuta huyo kagangamara kama kisiki, udsm! udsm! udsm!

😀 😀
Mkuu sana, mada haikuwa huku but anyways ngoja nikupe mfano mmoja tu Wa wataalam Wa kiswahili kutoka UDSM na simaanishi kuwa vyuo vingine havina impact ila kwa kuwa issue on the table ni UDSM.

Point: mkataba Wa EPA uliosomwa Bungeni na Prof. Paramagamba Kabuni umetafsiriwa na IDARA YA TAALUMA ZA KISWAHILI( TATAKI ) UDSM. Huo ni mfano mmoja in million
 
Kuvaa hizo ID holder kwa lengo la kuwekea ID sio ujinga ila itakuwa ujinga kama wanavaa holders peke yake bila kuweka ID lakini ni ujinga zaidi kutaka vijana wasivae hizo holders kwa ajili ya lengo lilokusudiwa!

Mkuu, kuvaa hadi nje ya maeneo ya chuo au hostel?
Kila kitu kina wakati na mahala pake. Asiyezingatia ukweli huu ni mjinga na limbukeni tu.
 
Kwa namna linavyojadiliwa,hapana shaka suala hili lina 'maslahi ya umma'.Ninajaribu kujibu kutoka 'viatu' vya wanafunzi wanaolalamikiwa.Haitakuwa haki kumtaka mwanafunzi aishiye Mabibo Hostel avue ID mara atokapo Chuoni awe anatembea kwa miguu ama kwa usafiri wa gari.Hii ni kutokana na ukweli kwamba akifika getini Mabibo atalazimika kuonyesha ID.

Wale wanaoenda nazo Posta ama Kimara ama kwingineko,wanakabiliwa na changamoto ile ile:wanaporejea Hosteli ama Mabwenini Mlimani watapaswa kuzionyesha na kwa hiyo kwenda nazo mtaani inaweza kuwa sahihi.Ipo hoja ya kuzivua na kuziweka mfukoni mara watokapo getini.Hii nayo haitekelezeki kirahisi kwa sababu upo uwezekano wa kuibiwa ama kupotea na kusababisha usumbufu mkubwa kwa muhusika.Bila ID hawapati huduma na kuzipata inagharimu nishati,nguvu,muda na pesa.

Kwa sehemu kubwa wanafunzi husika wanazo sababu za msingi za kuvaa ID zao.Tujifunze kuvumiliana na kuchukuliana.Kabla ya kutafuta makosa elewa mazingira.
Hivi kuitoa mfukoni na kuionesha au kuivaa anapoingia maeneo anayotakiwa awe ameivaa kunachua muda gani?
Wafanyakazi huwa tunavaa tukiwa eneo la ofisi, tukitoka kidogo tu tunavua hivyo vitambulisho vyetu.
Kuning'iniza kitambulisho maeneo yasiyohitaji kitambulisho ni ulimbukeni.
 
Ndiyo maana mimi nayanyima lift huku njia ya baruti vitambulisho utadhani manamba wa mashamba ya mkoloni. Hasa mijidume unalikuta limenong'niza Id linadhani ujiko kumbr ushamba tu.
 
Wasukuma katika ubora wao wa kuvaa I.D CARD kila mahali,
Teh teh teh teh teh.......
 
Jina tu kichwani hakuna kitu. Hawa wanakuja sana field huku na huwa tunawashangaa sana.

Wakati wa muda wa kazi wao ni kuzunguka zunguka tu na laptops zao as if ni ma-secretary. Hakuna wanachokuja kujifunza zaidi ni kuja tu kazini kuja kuandika report na laptops zao. Facebook, WhatsApp na Instagram ndio vijiwe vyao.

Miaka yangu yote ya ku-interact na wanafunzi sijawahi kukutana na mwana UD ninaemwona anaweza kuwa Engineer wa kweli.

Jifunzeni kwa majirani zenu huko DIT na Mbeya. Hawa nawakubali sana na hata kwenye kazi wanajituma sana

Ndio maana mnapokuja kuomba kazi tunawaona ni wale wale. Sio kwamba mmelogwa bali mnajiloga wenyewe.

Ingekuwa na amri yangu nisingewapokea kabisa zaidi mnakuja kututia hasara ya vyakula tu.
 
Watu bahna, ule ni utambulisho wao. They are proud of! wacha wavae wanajikubali ni wanafunzi mbona askari anapita na nguo zake popote? Huo ni utambulisho kuwa yeye ni mwanafunzi sio dhambi. Wacha wafurahie wakati ukipita basi.
 
Acheni kufuatilia vitu vidogo vidogo, kuvaa au kutokuvaa ID nje ya neeo husika ni maamuzi ya mtu mwenyewe na wala haimpunguzii chochote mtu mwingine.
Ukiwa na fikra za kudharauliwa ndio utajiona upo chini kwa kila kitu.
Wapo watu wengi tunawaona na vitambulisho vyao njiani lakini hatuchukulii kama kujionyesha.
Na nadhani kutakuwa na utofauti wa kweli kwa UDSM ndio maan imekuuma.
Fanya yako kiongozi.
upungufu wa akili kichwanii.. soma uzi vizuri na pangua hoja zote kama sio masifa hayo ni nini,, ukweli wajulikana bana tubishe tuu UDSM TUNAJIONA HADI YAWA KERO KITU KIDOGO UDSM
 
shida
Ktk mazingira official ni lazima kuvaa id hata kama upo monchwari . kwenda nayo popote ni sawa inawasaidia sana wanafunzi wanapotoka lekcha za Usiku kurudi hostel ila wanaonenda nazo k,koo wamezidi ila kwa ubungo ni sawa tuu assume mtu katoka lekcha SAA 2 Usiku anaenda mabibo hostel kwa mguu akifika getini anatakiwa aivae tena shingoni sasa akiiacha mpka anaingia rum kwake kuna shida gani
ukweli ni kwamba zimeandikwa UDSM STUDENT sasa inawapa vichwa weng kuivaa muda wote nahisi hata ww unahak kau ugonjwa,,, tuacheni ujing wakujiona tukumbuke kuna maisha baada ya chuo hayo maisha hayatajali umesoma chuo gani
 
Back
Top Bottom