IDS-UDSM badilikeni

Lugumya

Senior Member
Apr 26, 2021
183
1,094
Taasisi ya IDS ya Chuo kikuu Cha Dar Es Salaam (UDSM), ninaomba kutumia jukwaa hili kuwaomba mbadilike hasa Kaimu Mkurugenzi wa Institute na Mratibu (Coordinator) wa Post-graduate Studies.

Nimeamua kuandika haya kutoka na ukweli kwamba mmekuwa mwiba mkali na kikwazo cha wanafunzi wa Masters na PhD kutomaliza kwa wakati. Usimamizi wenu umekuwa ni butu na usiokuwa na uungwana, wala kujali.

Baadhi ya changamoto ambazo ni kero ni pamoja na;
1. Mwanafunzi akisha-develop Mfano Research Proposal, na msimamizi wake (supervisor) akamruhusu akusanye, ikifika kwa coordinator na Mkurugenzi kwa ajili ya kuitwa kwenye presentation, lazima uchukue walau Miezi mitatu. Imagine Miezi mitatu, umekusanya research proposal mwezi Juni, unaitwa Kupresent October au November! Na siku hiyo kama supervisor wako hayupo, huwezi kufanya presentation hadi siku atakayokuwepo (hili ni utaratibu mpya).

2. Mwanafunzi akimaliza kuwasilisha Proposal, na baadae kukubaliana na msimamizi wake kukusanya kwa ajili ya kupata kibali Cha Utafiti (Research Clearence), hapo kasheshe ndo litakapoanza. Kibali hicho kwa sasa kinapatikana kwa mfumo (online).

Kasheshe lenyewe liko hivi;
(i). Mwanafunzi anaanzisha, akishaanzisha, anatuma proposal yake kwa supervisor, supervisor anatoa maoni yake, akishatoa maoni yake, hatua inayofuata ni kwa Coordinator, hapo kwa coordinator vumilia wiki 1 hadi 2 (kumbuka hapa ni kusema tu kama "sawa", au naridhia basi. Hayo maneno yanasubiri wiki.

Sasa kikitoka kwake kinaenda kwa Mkurugenzi wa Idara yaani Mkurugenzi wa Idara, hapo vumilia Miezi miwili au mitatu. Piga simu, tuma meseji jamaa wala haangaiki na wewe. Baada ya miezi miwili au mitatu ndo anaweza kukitoa.

Yaani mpaka ajisikie mwenyew, mwanafunzi atakula msoto akisubiri hisani ya le boss. Then, utasikia anasema master or PhD si mchezo unafikir Miezi 18 tu utakuwa umeimaliza?? Jamni, Sasa kwa nn mmeweka hiyo miezi, si iondoeni ijulikane tu kuwa muda haujulikani.

(ii). Mwanafunzi akitoka kukusanya data, akafanya analysis then Hadi mwisho akakubaliana na supervisor wake kukusanya, kimbembe kinaanza. Tarajia tena Miezi mitatu hadi minne ndo uitwe Kupresent findings. Yaani ni vurugu tupu.

Sasa utakuta mwanafunzi, labda ana ruhusa ya masomo, muda unaisha hata proposal hajapresent kisa tangu akamilishane na supervisor wake, bado kwenye idara hawajapanga tarehe ya kumuita muda unayoyoma mwisho wa siku muda unaisha mwanafunzi hajafanya chochote. Jambo ambalo si la uungwana!

KUHUSU ONLINE.

Ili mwanafunzi aweze kukusanya kazi yake mfano Proposal au Dissertation lazima iwe approved na supervisor, Coordinator na Director of institute. Na hawa unawapandia gari ili wakakusainie hizo nyaraka. Sasa mfumo ni online, niko huku Tandahimba, nipange superfeo kwenda Dsm kusainiwa hiyo form ya Approval afu sijui nirudi Tandahimba ndo niiscan na kuanza kutuma online! Online gani hiyo!

Hapo hapo, mwanafunzi akishasainiwa ndo anaiscan tena hiyo form na kuambatisha kwenye proposal au Dissertation ndo anaanza mchakato wa kuituma tena kwa Supervisor, huyo supervisor ambaye ameaprove manually anatumiwa tena ku-approve kwa kuweka comments, then atamfowadia Coordinator na Director, na kuendelea. Sasa sijui hii ni online gani hii jmn. Kwa nini mwanafunzi asipachike hiyo form, Wanafuata waweke scanned signature kwenye mfumo huko huko? Nini kinashindikana?

MALIPO YA EXTENSION

Hili ni kwa Chuo kizima. Watakuzungusha kote huko ikiwemo kukuharibia muda, lakini ile Miezi ikiisha wanakupa Miezi mitatu ya ziada, baada ya hiyo utatakiwa kulipa 25-50 elfu per month, hadi pale utakapohitimu. Wizi wa ajabu. Kama nyie ndo mmesababisha nalipaje extension?

