Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Siku 34 zimepita tangu kesi ya Uhaini inayomkabili Mhe. Tundu Lissu isimame, hii ni baada ya ombi la mapitio lililofunguliwa na Jamhuri katika mahakama ya rufaa, ambayo halijapangiwa tarehe hadi leo.
1774917699995.jpg
 
KUTOKA KATIKATI YA KUTA ZA MAGEREZA UKONGA, ANAANDIKA TUNDU ATIPHAS LISU:

Mwaka 1988 mto Vaal huko Free State ulifurika na kujaza bwawa kubwa la kuzalisha umeme la Vaal Dam. Bwawa likazidiwa maji na kutapika. Sehemu kubwa ya maji yakaenda kuathiri mashamba ya makaburu huko Free State na Gauteng. Nyumba za wakulima wa kizungu zikabomoka, na vifo 11 vikaripotiwa.

Wakati huo kulikuwa na mapambano makali ya watu weusi kudai uhuru kutoka kwa makaburu. Baada ya makaburu kupata majanga hayo ya mafuriko, maelfu ya watu weusi walishangilia mitaani na wengine wakifanya sherehe kama ishara ya kushukuru "miungu" yao kwa kuwalipia kisasi.

Rais Pieter Willem Botha, mmoja wa Marais katili mno wa Kikaburu, akalaani kitendo cha Waafrika kushangilia vifo vya makaburu. Huyu ni yule aliyewahi kusema Waafrika hawana akili za kujitawala, wanapaswa kutawaliwa milele. Baada ya mafuriko hayo P.W Botha akasema serikali yake haitawavumilia walioshangilia vifo vya makaburu kwa sababu huo si ubinadamu.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama cha ANC, Walter Sisulu, akamjibu P.W Botha kwa maneno ambayo yanaishi hadi leo. Sisulu alisema:

"Kama makaburu hawaumizwi na vifo vya watu weusi, wasitegemee kwamba weusi wataumizwa na vifo vyao. Weusi wameuawa kinyama na makaburu, na wengine hawakupewa hata heshima ya kuzikwa; walifukiwa kwenye makaburi ya halaiki kama wanyama. Leo, makaburu wakifa wanataka weusi waomboleze? Huku ni kujipa haki kubwa kuliko hata malaika.

Hamuwezi kuua watu weusi, muwafukie kama mizoga, halafu mkifa nyie mnataka watu haohao wasikitike. Binadamu ni yule yule, awe mwenye ngozi nyeusi au nyeupe. Kama wewe kaburu unaumizwa na kifo cha kaburu mwenzako; unapaswa kuumizwa na kifo cha mtu mweusi pia. Kuwa mweupe au kuwa na madaraka hakukufanyi kuwa binadamu kuliko wengine. Utu wetu haupo kwenye rangi za ngozi zetu wala
1774918724007.jpg
vyeo vyetu.”
 
Niliwaambia hawa DPP na serikali wamekimbilia kwa Jaji Mkuu 😁 - Lissu kawabana kila kona kweli! Wameishiwa legal arguments!
Yaani ni vituko 🙄
Na niwaambie @ccmtanzania the only solution ili Taifa itulie ni #FreeTunduLissu na #SamiaMustGo
Mnachelewesha the inevitable! Na mtatekeleza tu haya!
Nasema #TutaelewanaTu
1775115196025.jpg
 
Tumebakiza siku chache Mhe. Tundu Lissu atimize mwaka mmoja tangu akamatwe Aprili 9, 2025.

Kwa sasa tuweke picha hii kwenye profile ya group.

Kwa baadae tutaeleza kinachofuata.

Loading......
1775321097281.jpg
 
Today is Tundu Lissu Arrest Day
It’s being one year since Samia Suluhu ordered his illegal detention
He remains behind bars while his trial has stalled
@UNHumanRights said his detention is illegal and the govt should release him IMMEDIATELY and compensate him - instead they continue to hold him
This is what an uncivilized barabaric authoritarian govt looks like!

Kiongozi wa nchi ambaye amepitia mengi na anaendelea kuteseka ila hajakata tamaa kuona uhuru, haki na usawa kwa wote!
Imetosha na mnajua hakuna kesi!
Muachieni Tundu Lissu
#FreeTunduLissu
1775724315095.jpg
1775724311764.jpg
1775724311764.jpg
1775724307993.jpg
1775724304365.jpg
 
Mwenyekiti wa baraza la vijana mkoa wa Kilimanjaro ameitaka mahakama kumuachilia huru mwenyekiti wa CHADEMA taifa Tundu Lissu akiddai kuwa Lissu anaonewa.
1775726750230.jpg
 
Back
Top Bottom