Ushauri.
1. Coordinator na Director badilikeni. Ni vijana ambao mungeweza kuwa mfano wa kuigwa. Kama mnaona mna majukumu mengi hizo nafasi ziachieni. Waje ambao watajua kuwa hata jukumu la kushughulikia wanafunzi ni sehemu ya jukumu lao.

2. Kutengezwe ratiba ya presentation kwa mwezi walau na kwamba mwanafunzi akishakusanya kazi yake kwa ajili ya presentation au kibali basi isimalize mwezi na sehemu. Iwe ndani ya siku 30.

4. Online iwe kamili. Hizo taratibu za approval zifanyike online kweli. Mwanafunzi akishasaini yeye wengine wafanye online. Siyo mtu anaanza kutoka huko kote aliko kuja kukimbizana na wahadhiri wakti jambo lenyewe ni online. Haipendezi wasomi kuwa namna hii.

5. Majibu yenu yenye ukakasi na viburi hayajengi. Elewesheni watu kwa staha. Nafasi hizo ni mpito tu. Fanyeni kwa weledi na kuzingatia muda wa wenzenu (wanafunzi)pia.

Nawasilisha.
 
Vituo vya mwendokasi kuchana tickets nalo ni ajabu la karne
Pole sana. Teknolojia na uhalisia wa maisha ya kila siku ya mwafrika ni pasua kichwa
 
Pole sana ndugu, kwa kweli hiki chuo sio rafiki kwa watumishi, kuna muda unafika inabidi uamue ama urudi kituoni kwa kuwa muda umeisha au uache kazi umalizie masomo usiyojua yataisha lini.
 
Mimi nilishaapa sitasoma tena masters au phd bongo. Mara nyingi elimu ya juu bongo imekaa ki kukomoana zaidi kuliko kuwasaidia wanafunzi kujifunza. Hii ni matokeo ya roho mbaya tu waliyonayo wa bongo wengi wengi tu ( including ma lecturers wengi wengi tu ambao ni sehemu ya wa bongo).

Nilifikia uamuzi huo baada ya kauli nilizokutana nazo wakati nasoma BA. Kauli hizo ni pamoja na:-

* Kwenye kozi yangu msome sana. Atakayejitahidi sana atapata angalau karai lakini si zaidi ya hapo.

* Yaani mimi mwalimu wenu mwenyewe nilipata C, halafu wewe unataka upate A, itoke wapi?

* Kazi ya prof sio kukufanya uelewe bali kukuchanganya.

* Kwa kawaida kwenye kozi yangu, huwa nashika angalau shuttle moja. Na.k

Ukiona mwalimu anamwambia mwanafunzi maneno kama haya, wewe unamwelewaje?

Kuna nchi, unaweza kumtafuta supervisor, coordinator au director hata saa nane usiku na akakusaidia. Wako kwa ajili ya kusaidia wanafunzi na sio kuwakwamisha, mwishowe mwaka tu unatoboa masters.
 
Desanjo ni nyoko kijana mdogo sio muelewa taasisi imebaki na vijana malimbukeni wasio taka kuwa part ya changes very shame kwa kweli
Huyu Kijana hana sifa za kuwa Kiongozi kabisa! Sijui aliyemkaimisha hiyo nafasi, aliwazia nini? Ni moja wa binadamu wenye sifa ya kutojali wengine kabisa!
 
I feel your pain but sidhani kama wahusika wanaweza fanyia kazi maandishi haya, nachokushauri tumia njia nyingine yenye uhakika zaidi kuwasilisha malalamishi mhimu haya.
Umeshauri vizuri Mkuu. Lakini JF ni jeshi kubwa. Unaweza kuhisi si sehemu sahihi, lakini mwisho wa siku ikawa na impact kubwa kuliko internal procedures.
 
Mimi nilishaapa sitasoma tena masters au phd bongo. Mara nyingi elimu ya juu bongo imekaa ki kukomoana zaidi kuliko kuwasaidia wanafunzi kujifunza. Hii ni matokeo ya roho mbaya tu waliyonayo wa bongo wengi wengi tu ( including ma lecturers wengi wengi tu ambao ni sehemu ya wa bongo).

Nilifikia uamuzi huo baada ya kauli nilizokutana nazo wakati nasoma BA. Kauli hizo ni pamoja na:-

* Kwenye kozi yangu msome sana. Atakayejitahidi sana atapata angalau karai lakini si zaidi ya hapo.

* Yaani mimi mwalimu wenu mwenyewe nilipata C, halafu wewe unataka upate A, itoke wapi?

* Kazi ya prof sio kukufanya uelewe bali kukuchanganya.

* Kwa kawaida kwenye kozi yangu, huwa nashika angalau shuttle moja. Na.k

Ukiona mwalimu anamwambia mwanafunzi maneno kama haya, wewe unamwelewaje?

Kuna nchi, unaweza kumtafuta supervisor, coordinator au director hata saa nane usiku na akakusaidia. Wako kwa ajili ya kusaidia wanafunzi na sio kuwakwamisha, mwishowe mwaka tu unatoboa masters.
Waafrika ni kama tuna kalaana fulani hivi.

Dada angu alimshtakia kwa Mungu lecturer mmoja pale SUA, siku tatu tu yule mwamba alikata. Sister aliogopwa kama ukoma maana alimwambia kabisa mbele ya wenzake kuwa hili swala naenda kumshirikisha Mungu maana haiwezekani niteseke hivi kama vile hatma ya maisha yangu umeishika wewe.

Haya maisha ukikutana na vizingiti huku mwilini unahamishia vita rohoni la sivyo utapiga sana mark time.
 
Huyu Kijana hana sifa za kuwa Kiongozi kabisa! Sijui aliyemkaimisha hiyo nafasi, aliwazia nini? Ni moja wa binadamu wenye sifa ya kutojali wengine kabisa!
Hawa vijana wa Sasa wameharibu taasisi hasa baada ya kuondoka ma Prof wazoefu, imagine vijana hawawezi kutoa msaada kwa wanafunzi ni mwendo wa kukomoana tu loh.
 
Komaeni hivyo hivyo kule hao lecturers wanasema walipata PhD zao kwa machozi, jasho na damu na wanafunzi lazima wapitie kwenye tanuri la moto, tena ukiwa kijana mdogo unaambiwa unaharaka ya nini "by 23 mimi hata degree ya kwanza nilikuwa sina, wewe unataka masters ? life begins at 40"🤣
 
Komaeni hivyo hivyo kule hao lecturers wanasema walipata PhD zao kwa machozi, jasho na damu na wanafunzi lazima wapitie kwenye tanuri la moto, tena ukiwa kijana mdogo unaambiwa unaharaka ya nini "by 23 mimi hata degree ya kwanza nilikuwa sina, wewe unataka masters ? life begins at 40"
Kuna lecturer Tena mkuu wa taasisi alinambia hivo your too young to get a master's degree, so huna haraka ya ku graduate hata mwakani itapendeza Mimi mbona umri wako Niko bachelor. In short bongo wasomi hawaelimiki na hawawi problem solver Zaid ya ku create more problem.
 
Komaeni hivyo hivyo kule hao lecturers wanasema walipata PhD zao kwa machozi, jasho na damu na wanafunzi lazima wapitie kwenye tanuri la moto, tena ukiwa kijana mdogo unaambiwa unaharaka ya nini "by 23 mimi hata degree ya kwanza nilikuwa sina, wewe unataka masters ? life begins at 40"


Ulimbukeni tu.
 
Mimi nilishaapa sitasoma tena masters au phd bongo. Mara nyingi elimu ya juu bongo imekaa ki kukomoana zaidi kuliko kuwasaidia wanafunzi kujifunza. Hii ni matokeo ya roho mbaya tu waliyonayo wa bongo wengi wengi tu ( including ma lecturers wengi wengi tu ambao ni sehemu ya wa bongo).

Nilifikia uamuzi huo baada ya kauli nilizokutana nazo wakati nasoma BA. Kauli hizo ni pamoja na:-

* Kwenye kozi yangu msome sana. Atakayejitahidi sana atapata angalau karai lakini si zaidi ya hapo.

* Yaani mimi mwalimu wenu mwenyewe nilipata C, halafu wewe unataka upate A, itoke wapi?

* Kazi ya prof sio kukufanya uelewe bali kukuchanganya.

* Kwa kawaida kwenye kozi yangu, huwa nashika angalau shuttle moja. Na.k

Ukiona mwalimu anamwambia mwanafunzi maneno kama haya, wewe unamwelewaje?

Kuna nchi, unaweza kumtafuta supervisor, coordinator au director hata saa nane usiku na akakusaidia. Wako kwa ajili ya kusaidia wanafunzi na sio kuwakwamisha, mwishowe mwaka tu unatoboa masters.
Ni kweli kabisa. Wahadhiri wa Bongo huwa wanataka kuwaonyesha wanafunzi kwamba wamesoma sana badala ya kufundisha. Pili majigambo ya tambo za namna hiyo ni psychological, mara nyingi mhadhiri wa namna hiyo ana uelewa mdogo sana na njia pekee ya kujikinga na "vijana wajuaji wa siku hizi" ni kuanza kuwatisha from day one.

Hali ni tofauti kwenye vyuo vya wenzetu hasa Ulaya. Wahadhiri wanajutahidi sana kukutoa hofu na kuiona kozi kuwa ni kitu rahisi sana. Mwalimu mmoja aliwahi kuniambia kstika kozi ya electronic engineering kuwa hii ni kozi nzuri " it's like kissing a woman for the first time. Halafu wanajitoa kwa hali na mali kuhakikisha mwanafunzi ametimiza malengo ya kwa wakati. Master mwaka 1, PhD miaka 3.
 
Back
Top Bottom